Jaweni na Upendo kwa Ajili ya Mungu | Muziki wa Akapela "Yasifu Maisha Mapya"

Haleluya! Twakushukuru na kukusifu Wewe, Mwenyezi Mungu! Kristo wa siku za mwisho ameonekana, akifanya kazi na kuzungumza miongini mwa wanadamu. Neno lake hutuhukumu, kutuadibu na kututakasa, likituongoza kwenye njia sahihi ya maisha ya binadamu.

Ukaribisheni Urejeaji wa Bwana Yesu | Sifa na Ibada “Mungu Ameleta Utukufu Wake Mashariki”

Mungu aliipa Israeli utukufu Wake kisha Akauhamisha mbali na pale, na kuwaleta Waisraeli na kuwaleta watu wote Mashariki. Mungu amewaelekeza wote kwenye mwanga ili waweze kuungana tena na kuwa pamoja na mwanga, wasilazimike kuutafuta tena, kuutafuta mwanga.

Je, Biblia ndiye Bwana, au ni Mungu? | “Bwana Wangu Ni Nani” ( Filamu za Injili )

Liu Zhizhong ni mzee katika kanisa moja la mtaani la nyumba nchini China. Amekuwa muumini kwa zaidi ya miaka 30, na amesisitiza bila kukoma kwamba “Biblia ni ufunuo wa Mungu,” “Biblia inamwakilisha Mungu, kuamini katika Mungu ni kuamini katika Biblia, kuamini katika Biblia ni kuamini katika Mungu.”

Karibu Kurudi kwa Bwana Yesu | Drama ya Muziki “ Kwaya ya Injili ya Kichina Onyesho la 19” | Haleluya

Mungu ametutunza daima–Yeye amesikiliza maombi yetu! Anajua tumekuwa tukitamani kurejea Kwake! Sasa kwa hakika Amerejea! Tunasubiri nini bado? Tafadhali endelea kutazama drama yenye muziki ya Kanisa la Mwenyezi Mungu—Kila Taifa Humwabudu Mungu wa Vitendo!

NYENDO ZA MATESO YA KIDINI NCHINI CHINA (Christian Videos) swahili

Wakristo wanaoteswa katika filamu hii ni watu kutoka kwa vikundi vya kidini na madhehebu tofauti ambao walitafuta ukweli, na ambao waliisikia sauti ya Mungu na hivyo wakarudi kwa Mwenyezi Mungu.

Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo siku-za-mwisho. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo siku-za-mwisho. Onyesha machapisho yote

Jumanne, 17 Septemba 2019

Wimbo Mpya wa Kuabudu 2019 | “Kristo wa Siku za Mwisho Ameleta Enzi ya Ufalme” (Swahili Gospel Song)


Wimbo Mpya wa Kuabudu 2019 | “Kristo wa Siku za Mwisho Ameleta Enzi ya Ufalme” (Swahili Gospel Song)

Yesu alipokuja katika ulimwengu wa mwanadamu, Akatamatisha Enzi ya Sheria, Alileta Enzi ya Neema. Mungu mara nyingine akakuwa mwili katika siku za mwisho. Akitamatisha Enzi ya Neema, Alileta Enzi ya Ufalme. Wote wanaokubali kupata mwili kwa Mungu kwa mara ya pili wataongozwa katika Enzi ya Ufalme na kupokea uongozi Wake. Baada ya mwanadamu kusamehewa dhambi zake, Mungu alirudi mwilini kumwongoza. Atamwongoza mwanadamu kuingia katika enzi mpya. Ameanza kazi ya hukumu ili kumleta mwanadamu katika ulimwengu wa juu zaidi. Wote wanaotii utawala Wake watavuna ukweli wa juu na baraka kuu. Ee wataishi katika mwangaza! Na kupata njia, ukweli, na uzima! Yesu alifanya kazi nyingi kati ya wanadamu. Ukombozi wa wanadamu wote ndio kazi aliyomaliza pekee. Aligeuka sadaka ya mwanadamu ya dhambi, lakini hakumwondolea mwanadamu tabia yake yote potovu, upotovu wote wa mwanadamu. Kumwokoa mwanadamu kutoka kwa Shetani kulimaanisha Yesu alilazimika kuchukua dhambi za mwanadamu, lakini kazi kubwa zaidi ya Mungu ilihitaji kumwondolea mwanadamu upotovu wa Shetani. Baada ya mwanadamu kusamehewa dhambi zake, Mungu alirudi mwilini kumwongoza. Atamwongoza mwanadamu kuingia katika enzi mpya. Ameanza kazi ya hukumu ili kumleta mwanadamu katika ulimwengu wa juu zaidi. Wote wanaotii utawala Wake watavuna ukweli wa juu na baraka kuu. Ee wataishi katika mwangaza! Na kupata njia, ukweli, na uzima! kutoka katika Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya
Unaweza Pia Kupenda : Wimbo wa Injili "Kiini cha Kristo Ni Mungu" | Differences Between the True Christ and False Christs

Jumatano, 26 Juni 2019

Maneno ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 111

Maneno ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 111

Mataifa yote yatabarikiwa kwa sababu Yako; watu wote watanikaribisha kwa shangwe na kunisifu kwa sababu Yako. Ufalme Wangu utafanikiwa na kukua, na utabaki milele. Hakuna mtu ataruhusiwa kuukanyaga na hakuna kitu kitaruhusiwa kuwepo ambacho hakikubaliani na Mimi, kwa sababu Mimi ni Mungu mwenye uadhama na asiyekosewa Mwenyewe. Sikubali mtu yeyote anihukumu na Sikubali mtu yeyote kutolingana na Mimi. Hili linatosha kuonyesha tabia Yangu na uadhama Wangu.

Jumapili, 19 Mei 2019

1. Kuna tofauti ipi kati ya maneno yaliyoonyeshwa na Bwana Yesu katika Enzi ya Neema na maneno yaliyoonyeshwa na Mwenyezi Mungu katika Enzi ya Ufalme?

V. Ni Lazima Mtu Ashuhudie Kipengele cha Ukweli Kuhusu Tofauti Kati ya Kazi ya Mungu ya Hukumu Katika Siku za Mwisho na Kazi Yake ya Ukombozi Katika Enzi ya Neema

1. Kuna tofauti ipi kati ya maneno yaliyoonyeshwa na Bwana Yesu katika Enzi ya Neema na maneno yaliyoonyeshwa na Mwenyezi Mungu katika Enzi ya Ufalme?


Aya za Biblia za Kurejelea:
Tubuni: kwa kuwa ufalme wa mbinguni u karibu” (Mathayo 4:17).
Na kwamba toba na msamaha wa dhambi vinapaswa kuhubiriwa katika jina lake miongoni mwa mataifa yote, kuanzia Yerusalemu” (Luka 24:47).
Bado ningali nayo mengi ya kuwaambieni, lakini hivi sasa hamwezi kuyavumilia. Hata hivyo, wakati yeye, Roho wa ukweli, atakapokuja, atawaongoza hadi kwenye ukweli wote: kwa maana hatazungumza juu yake mwenyewe; bali chochote atakachosikia, atakinena: na atawaonyesha mambo yajayo” (Yohana 16:12-13).
Na iwapo mtu yeyote atayasikia maneno yangu, na asiyaamini, Mimi sitamhukumu: kwa kuwa mimi sikuja ili niihukumu dunia, bali kuiokoa dunia. Yeye ambaye ananikataa mimi, na hayakubali maneno yangu, ana yule ambaye anamhukumu: neno hilo ambalo nimelisema, ndilo hilo ambalo litamhukumu katika siku ya mwisho” (Yohana 12:47-48).
Maneno Husika ya Mungu:
Kazi ya Yesu ilikuwa kwa ajili ya ukombozi wa mwanadamu na kusulubiwa tu. Kwa hivyo, hakukuwa na haja Kwake kusema maneno zaidi ili kumshinda mtu yeyote. Mengi ya yale Aliyomfundisha mwanadamu yalitolewa kutoka kwa Maandiko, na hata kama kazi yake haikuzidi Maandiko, bado Aliweza kutimiza kazi ya kusulubiwa. Yake haikuwa kazi ya neno, wala kwa ajili ya kumshinda mwanadamu, lakini kwa minajili ya kumkomboa mwanadamu. Yeye Alihusika kama dhabihu ya dhambi tu kwa mwanadamu, na hakuhusika kama chanzo cha Neno kwa mwanadamu.
kutoka katika “Maono ya Kazi ya Mungu (1)” katika Neno Laonekana katika Mwili
Wakati huo, Yesu alizungumza tu na wanafunzi Wake mfululizo wa mahubiri kwa Enzi ya Neema, kama jinsi ya kuweka vitendoni, jinsi ya kukusanyika pamoja, jinsi ya kuuliza kwa maombi, jinsi ya kuwatendea wengine, na mengineyo. Kazi Aliyoifanya ilikuwa hiyo ya Enzi ya Neema, na alielezea tu juu ya jinsi wanafunzi na waliomfuata wanapaswa kuweka vitendoni. Alifanya tu kazi ya Enzi ya Neema na hakuna hata moja ya siku za mwisho. Wakati Yehova aliandika sheria ya Agano la Kale kwa Enzi ya Sheria, mbona basi hakufanya kazi ya Enzi ya Neema? Mbona hakueleza wazi mapema kazi ya Enzi ya Neema? Hii haingekuwa ya manufaa kwa kukubali kwa mwanadamu? Alitabiri tu kwamba mtoto mchanga wa kiume angezaliwa na kuja mamlakani, lakini Hakutekeleza mapema kazi ya Enzi ya Neema. Kazi ya Mungu katika kila enzi ina mipaka ya wazi; Anafanya tu kazi ya enzi ya sasa na Hatekelezi hatua ifuatayo ya kazi mapema. Kwa njia hii tu kazi Yake ya kuwakilisha ya kila enzi inaweza kuletwa mbele. Yesu alizungumzia tu ishara za siku za mwisho, kuhusu jinsi ya kuwa mtulivu na jinsi ya kuokolewa, jinsi ya kutubu na kukiri, na pia jinsi ya kubeba msalaba na kuvumilia mateso; Kamwe hakuzungumza kuhusu jinsi mwanadamu katika siku za mwisho anapaswa kuingia ndani, ama jinsi ya kutafuta kukidhi matakwa ya Mungu.
kutoka katika “Ni Jinsi Gani Mwanadamu Ambaye Amemfafanua Mungu katika Dhana Zake Anaweza Kupokea Ufunuo wa Mungu?” katika Neno Laonekana katika Mwili
Hebu kwanza tuangalie katika kila sehemu ya “Ibada Mlimani.” Haya yote yanahusiana na nini? Yaweza kusemekana kwa uhakika kwamba haya yote yameinuliwa zaidi, yana uthabiti zaidi na karibu zaidi katika maisha ya watu kuliko taratibu zile za Enzi ya Sheria. Kuzungumza katika muktadha wa kisasa, yanahusiana zaidi na matendo halisi ya watu.
Hebu tusome maudhui mahususi ya yafuatayo: Mnafaa kuzielewa vipi hali hizi za heri? Ni nini mnachofaa kujua kuhusu sheria? Ghadhabu inafaa kufasiliwa vipi? Wazinzi wanafaa kushughulikiwa vipi? Ni nini kinachosemwa, na ni sheria aina gani zipo kuhusu talaka, na ni nani anayeweza kutalikiwa na ni nani asiyeweza kutalikiwa? Na je, viapo, jicho kwa jicho, kuwapenda adui zako, maagizo kuhusu sadaka, n.k? Mambo haya yote yanahusu kila kipengele cha matendo ya imani ya mwanadamu kwa Mungu, na ufuataji wao wa Mungu. Baadhi ya desturi hizi zinatumika leo, lakini bado yapo katika hali ya kimsingi kuliko mahitaji ya sasa ya watu. Kwa kiasi kikubwa uko katika hali ya kimsingi ambao watu wanakumbana nao katika kuamini kwao katika Mungu. Tangu wakati Bwana Yesu alianza kufanya kazi, Alikuwa tayari anaanza kufanya kazi kwa tabia ya maisha ya binadamu, lakini yalitokana na msingi wa sheria. Je, sheria na misemo kuhusu mada hizi ilikuwa na uhusiano wowote na ukweli? Bila shaka zilikuwa nao! Taratibu, kanuni na ibada zote zingine za awali katika Enzi ya Neema zilikuwa na uhusiano, na tabia ya Mungu na kile Alicho nacho na kile Alicho na bila shaka kwa ukweli. Haijalishi ni nini ambacho Mungu anaonyesha, kwa njia gani Anaonyesha, au Akitumia lugha gani, asili yake, na mwanzo wake, vyote vinatokana na kanuni za tabia Yake na kile Alicho nacho na kile Alicho. Hili halina kosa. Kwa hivyo ingawa haya mambo Aliyoyasema yanaonekana kuwa ya juujuu, bado hamwezi kusema kwamba mambo haya si ukweli, kwa sababu yalikuwa mambo ambayo yalikuwa ya lazima kwa watu katika Enzi ya Neema ili kuridhisha mapenzi ya Mungu na kutimiza mabadiliko katika tabia yao ya maisha. Unaweza kusema kwamba mambo yoyote yale katika ibada hayaambatani na ukweli? Huwezi! Kila mojawapo ya mambo haya ni ukweli kwa sababu yote yalikuwa mahitaji ya Mungu kwa mwanadamu; yote yalikuwa kanuni na mawanda yaliyotolewa na Mungu kuhusu namna ambavyo unaweza kuwa na mwenendo, na yanawakilisha tabia ya Mungu. Hata hivyo, kutokana na kiwango cha ukuaji wao katika maisha wakati huo, waliweza tu kukubali na kuyafahamu mambo haya. Kwa sababu dhambi ya mwanadamu ilikuwa bado haijatatuliwa, Bwana Yesu angeweza tu kuyatoa maneno haya, na Angeweza kutumia mafundisho mepesi kama hayo miongoni mwa aina hii ya upana ili kuwaambia watu wa wakati huo namna ambavyo walifaa kutenda, kile walichofaa kufanya, ndani ya kanuni na upana gani walifaa kufanya mambo, na vipi walivyofaa kuamini katika Mungu na kutimiza mahitaji Yake. Haya yote yaliamuliwa kulingana na kimo cha mwanadamu wakati huo. Haikuwa rahisi kwa watu wanaoishi katika sheria kuyakubali mafundisho haya, hivyo basi kile Alichofunza Bwana Yesu lazima kingebaki ndani ya mawanda haya.
kutoka katika “Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe III” katika Neno Laonekana katika Mwili
Maneno ambayo Mungu Alizungumza katika enzi hii ni tofauti na yale yaliyozungumzwa katika Enzi ya Sheria, na kwa hivyo, pia yako tofauti na maneno yaliyonenwa katika Enzi ya Neema. Katika Enzi ya Neema, Mungu hakufanya kazi ya neno, lakini Alieleza tu usulubisho ili kuwakomboa binadamu wote. Biblia inaelezea tu ni kwa nini Yesu alikuwa Asulubiwe, na mateso ambayo Alipitia kwenye msalaba, na jinsi mwanadamu anapaswa kusulubiwa kwa ajili ya Mungu. Katika enzi hiyo, kazi yote iliyofanywa na Mungu ilikuwa kuhusu usulubisho. Katika Enzi ya Ufalme, Mungu katika mwili Anazungumza maneno ili kushinda wale wote wanaomwamini. Huu ni, “Neno kuonekana katika mwili”; Mungu amekuja katika siku za mwisho ili kufanya kazi hii, ambayo ni kusema, Amekuja kutimiza umuhimu wenyewe wa Neno kuonekana katika mwili. Ananena tu maneno, na majilio ya ukweli ni chache. Hii ndiyo dutu kamili ya Neno kuonekana katika mwili, na wakati Mungu katika mwili Anaponena maneno Yake, huku ndiko kuonekana kwa Neno katika Mwili, na ni Neno kuja katika mwili. “Mwanzoni kulikuwa na Neno, na Neno alikuwa na Mungu, na Neno alikuwa Mungu, na Neno likawa mwili.” Hii (kazi ya kuonekana kwa Neno katika mwili) ni kazi ambayo Mungu atatimiza katika siku za mwisho, na ni sura ya mwisho ya mpango Wake mzima wa uongozi, kwa hivyo Mungu lazima Aje duniani na kudhihirisha maneno Yake katika mwili. Yale yanayofanywa leo, yale yatakayofanywa baadaye, yale yatakayotimizwa na Mungu, hatima ya mwisho mwanadamu, wale watakaookolewa, wale watakaoangamizwa, na mengine mengi—kazi hii ambayo lazima itimizwe mwishowe imesemwa wazi, na yote ni kwa ajili ya kutimiza umuhimu halisi wa Neno kuonekana kwa mwili. Amri za utawala na katiba ambayo ilipeanwa hapo awali, wale ambao wataangamizwa, wale watakaoingia katika mapumziko—maneno haya lazima yatimizwe. Hii ni kazi iliyotimizwa kimsingi na Mungu katika mwili katika siku za mwisho. Anawafanya watu waelewe kule ambako wale waliopangiwa na Mungu wanapaswa kuwa na wale wasiopangiwa na Mungu wanapaswa kuwa, jinsi ambavyo watu Wake na wana Wake watawekwa kwenye vikundi, ni nini kitaifanyikia Uyahudi, ni nini kitaufanyikia Misri—katika siku za usoni, kila mojawapo ya maneno haya yatatimizwa. Hatua za kazi za Mungu zinaharakishwa. Mungu hutumia neno kama mbinu ya kumfichulia mwanadamu kinachopaswa kufanyika katika kila enzi, kinachopaswa kufanywa na Mungu katika mwili wa siku za mwisho, na huduma Yake ambayo inapaswa kufanywa, na maneno haya ni kwa ajili ya kutimiza umuhimu hasa wa Neno kuonekana kwa mwili.
kutoka katika “Yote Yanafanikishwa Kupitia kwa Neno la Mungu” katika Neno Laonekana katika Mwili
Kile ambacho Nasema leo ni kuhukumu dhambi za watu na maovu yao; ni kulaani uasi wa watu. Udanganyifu na upotovu wao, na maneno na matendo yao, mambo yote ambayo hayako sambamba na mapenzi Yake yatapitia hukumu, na uasi wa watu unaamuliwa kuwa wenye dhambi. Ananena kulingana na kanuni za hukumu, naye anadhihirisha tabia Yake yenye haki kwa kuhukumu maovu yao, kulaani uasi wao, na kufichua nyuso zao zote mbaya.
kutoka katika “Jinsi Hatua ya Pili ya Kazi ya Ushindi Huzaa Matunda” katika Neno Laonekana katika Mwili
Kazi inayofanywa na Mungu katika enzi hii ni hasa ya kutoa maneno kwa ajili ya uzima wa mwanadamu, kuweka wazi hulka ya asili ya mwanadamu na tabia ya mwanadamu iliyoharibika, uondoaji wa dhana za kidini, fikra za kinjozi, mitazamo iliyopitwa na wakati, vilevile maarifa na utamaduni wa mwanadamu. Hii ni lazima iwekwe wazi na kusafishwa kupitia maneno ya Mungu. Katika siku za mwisho, Mungu Anatumia maneno na siyo ishara na maajabu ili kumfanya mwanadamu kuwa mkamilifu. Anatumia maneno Yake kumweka wazi mwanadamu, kumhukumu mwanadamu, kumwadibu mwanadamu, na kumkamilisha mwanadamu, ili katika maneno ya Mungu, mwanadamu aje kuona hekima na wema wa Mungu, na aje kuelewa tabia ya Mungu, ili kupitia maneno ya Mungu, mwanadamu aone matendo ya Mungu.
kutoka katika “Kuijua Kazi ya Mungu Leo” katika Neno Laonekana katika Mwili
Ikifika kwa neno “hukumu,” utawaza juu ya maneno ambayo Yehova alizungumza kila mahali na pia maneno ya kukaripia ambayo Yesu aliwaambia Mafarisayo. Ingawa maneno haya ni yenye ukali, sio hukumu ya Mungu kwa mwanadamu; maneno tu ambayo yamezungumzwa na Mungu katika mazingira tofauti, yaani, mandhari tofauti, maneno haya ni tofauti kabisa na yale maneno anayonena Kristo wakati Anamhukumu mwanadamu siku za mwisho. Katika siku za mwisho, Kristo anatumia ukweli tofauti kumfunza mwanadamu, kufichua kiini cha mwanadamu, na kuchangua maneno na matendo yake. Maneno haya yanajumuisha ukweli mbalimbali, kama vile wajibu wa mwanadamu, jinsi mwanadamu anavyofaa kumtii Mungu, jinsi mwanadamu anavyopaswa kuwa mwaminifu kwa Mungu, jinsi mwanadamu anavyostahili kuishi kwa kudhihirisha ubinadamu wa kawaida, na pia hekima na tabia ya Mungu, na kadhalika. Maneno haya yote yanalenga nafsi ya mwanadamu na tabia yake potovu. Hasa, maneno hayo yanayofichua vile mwanadamu humkataa Mungu kwa dharau yanazungumzwa kuhusiana na vile mwanadamu alivyo mfano halisi wa Shetani na nguvu ya adui dhidi ya Mungu. Mungu anapofanya kazi Yake ya hukumu, Haiweki wazi asili ya mwanadamu kwa maneno machache tu; Anaifunua, na kuishughulikia na kuipogoa kwa muda mrefu. Mbinu hizi za ufunuo, kushughulika, na kupogoa haziwezi kubadilishwa na maneno ya kawaida, ila kwa ukweli ambao mwanadamu hana hata kidogo. Mbinu kama hizi pekee ndizo huchukuliwa kama hukumu; ni kwa kupitia kwa hukumu ya aina hii pekee ndio mwanadamu anaweza kutiishwa na kushawishiwa kabisa kujisalimisha kwa Mungu, na zaidi ya hayo kupata ufahamu kamili wa Mungu. Kile ambacho kazi ya hukumu humletea mwanadamu ni ufahamu wa uso halisi wa Mungu na ukweli kuhusu uasi wake mwenyewe. Kazi ya hukumu humruhusu mwanadamu kupata ufahamu zaidi wa mapenzi ya Mungu, wa makusudi ya kazi ya Mungu, na wa mafumbo yasiyoweza kueleweka kwa mwanadamu. Pia inamruhusu mwanadamu kutambua na kujua asili yake potovu na asili ya upotovu wake, na pia kugundua ubaya wa mwanadamu. Matokeo haya yote huletwa na kazi ya hukumu, kwa maana asili ya kazi ya aina hii hasa ni kazi ya kuweka wazi ukweli, njia, na uhai wa Mungu kwa wale wote walio na imani ndani Mwake. Kazi hii ni kazi ya hukumu inayofanywa na Mungu.
kutoka katika “Kristo Hufanya Kazi ya Hukumu kwa Ukweli” katika Neno Laonekana katika Mwili
Ingawa neno “neno” ni rahisi na la kawaida, neno kutoka kwenye kinywa cha Mungu mwenye mwili hutikisa dunia nzima; neno Lake hubadilisha moyo wa binadamu, fikira na tabia zee za binadamu, na sura nzee ya ulimwengu mzima. Kupitia enzi nyingi, Mungu pekee wa leo ndiye anayefanya kazi katika njia kama hiyo, na ni Yeye tu Anayeongea na kumwokoa binadamu hivyo. Kuanzia wakati huu kuendelea, binadamu huishi katika mwongozo wa neno, wakichungwa na kuruzukiwa na neno. Binadamu wote wanaishi katika ulimwengu wa neno, wanaishi katika laana na baraka za neno la Mungu, na hata kuna binadamu zaidi wanaoishi chini ya hukumu na kuadibu kwa neno. Maneno haya na kazi hii vyote ni kwa minajili ya wokovu wa binadamu, kwa minajili ya kutimiza mapenzi ya Mungu, na kwa minajili ya kubadilisha sura asilia ya ulimwengu wa uumbaji wa kale. Mungu aliuumba ulimwengu kwa neno, huwaongoza wanadamu kote ulimwenguni kwa neno, na pia hushinda na kuwaokoa binadamu kwa neno. Hatimaye, Yeye atatumia neno ili kuutamatisha ulimwengu mzima wa kale. Ni hapo tu ndipo mpango wa usimamizi unapokuwa mkamilifu kabisa.
kutoka katika “Enzi ya Ufalme Ndiyo Enzi ya Neno” katika Neno Laonekana katika Mwili
Wakati huo, Yesu alifanya kazi kubwa ambayo haikueleweka kwa wanafunzi Wake, na kusema mengi kwamba watu hawakuelewa. Hii ni kwa sababu, wakati huo, Hakutoa maelezo. … Yesu hakuja kumkamilisha na kumpata mwanadamu, lakini kufanya awamu moja ya kazi: kuleta injili ya ufalme wa mbinguni na kukamilisha kazi ya kusulubiwa—na punde tu Yesu Aliposulubishwa, kazi Yake ilifika mwisho kamili. Lakini kwa awamu iliyoko sasa—kazi ya ushindi—maneno mengi zaidi lazima yasemwe, kazi nyingi zaidi lazima ifanywe, na lazima kuwe na hatua nyingi. Hivyo pia ni lazima siri za kazi ya Yesu na Yehova zitafichuliwa, ili wanadamu wote waweze kuwa na ufahamu na uwazi wa imani yao, kwa kuwa hii ni kazi ya siku za mwisho, na siku za mwisho ni mwisho wa kazi ya Mungu, wakati wa kuhitimisha kazi hii. Hii awamu ya kazi itakufafanulia sheria ya Yehova na ukombozi wa Yesu, na ni hasa ili uweze kuelewa kazi nzima ya mpango wa usimamizi wa Mungu wa miaka elfu sita, na kuelewa kusudi la kazi zote Alizozifanya Yesu na maneno Aliyoyasema, na hata upofu wako wa imani kwenye na katika ibada ya Biblia. Yote haya yatakuwezesha kujua. Wewe utakuja kufahamu kazi anayoifanya Yesu na kazi ya Mungu leo; utaelewa na kushuhudia ukweli wote, uzima, na njia. Katika awamu ya kazi Aliyoifanya Yesu, kwa nini Yesu Aliondoka bila kumaliza kazi ya Mungu? Kwa sababu awamu ya kazi ya Yesu haikuwa kazi ya kumalizia. Wakati Yeye Alisulubishwa msalabani, maneno Yake pia yalifika mwisho; baada ya kusulubiwa kwake, kazi Yake kwa hivyo ilimalizika. Awamu ya sasa ni tofauti. Ni baada tu ya maneno hayo kusemwa hadi mwisho na kazi nzima ya Mungu iwe imehitimika ndipo kazi yake itakapokuwa imemalizika. Wakati wa awamu ya kazi ya Yesu, kulikuwa na maneno mengi yaliyobakia bila kusemwa, au ambayo hayakuwa yameelezwa kikamilifu kwa ufasaha. Waama, Yesu hakujali Alichosema au kile ambacho hakusema, kwa kuwa huduma yake haikuwa huduma ya maneno; na hivyo baada ya Yeye kusulubishwa msalabani Aliondoka. Awamu hiyo ilikuwa hasa kwa ajili ya kusulubiwa, na ni tofauti na awamu ya sasa. Awamu ya kazi hii ni hasa kwa ajili ya kukamilisha, kufumbua, na kuleta kazi yote kwenye hitimisho. Kama maneno hayasemwi hadi tamati yake kabisa, hakutakuwa na mbinu ya kuhitimisha kazi hii, kwa kuwa awamu hii ya kazi yote inafikishwa mwisho na kukamilika kwa kutumia maneno. Wakati huo, Yesu Alifanya kazi kubwa isiyoeleweka na mwanadamu. Akaondoka kimyakimya, na leo bado kunao wengi wasioelewa maneno Yake, ambao ufahamu wao ni potofu lakini bado unaaminika nao kwamba ni sahihi, ambao hawajui kuwa wao si sahihi. Mwishoni, awamu hii ya sasa itafikisha kazi ya Mungu mwisho ulio kamilifu, na kutoa hitimisho Lake. Wote watakuja kufahamu na kujua mpango wa usimamizi wa Mungu. Dhana zilizo ndani ya mwanadamu, nia yake, fahamu yake potofu, dhana zake kuhusu kazi ya Yehova na Yesu, maoni yake kuhusu watu wa Mataifa mengine na michepuko yake ingine na makosa yake yatarekebishwa. Na mwanadamu ataelewa njia yote ya haki ya uzima, na kazi yote anayofanya Mungu, na ukweli wote. Wakati hayo yatafanyika, awamu hii ya kazi itafikia kikomo.
kutoka katika “Maono ya Kazi ya Mungu (2)” katika Neno Laonekana katika Mwili
Chanzo: Kanisa la Mwenyezi Mungu | Kondoo wa Mungu Huisikia Sauti ya Mungu

Jumapili, 12 Mei 2019

Matamshi ya Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee II Tabia ya Haki ya Mungu” Sehemu ya Kwanza


Matamshi ya Kristo wa Siku za Mwisho | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee II Tabia ya Haki ya Mungu” Sehemu ya Kwanza


Maneno ya Mungu katika video hii ni kutoka kitabu “Neno Laonekana katika Mwili”.
Maudhui ya video hii:
Kwa Kupinga Mungu kwa Ukaidi, Binadamu Anaangamizwa na Hasira za Mungu
Kupotoka kwa Sodoma: Kunakasirisha Binadamu, Kunaghadhibisha Mungu
Sodoma Yaangamizwa kwa Kukosea Hasira za Mungu
  Baada ya Ukinzani wa Mara kwa Mara wa Sodoma na Ukatili Wao Dhidi Yake, Mungu Anaufuta Kabisa

Tufuate: Asili ya Kanisa la Mwenyezi Mungu

Jumatano, 8 Mei 2019

Matamshi ya Kristo wa Siku za Mwisho | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee IX Mungu ni Chanzo cha Uhai kwa Vitu Vyote (III)” Sehemu ya Pili


Matamshi ya Kristo wa Siku za Mwisho | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee IX Mungu ni Chanzo cha Uhai kwa Vitu Vyote (III)” Sehemu ya Pili

Mwenyezi Mungu anasema, “Vitu vyote haviwezi kutenganishwa na kanuni ya Mungu, na hakuna mtu hata mmoja ambaye anaweza kujitenganisha kwenye kanuni Yake. Kupoteza kanuni Yake na kupoteza uangalizi wake kungekuwa na maana kwamba maisha ya watu, maisha ya watu katika mwili yangetoweka. Huu ndio umuhimu wa Mungu kuanzisha mazingira kwa ajili ya binadamu kuendelea kuishi.

Jumamosi, 13 Aprili 2019

Matamshi ya Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee VII” Sehemu ya Kwanza


Matamshi ya Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee VII ” Sehemu ya Kwanza

Maneno ya Mungu katika video hii ni kutoka kitabu “Neno Laonekana katika Mwili”. Maudhui ya video hii: Mhutasari wa Mamlaka ya Mungu, Tabia ya Haki ya Mungu, na Utakatifu wa Mungu

Yaliyopendekezwa: Matamshi ya Kristo wa Siku za Mwisho | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee VII” Sehemu ya Pili

Jumanne, 5 Machi 2019

Matamshi ya Kristo wa Siku za Mwisho | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee VIII Mungu ni Chanzo cha Uhai kwa Vitu Vyote (II)” Sehemu ya Kwanza

Matamshi ya Kristo wa Siku za Mwisho | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee VIII Mungu ni Chanzo cha Uhai kwa Vitu Vyote (II)” Sehemu ya Kwanza

Mwenyezi Mungu anasema, “Mungu aliumba vitu vyote na akatumia mbinu Zake kutunga sheria za ukuaji wa vitu vyote, na vilevile njia na mpangilio wa ukuaji wa vitu hivyo, na pia alitunga njia za kuwepo kwa vitu vyote duniani, ili viweze kuishi kwa kuendelea na kutegemeana.

Jumatatu, 11 Februari 2019

Kazi ya Hukumu katika Siku za Mwisho Ni kwa Ajili ya Kutamatisha Enzi

Kazi ya Hukumu katika Siku za Mwisho Ni kwa Ajili ya Kutamatisha Enzi

I
Siku za mwisho ni tofauti sana na Enzi ya Neema na Enzi ya Sheria.
Kazi ya siku za mwisho haifanywi katika Israeli,
lakini inatekelezwa kati ya Mataifa.
Ni ushindi wa mataifa yote mbele ya kiti cha enzi cha Mungu.
Na utukufu wa Mungu utajaza ulimwengu mzima.

Jumamosi, 9 Februari 2019

Nyimbo za dini | Kizazi cha Siku za Mwisho Kimebarikiwa

Nyimbo za dini | Kizazi cha Siku za Mwisho Kimebarikiwa
              I
Yote ni neema ya Mungu kwamba tunaweza kuona uzuri wa Mungu,
kwamba leo tunatafuta kumpenda,
kwamba tunataka kukubali
mafunzo ya ufalme wa wakati wetu.

Ijumaa, 8 Februari 2019

Ni Wale tu Ambao Wametakaswa Watakaoingia Katika Pumziko

I
Jamii ya wanadamu ya baadaye, ingawa imetoka kwa Adamu na Hawa,
haitaishi tena chini ya miliki ya Shetani,
lakini jamii ya waliookolewa, waliotakaswa.

Jumatano, 6 Februari 2019

Ni Wale tu Wenye Imani ya Kweli Hupata Kibali cha Mungu

I
Musa alipogonga mwamba na maji yakatoka,
zawadi kutoka Yehova, ilikuwa ni kwa imani.
Daudi alipocheza muziki kumsifu Yehova,
kama moyo wake ukijaa furaha, ilikuwa ni kwa imani.

Jumatano, 9 Januari 2019

Umeme wa Mashariki | Matamanio ya Pekee ya Mungu

I
Utukufu wa Yehova, ukombozi wa Yesu,
na matendo yote ya Mungu leo, ndiyo unayoyaona leo.
Maneno ya Roho wa Mungu umeyasikia,
Hekima Yake na ajabu Yake,
Tabia Yake umeijua,
Mpango Wake wa usimamizi umeambiwa.

Jumamosi, 22 Desemba 2018

"Nimewahi Treni ya Mwisho" (5) : Matokeo Yanayofikiwa na Kazi ya Mungu Aliyepata Mwili

"Nimewahi Treni ya Mwisho" (5) : Matokeo Yanayofikiwa na Kazi ya Mungu Aliyepata Mwili

Bwana Yesu alitabiri kwamba katika zile siku za mwisho, ngano itatenganishwa na matawi, kondoo na mbuzi, na watumishi wema kutoka kwa watumishi waovu.

Ijumaa, 14 Desemba 2018

Ufafanuzi wa Tamko la Ishirini na Saba

Leo, maneno ya Mungu yamefikia kilele chake, ambako ni kusema, sehemu ya pili ya enzi ya hukumu imefikia kilele chake. Lakini sio kilele cha juu kabisa. Wakati huu, sauti ya Mungu imebadilika, si ya kudhihaki wala ya ucheshi, na haigongi au kulaani; Mungu ametuliza sauti ya maneno Yake. Sasa, Mungu anaanza "kubadilishana maoni" na mwanadamu. Mungu anaendeleza kazi ya enzi ya hukumu na pia kufungua njia ya sehemu inayofuata ya kazi, ili sehemu zote za kazi Yake zipatane.!--more--> Kwa upande mmoja, Anasema kuhusu "ukaidi na uhalifu sugu wa mwanadamu," na kwa upande mwingine, Anasema "katika furaha na huzuni ya kutengana na kuunganika Kwangu na mwanadamu"— vyote viwili vinachochea mjibizo katika mioyo ya watu, na hata vinawasisimua walio sugu zaidi kati yao. Lengo la Mungu katika kusema maneno haya hasa ni kuwafanya watu wote waanguke chini mbele za Mungu, bila mnong'ono, mwisho kabisa, na baadaye tu "ndipo matendo Yangu hudhihirika, na kumfanya kila mmoja, katika upotovu wake, kunitambua Mimi." Ufahamu kuhusu Mungu wa watu wa kipindi hiki unasalia wa juujuu kabisa, sio ufahamu wa kweli. Ingawa wanajikakamua kadri wawezavyo, hawawezi kufikia mapenzi ya Mungu; leo, maneno ya Mungu yamefikia upeo wake, lakini watu wanabakia katika hatua za mwanzo, na hivyo hawawezi kuingia katika matamko ya sasa hivi—ambalo linaonyesha kuwa Mungu na mtu ni tofauti kabisa. Kulingana na hili, wakati maneno ya Mungu yatamalizika watu wataweza tu kufikia viwango vya chini zaidi vya Mungu. Hii ndio njia ambayo Mungu hufanya kazi ndani ya watu hawa ambao wamepotoshwa kabisa na joka kubwa jekundu, na Mungu lazima afanye hivyo ili Atimize matokeo bora kabisa. Watu wa makanisa huzingatia maneno ya Mungu kiasi kidogo zaidi, lakini nia ya Mungu ni kwamba waweze kumjua Mungu katika maneno Yake—je, tofauti haipo? Hata hivyo, jinsi mambo yalivyo, Mungu hajali tena kuhusu udhaifu wa mwanadamu, na Anaendelea kusema bila kujali kama watu wanaweza kukubali maneno Yake au la. Kulingana na nia Yake, wakati maneno Yake yatamalizika utakuwa wakati ambapo kazi Yake duniani itakamilika. Lakini kazi hii ni tofauti na ya zamani. Wakati matamko ya Mungu yatamalizika, hakuna mtu atakayejua; wakati kazi ya Mungu itafika mwisho, hakuna mtu atakayejua; na wakati umbo la Mungu litabadilika, hakuna mtu atakayejua. Hivyo ndivyo hekima ya Mungu ilivyo. Ili kuepuka mashtaka yoyote kutoka kwa Shetani na kuingiliwa kokote na nguvu za uhasama, Mungu hufanya kazi bila mtu yeyote kujua, na wakati huu hakuna mjibizo miongoni mwa watu wa dunia. Ijapokuwa ishara za kugeuka sura kwa Mungu zilizungumziwa wakati mmoja, hakuna mtu anayeweza kulitambua hili, kwa kuwa mwanadamu amesahau jambo hili, naye halizingatii. Na kwa sababu ya mashambulizi kutoka ndani na nje—maafa ya ulimwengu wa nje na kuchomwa na kutakaswa na maneno ya Mungu—watu hawako radhi tena kumfanyia Mungu kazi, kwa sababu wanashughulika sana na shughuli zao wenyewe. Wakati watu wote wanakana ufahamu na ufukuziaji wa zamani, wakati watu wote wamejiona kwa dhahiri, watashindwa na nafsi zao wenyewe hazitakuwa na nafasi tena mioyoni mwao. Wakati huo tu ndio watu watatamani maneno ya Mungu kwa kweli, wakati huo tu ndio maneno ya Mungu yatakuwa na nafasi kweli katika mioyo yao, na wakati huo tu ndio maneno haya yatakuwa yamekuwa chanzo cha kuwepo kwao—na wakati huu, mapenzi ya Mungu yatakuwa yametimizwa. Lakini watu wa leo wako mbali sana na hilo. Baadhi yao wameweza kusonga kwa shida, na hivyo Mungu anasema huu ni "ukaidi sugu."
Maneno yote ya Mungu yana maswali mengi. Kwa nini Mungu anaendelea kuuliza maswali kama hayo? "Mbona wasitubu dhambi zao na kuzaliwa mara ya pili? Mbona binadamu hupenda kuishi kwenye chemichemi badala ya kuishi mahali pasipo na matope? ..." Zamani, Mungu alifanya kazi kwa njia ya kuelezea mambo moja kwa moja au kuwa wazi moja kwa moja. Lakini baada ya watu kupitia maumivu mengi, hivyo Mungu hakuzungumza moja kwa moja. Kwa upande mmoja, watu wanaona kasoro zao wenyewe katika maswali haya, na kwa upande mwingine, wanafahamu njia ya kufanya mazoezi. Kwa sababu watu wote hupenda kufurahia matunda ya jasho la wengine, Mungu ananena kama yanavyostahili mahitaji yao, Akiwapa mada za kutafakari, ili waweze kuzitafakari. Hii ni hali moja ya umuhimu wa maswali ya Mungu. Kwa kawaida, huu sio umuhimu wa baadhi ya maswali Yake, kwa mfano: "Inawezekana kuwa Mimi Nimewadhulumu? Inawezekana kuwa Mimi Nimewapotosha? Inawezekana kuwa Mimi nimewaelekeza kuzimu?" Maswali kama haya huonyesha dhana zilizo katika vina vya mioyo ya watu. Ingawa midomo yao haisemi, kuna shaka ndani ya mioyo ya wengi wao, na wanaamini kwamba maneno ya Mungu yanawafafanua kama wasiokuwa na faida. Kwa kawaida, watu kama hao hawajijui, lakini hatimaye, watakubali kushindwa na maneno ya Mungu—hili haliepukiki. Kufuatia maswali haya, Mungu anasema pia "Nitasambaratisha mataifa yote, na hata familia ya mwanadamu." Watu wanapolikubali jina la Mungu, hivyo mataifa yote yatatetemeka, watu watabadili mawazo yao polepole, na katika familia mahusiano kati ya baba na mwana, mama na binti au mume na mke yatakoma kuwapo. Zaidi ya hayo, mahusiano kati ya watu katika familia yatakuwa ya kufarakana zaidi; watajiunga na familia kubwa, na ukawaida wa maisha ya takriban familia zote utatenganishwa. Na kwa sababu ya hili, dhana ya familia katika mioyo ya watu itazidi kuwa ya wasiwasi.
Kwa nini, katika maneno ya Mungu ya leo, mengi sana yametolewa kwa "kubadilishana hisia za moyoni" na watu? Kwa kawaida, hili pia ni kwa ajili ya kutimiza matokeo thabiti: likionyesha jinsi moyo wa Mungu umejaa wasiwasi. Mungu anasema, "Nionapo huzuni, nani anaweza kunifariji kwa moyo wake?" Mungu anasema maneno haya kwa sababu moyo Wake umelemewa na huzuni. Kwa sababu watu hawawezi kuyajali kabisa mapenzi ya Mungu, na daima huwa ni wapotovu, na hawawezi kujizuia—wanafanya wapendavyo; kwa sababu wao ni duni sana, na daima wao hujisamehe, na hawajali kuhusu mapenzi ya Mungu. Lakini kwa sababu watu wamepotoshwa na Shetani hadi leo, na hawawezi kujikomboa, Mungu anasema: "Wanawezaje kuepuka kutoka kwa midomo ya mbwa mwitu mlafi? Wanawezaje kujiokoa kutokana na tishio na majaribu yake?" Watu wanaishi katika mwili—katika kinywa cha mbwa mwitu mlafi. Kwa sababu ya hili, na kwa sababu watu hawajijui na daima wao hujiendeka na kujiingiza katika uzinzi, Mungu hana budi kuhisi wasiwasi. Kadri Mungu anavyowakumbusha watu hivyo, ndivyo wanavyohisi bora zaidi mioyoni mwao, na ndivyo wanavyokuwa radhi zaidi kushirikiana na Mungu. Wakati huo tu ndipo mwanadamu na Mungu watapatana, bila utengano wowote au umbali kati yao. Leo, wanadamu wote wanasubiri ujio wa siku ya Mungu, na kwa hiyo wanadamu hawajawahi kusonga mbele. Lakini Mungu anasema: "Wakati ambapo Jua la haki litaonekana, Mashariki itaangazwa, kisha litaangaza ulimwenguni kote, likimfikia kila mtu." Kwa maneno mengine, wakati Mungu atabadili umbo Lake, Mashariki itaangazwa kwanza na nchi ya Mashariki itakuwa ya kwanza kuchukua nafasi yake, baada ya hapo nchi zilizobaki zitafanywa upya kutoka kusini hadi kaskazini. Huu ndio utaratibu, na yote yatakuwa kwa mujibu wa maneno ya Mungu, na mara tu awamu hii itakapokuwa imekamilishwa watu wote wataona. Mungu hufanya kazi kulingana na utaratibu huu. Watakapoiona siku hii, watu watafurahi sana. Inaweza kuonekana kutoka kwa nia muhimu ya Mungu kwamba siku hii haiko mbali sana.
Katika maneno ya leo, sehemu ya pili na ya tatu zinachochea machozi ya uchungu kwa wote wanaompenda Mungu. Mioyo yao imegubikwa kivulini mara moja, na tangu wakati huu na kuendelea watu wote wamejaa huzuni kubwa mno kwa sababu ya moyo wa Mungu—baada tu ya Mungu kumaliza kazi Yake duniani, watahisi utulivu. Huu ni mwenendo wa kawaida. "Hasira inainuka ndani ya moyo Wangu, ikiandamana na hisia ya huzuni inayotapakaa. Wakati macho Yangu yanaangalia matendo ya watu na kila neno lao na kitendo kuwa vichafu, ghadhabu Yangu huzidi, na moyoni Mwangu kuna hali kubwa zaidi ya udhalimu wa ulimwengu wa mwanadamu, ambalo linanifanya kuwa na huzuni zaidi; Natamani kuumaliza mwili wa mwanadamu mara moja. Sijui kwa nini mwanadamu hawezi kujitakasa katika mwili, kwa nini mwanadamu hawezi kujipenda katika mwili. Yawezekana kwamba 'kazi' ya mwili ni kubwa sana?" Katika maneno ya Mungu leo, Mungu amemfichulia mwanadamu hadharani wasiwasi wote ulio ndani ya moyo Wake bila kuficha chochote. Wakati malaika wa mbingu ya tatu wanamchezea muziki na kumpigia vibati, Mungu bado anahisi kuwapenda watu walio duniani, na ni kwa ajili ya hili ndipo Anasema "Malaika wanapocheza muziki wakinisifu, hii inasisimua huruma kwa ajili ya binadamu. Ninajawa ghafla na huzuni moyoni Mwangu, na inakuwa vigumu kujiondoa katika hisia hii ya kuhuzunisha." Ni kwa sababu hii ndio Mungu anasema maneno haya: "Nitarekebisha udhalimu katika dunia ya mwanadamu. Nitafanya kazi Yangu kwa mikono Yangu mwenyewe ulimwenguni kote, Nikimkomesha Shetani asiwadhuru watu Wangu tena, Nikiwakomesha maadui wasifanye kile wapendacho tena. Nitakuwa Mfalme duniani na kukipeleka kiti Changu cha enzi huko, na kuwafanya maadui waanguke chini na kukiri makosa yao mbele Yangu" Huzuni ya Mungu inaongeza chuki Yake kwa pepo, na hivyo Anafichua mwisho wao kwa umati mapema. Hii ni kazi ya Mungu. Daima Mungu ametaka kuunganishwa tena na watu wote na kuimaliza enzi ya kale. Watu wote kotekote duniani wanaanza kusonga—ambalo ni kusema, watu wote chini ya dunia wanaingia katika uongozi wa Mungu. Kwa hiyo, mawazo yao yanageuka na kuwachukia wafalme wao. Punde si punde, watu wa dunia wataingia katika machafuko na wakuu wa nchi zote watakimbia kwenda kila upande, hatimaye watu wao watawaingiza kwenye bamba la kukata kichwa. Huu ndio mwisho kabisa wa wafalme wa pepo; hatimaye, hakuna mtu atakayeweza kutoroka, wote lazima waupitie. Leo, wale ambao ni "wajanja" wameanza kujiuzulu. Wanapoona kwamba mambo hayaonekani kuwa mazuri, wanatumia fursa hii kusalimu amri na kutoroka shida ya msiba. Lakini Nasema wazi, kazi ambayo Mungu anafanya katika siku za mwisho ni hasa kumwadibu mwanadamu, kwa hiyo watu hawa wangewezajekutoroka? Leo ni hatua ya kwanza. Siku moja, wote kotekote ulimwenguni wataingia katika ghasia ya vita, watu wa dunia hawatakuwa na viongozi tena, ulimwengu wote utakuwa kama rundo la mchanga uliochimbuliwa, usioongozwa na mtu yeyote, na watu watayajali tu maisha yao wenyewe, bila kumjali mtu mwingine yeyote, kwani kila kitu kinadhibitiwa na mkono wa Mungu—ndiyo maana Mungu anasema, "binadamu wote wanayagawanya mataifa kulingana na mapenzi Yangu." "Tarumbeta za malaika" ambazo Mungu anazungumzia sasa ni ishara, zinamwonya mwanadamu, na wakati tarumbeta zitalia mara nyingine, siku ya mwisho ya dunia itakuwa imefika. Wakati huo, kuadibu kote kwa Mungu kutaifika duniani kwa ukamilifu wake; hii itakuwa hukumu katili, na kuanza rasmi kwa nyakati za kuadibu. Miongoni mwa Waisraeli, mara nyingi kutakuwa na sauti ya Mungu ili kuwaongoza kupitia mazingira tofauti, na pia malaika wataonekana kwao. Waisraeli watakamilishwa katika miezi michache tu, kwa sababu hawatastahili kupitia hatua ya kuondoa sumu ya joka kubwa jekundu, itakuwa rahisi kwao kuingia kwenye njia sahihi chini ya aina mbalimbali ya uongozi. Kutokana na maendeleo yaliyo Israeli inaweza kuonekana hali ya ulimwengu wote, na hii inaonyesha jinsi hatua za kazi ya Mungu zilivyo za haraka. "Wakati umewadia! Nitaianza kazi Yangu, Nitatawala miongoni mwa wanadamu!" Zamani, Mungu alitawala tu mbinguni. Leo, Anatawala duniani; Mungu amechukua mamlaka Yake yote, na hivyo inatabiriwa kuwa wanadamu wote hawatakuwa tena na maisha ya kawaida ya binadamu, kwa kuwa Mungu atapanga upya mbingu na dunia, na hakuna mtu anaruhusiwa kuingilia. Hivyo, mara nyingi Mungu humkumbusha mwanadamu kuwa "wakati umewadia." Wakati Waisraeli wamekwisharudi katika nchi yao—siku ambayo nchi ya Israeli itakuwa imepatwa tena—kazi kubwa ya Mungu itakuwa imekamilika. Bila mtu yeyote kutambua, watu duniani kote wataasi, na nchi kotekote ulimwenguni zitaanguka kama nyota zilizo mbinguni; kufumba na kufumbua, zitakuwa magofu. Na baada ya kuwashughulikia, Mungu atajenga ufalme unaopendwa naye.
kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili 

Alhamisi, 22 Novemba 2018

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 22

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Mwenyezi Mungu,

Matamshi ya Mwenyezi MunguSura ya 22

Kumwamini Mungu si jambo rahisi kufanya. Ninyi mnajiboronga, mkiteketeza kila kitu mbele yenu mkifikiri kuwa haya yote ni ya kuvutia sana, matamu mno! Kuna baadhi ambao bado wanashangilia—wao tu hawana utambuzi katika roho zao. Ni vyema kuchukua muda wa kuuweka katika muhtasari uzoefu huu. Katika siku za mwisho, kila aina za pepo huibuka kutekeleza majukumu yao, wakikaidi kwa uwazi hatua za mbele za wana wa Mungu na kushiriki katika kuuvunja ujenzi wa kanisa.

Jumanne, 20 Novemba 2018

Neno la Mungu "Je, Kazi ya Mungu ni Rahisi Jinsi Mwanadamu Anavyodhania?" (Official Video)


Neno la Mungu "Je, Kazi ya Mungu ni Rahisi Jinsi Mwanadamu Anavyodhania?"(Official Video)

Mwenyezi Mungu anasema, "Unapaswa kuona kuwa mapenzi Yake na kazi Yake si rahisi kama ilivyokuwa katika kuumba mbingu na nchi na vyote vilivyomo. Kwa sababu kazi ya leo ni kubadilisha wale waliopotoshwa, wale waliokufa ganzi, na kutakasa walioumbwa kisha kushughulikiwa na Shetani, si kuumba Adamu na Hawa, ama hata kuumba mwanga, ama aina yote ya mimea na wanyama.

Alhamisi, 1 Novemba 2018

Maneno ya Roho Mtakatifu | "Kuijua Kazi ya Mungu Leo"


Maneno ya Roho Mtakatifu | "Kuijua Kazi ya Mungu Leo"

Mwenyezi Mungu anasema, "Kwa upande mmoja, Mungu katika mwili katika siku za mwisho Anaondoa nafasi iliyochukuliwa na Mungu asiye yakini katika dhana za mwanadamu, ili taswira ya Mungu asiye yakini isiwepo kabisa katika moyo wa mwanadamu. Kwa kutumia maneno Yake halisi na kazi Yake halisi, Anazunguka katika nchi zote, na kazi Anayoifanya miongoni mwa wanadamu ni halisi kabisa na ya kawaida, kana kwamba mwanadamu anakuja kujua uhalisia wa Mungu na Mungu asiye yakini Anapoteza nafasi Yake moyoni mwake. Kwa upande mwingine, Mungu Anatumia maneno yaliyozungumzwa na mwili Wake ili kumfanya mwanadamu mkamilifu, na kukamilisha vitu vyote. Hii ndiyo kazi ambayo Mungu Ataikamilisha wakati wa siku za mwisho."

Jumatano, 24 Oktoba 2018

Swahili Christian Skit | "Baba Yangu, Mchungaji" | A Debate on the Bible in a Family


Utambulisho


Swahili Christian Skit | "Baba Yangu, Mchungaji" | A Debate on the Bible in a Family

Chi Shou, mchungaji wa dini ambaye amekuwa muumini wa Bwana kwa miaka arubaini, daima ameshikilia mitazamo kwamba "maneno na kazi yote ya Bwana yako ndani ya Biblia," na kwamba "imani katika Bwana haiwezi kuacha Biblia, na kuiamini Biblia humaanisha kumwamini Bwana."

Swahili Christian Video "Bwana Anakuja Kwa Namna Gani Hasa?" | The Son of Man Has Come to Earth


Utambulisho


Swahili Christian Video "Bwana Anakuja Kwa Namna Gani Hasa?" (Mazungumzo Chekeshi) | The Son of Man Has Come to Earth

Katika siku za mwisho, hali ya moyo ya Wakristo wanaongoja kurudi kwa Bwana Yesu inakuwa kali sana, lakini ni kwa vipi, hasa, Bwana atarudi? Baadhi wanasema, "Bwana Yesu atakuja na mawingu." Wengine wanasema, "Unabii unaotabiri kurudi Kwake nao unasema, 'Tazama, mimi nakuja kama mwizi' (Ufu 16:15).

Jumanne, 23 Oktoba 2018

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Tamko la Mia Moja na Kumi

Matamshi ya Mwenyezi Mungu  | Tamko la Mia Moja na Kumi

Kila kitu kitakapofichuliwa utakuwa wakati ambapo Nitapumzika, na hata zaidi, utakuwa wakati ambapo kila kitu kitakuwa sawa. Mimi hufanya kazi Yangu binafsi; Mimi hupanga kila kitu na kusafidi kila kitu Mwenyewe. Nitakapotoka Sayuni na Nitakaporejea, wazaliwa Wangu wa kwanza watakapokuwa wamekamilishwa na Mimi, Nitakuwa Nimemaliza kazi Yangu kubwa. Katika mawazo ya watu kitu ambacho kinafanywa ni sharti kiweze kuonekana na kuguswa, lakini jinsi Ninavyoona, kila kitu ni kikamilifu wakati ambapo Ninafanya mpango Wangu.