Jaweni na Upendo kwa Ajili ya Mungu | Muziki wa Akapela "Yasifu Maisha Mapya"

Haleluya! Twakushukuru na kukusifu Wewe, Mwenyezi Mungu! Kristo wa siku za mwisho ameonekana, akifanya kazi na kuzungumza miongini mwa wanadamu. Neno lake hutuhukumu, kutuadibu na kututakasa, likituongoza kwenye njia sahihi ya maisha ya binadamu.

Ukaribisheni Urejeaji wa Bwana Yesu | Sifa na Ibada “Mungu Ameleta Utukufu Wake Mashariki”

Mungu aliipa Israeli utukufu Wake kisha Akauhamisha mbali na pale, na kuwaleta Waisraeli na kuwaleta watu wote Mashariki. Mungu amewaelekeza wote kwenye mwanga ili waweze kuungana tena na kuwa pamoja na mwanga, wasilazimike kuutafuta tena, kuutafuta mwanga.

Je, Biblia ndiye Bwana, au ni Mungu? | “Bwana Wangu Ni Nani” ( Filamu za Injili )

Liu Zhizhong ni mzee katika kanisa moja la mtaani la nyumba nchini China. Amekuwa muumini kwa zaidi ya miaka 30, na amesisitiza bila kukoma kwamba “Biblia ni ufunuo wa Mungu,” “Biblia inamwakilisha Mungu, kuamini katika Mungu ni kuamini katika Biblia, kuamini katika Biblia ni kuamini katika Mungu.”

Karibu Kurudi kwa Bwana Yesu | Drama ya Muziki “ Kwaya ya Injili ya Kichina Onyesho la 19” | Haleluya

Mungu ametutunza daima–Yeye amesikiliza maombi yetu! Anajua tumekuwa tukitamani kurejea Kwake! Sasa kwa hakika Amerejea! Tunasubiri nini bado? Tafadhali endelea kutazama drama yenye muziki ya Kanisa la Mwenyezi Mungu—Kila Taifa Humwabudu Mungu wa Vitendo!

NYENDO ZA MATESO YA KIDINI NCHINI CHINA (Christian Videos) swahili

Wakristo wanaoteswa katika filamu hii ni watu kutoka kwa vikundi vya kidini na madhehebu tofauti ambao walitafuta ukweli, na ambao waliisikia sauti ya Mungu na hivyo wakarudi kwa Mwenyezi Mungu.

Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Vitabu. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Vitabu. Onyesha machapisho yote

Jumamosi, 5 Oktoba 2019

Neno la Mungu: Sura ya 87

Neno la Mungu: Sura ya 87

Lazima uharakishe hatua na ufanye kile Nataka kufanya. Hii ni kusudi Langu lenye hamu kwenu. Inawezekana kuwa kwa wakati huu bado hamjaelewa maana ya maneno Yangu? Inawezekana kuwa bado hamjui kusudi Langu? Nimezungumza wazi zaidi na zaidi, na kusema mengi zaidi, lakini, je, ninyi hamjajitahidi kujaribu kuelewa maana ya maneno Yangu? Shetani, usifikiri kwamba unaweza kuharibu mpango Wangu! Wale wanaomtumikia Shetani, yaani, uzao wa Shetani (hii inahusu wale ambao wanamilikiwa na Shetani.Wale wanaomilikiwa na Shetani kwa hakika wana uhai wa Shetani, na kwa hivyo wanaitwa kuwa uzao wa Shetani) wanaomba rehema miguuni Pangu, wanalia na kusaga meno yao, lakini Siwezi kufanya kitu kama hicho cha kijinga! Ninaweza kumsamehe Shetani? Ninaweza kuleta wokovu kwa Shetani? Haiwezekani! Ninafanya kile Ninachosema na Siwezi kujuta kamwe!
Chochote Ninachosema kinakuja kutukia, si hivyo? Lakini ninyi bado kila mara hamniamini, mnashuku maneno Yangu, na kufikiri kwamba Ninawafanyia mzaha. Hiyo kwa kweli ya dhihaka. Mimi ni Mungu Mwenyewe! Mnaelewa? Mimi ni Mungu Mwenyewe! Ikiwa Sina hekima na sina nguvu, Ninaweza tu kufanya na kusema kama inavyonipendeza? Lakini bado hamniamini. Nimesisitiza mara kwa mara kwenu, na Nimewaambia mara kwa mara. Ni kwa nini wengi wenu bado hawaamini? Kwa nini bado mna mashaka? Kwa nini mnamshikilia kabisa mawazo yenu wenyewe? Yanaweza kukuokoa? Ninatenda kile ninachosema. Nimewaambia mara nyingi: Angalieni maneno Yangu kuwa ni ya kweli na msishuku. Je, mmechukulia maneno Yangu kwa uzito? Wewe peke yako huwezi kufanya chochote, lakini huwezi kuamini katika kile Ninachotenda. Ni nini kinaweza kusemwa juu ya mtu kama huyo? Kusema wazi wazi, ni kama kwamba Sikuwahi kuwaumba kamwe, ambayo ni kusema, wewe hujahitimu katika kila hali kuwa mtumishi Wangu. Kila mtu lazima aamini maneno Yangu! Wote wanapaswa kupitia jaribio—Sitamuacha mtu yeyote kukwepa. Bila shaka, hii ni isipokuwa wale wanaoamini. Watu wanaoamini maneno Yangu kwa hakika watapata baraka Yangu, ambayo utapewa kulingana na kile unachoamini, na itatimizwa ndani yako. Wana Wangu wazaliwa wa kwanza! Sasa, Ninaanza kuwapa baraka Zangu zote. Mtaanza kuvitupa vifungo vyote vinavyochukiza vya mwili kidogo na kidogo: ndoa, familia, kula, kuvaa, kulala, majanga yote ya asili (upepo, jua, mvua, dhoruba inayouma, shida ya kuanguka kwa theluji, na mambo mengine yote mnayochukia). Ninyi mtasafiri baharini, ardhini, na angani bila kuathiriwa na vizuio vya anga, wakati, au jiografia, kujifurahisha kikamilifu katika kumbatio Langu la upendo, mkiwa na wajibu juu ya kila kitu chini ya utunzaji Wangu wa upendo.
Ni nani asiyejivunia wana Wangu wazaliwa wa kwanza ambao Nimewafanya wakamilifu? Ni nani asiyelisifu jina Langu kwa ajili ya wana Wangu wazaliwa wa kwanza? Kwa nini sasa Ninataka kuwaonyesha siri nyingi sana? Mbona si katika wakati uliopita, lakini leo? Hii yenyewe pia ni siri, wewe unajua? Kwa nini Sikusema hapo nyuma kuwa China ni taifa Nilililolilaani? Na kwa nini Sikuwafichua wale wanaonitumikia? Leo Nawaambieni hili: Leo, kwa maoni Yangu, kila kitu kimetimilika—Ninasema hili kuhusu wana Wangu wazaliwa wa kwanza. (Kwa kuwa leo wana Wangu wazaliwa wa kwanza wametawala pamoja nami, sio tu kuoneka, lakini kwa kweli wanatawala pamoja nami. Kwa sasa, ni kwa yeyote ambaye Roho Mtakatifu anafanya kazi ndani yake ambaye kwa hakika anatawala pamoja nami, na hii inafichuliwa sasa, sio jana, wala kesho.) Leo Ninafichua siri zangu Zangu zote katika ubinadamu wa kawaida kwa sababu wale watu ambao Nataka kuwafichua wamefichuliwa, na hii ni hekima Yangu. Kazi Yangu imeendelea hadi hatua hii: Yaani, kwa wakati huu ni lazima Nitekeleze mpango wa maagizo ya utawala Niliyoamua juu ya wakati huu. Kwa hiyo, Ninawatunukia wana Wangu wazaliwa wa kwanza, wana, watu, na watumishi wa huduma muhuri unaofaa tu, kwa sababu Nina mamlaka na Nitahukumu na kutatawala kwa ukali. Ni nani anayethubutu kutonifanyia huduma kwa utii? Ni nani anayethubutu kunilalamikia? Ni nani anayethubutu kusema kwamba Mimi si Mungu wa haki? Najua, asili yenu ya kipepo imefichuliwa kwa muda mrefu mbele Yangu: Kwa yeyote Ninayekuwa mwema kwake, ninyi mnamwonea wivu na mnamchukia. Hii ni asili ya Shetani kabisa! Mimi ni mwema kwa wana Wangu—je, unathubutu kusema kuwa Mimi si mwenye haki? Naweza kukufukuza kabisa. Kwa bahati nzuri wewe unanifanyia huduma na sasa sio wakati; vinginevyo, Ningekuwa nimekufukuza!
Aina ya Shetani! Acheni kuwa washenzi! Msiseme tena! Msitende tena! Kazi Yangu imeanza kufanywa kati ya wana na watu Wangu waliochaguliwa, na tayari inaenea katika mataifa yote, makundi yote, madhehebu yote, na kazi zote za maisha nje ya China. Ni kwa nini wale wanaonipa huduma kila mara huzuiwa kiroho? Ni kwa nini hawaelewi kamwe mambo ya kiroho? Ni kwa nini kila mara Roho Yangu haifanyi kazi kwa watu hawa? Kwa ujumla, Siwezi kutumia nguvu nyingi sana juu ya wale ambao Sikuwaamulia kabla au kuwagua. Mateso Yangu yote ya awali, bidii Yangu ya kazi ya ulinzi imekuwa kwa wana Wangu wazaliwa wa kwanza na sehemu ndogo ya wana na watu, na zaidi ya hayo, pia wamekuwa kwa niaba ya kukamilika kwa ufanisi wa kazi Yangu ya baadaye, ili mapenzi Yangu yasizuiliwe. Kwa sababu Mimi ni Mungu Mwenye busara Mwenyewe, Nimepanga vizuri kila hatua. Mimi sijitahidi kwa vyoyote kubaki na mtu yeyote (hii inaelekezwa kwa wale ambao hawakuchaguliwa au kuamuliwa kabla), na Sitamuangusha mtu yeyote kwa bahati (hii inaelekezwa na waliochaguliwa na kuamuliwa kabla): Hii ni amri Yangu ya utawala, ambayo hakuna mtu anayeweza kuibadilisha! Kwa wale ambao Ninawachukia, Mimi ni mkatili; kwa wale Ninaowapenda, Ninawalinda na kuwahifadhi. Kwa hiyo, Ninatenda kile Ninachosema (Ninaowachagua, wamechaguliwa; Ninaowaamulia kabla, wameamuliwa kabla; haya ni mambo Yangu ambayo Nimeyapanga kabla ya uumbaji).
Nani anaweza kubadilisha moyo Wangu? Isipokuwa Mimi kufanya kulingana na mipango Ninayofanya Nitakavyo, ni nani anathubutu kutenda kwa pupa na kutotii amri Yangu? Hizi ni amri Zangu za utawala, na ni nani anayethubutu kuondoa moja yao kutoka Kwangu? Wote lazima wawe katika amri Yangu. Watu wengine wanasema, mtu huyo ameteseka sana, na ni mwaminifu na anafikiria moyo Wangu kabisa, lakini kwa nini hakuchaguliwa? Hii pia ni amri Yangu ya utawala. Nikisema mtu anaupendeza moyo Wangu, basi mtu huyo anaupendeza moyo Wangu na ni yule Ninayempenda; Nikisema kwamba mtu ni mtoto wa Shetani, basi mtu huyo ni yule Ninayemchukia. Usimpendekeze mtu yeyote! Je, unaweza kumng’amua? Haya yote yanaamuliwa na Mimi. Mwana ni mwana daima, na Shetani ni Shetani daima, ambayo ni kusema, asili ya mwanadamu haibadiliki. Isipokuwa Mimi Niwafanye wabadilike, wote watafuata aina yao wenyewe na hawawezi kamwe kubadilika!
Ninafichua siri Zangu kwenu kazi Yangu inavyoendelea. Leo, kazi Yangu imeendelea hadi hatua gani, je, mnajua kwa kweli? Je, mtafuata kwa kweli uongozi wa Roho Wangu kufanya kile Ninachofanya na kusema kile Ninachosema? Ni kwa nini Nasema kuwa China ni taifa ambalo Nimelilaani? Kwanza, Niliwaumba Wachina wa leo kwa sura Yangu. Hawakuwa na roho, na mwanzoni wao walipotoshwa na Shetani na hawangeweza kuokolewa. Kwa hivyo Niliwakasirikia watu hawa na nikawalaani. Ninawachukia watu hawa zaidi, na Ninakasirika wanapotajwa kwa sababu ni watoto wa joka kubwa jekundu. Kutokana na hili mtu anaweza kufikiria wakati ambapo nchi za dunia zimetwaa kwa nguvu China. Bado ni vivyo hivyo leo, na yote imekuwa laana Yangu—hukumu Yangu yenye nguvu zaidi dhidi ya joka kubwa jekundu. Hatimaye, Nikawaumba aina nyingine ya watu, ambao pamoja nao Niliwaamulia kabla wana Wangu wazaliwa wa kwanza, wana, watu, na wale wanaonifanyia huduma, kwa hivyo kile Ninachofanya leo Nilipanga kitambo kufanya. Kwa nini wale walio katika mamlaka nchini China wanatesa mara kwa mara na kuwadhulumu ninyi? Ni kwa sababu joka kubwa jekundu halifurahii laana Yangu na ananipinga. Lakini ni chini ya aina hii ya mateso na tishio hasa kwamba Mimi huwakamilisha wana Wangu wazaliwa wa kwanza kurudisha mashambulio dhidi ya joka kubwa jekundu na watoto wake. Baadaye Nitawaainisha. Baada ya kusikiliza maneno Yangu, je, mnaelewa umuhimu wa kuwaruhusu kutawala pamoja nami? Ninaposema kwamba joka kubwa jekundu limesononeshwa kabisa hadi kifo chake, pia ni wakati wana Wangu wazaliwa wa kwanza watawale pamoja nami. Mateso ya joka kubwa jekundu ya wana Wangu wazaliwa wa kwanza hutoa huduma sana Kwangu, na wakati wana Wangu wanapokua na wanaweza kusimamia masuala ya nyumba Yangu, basi watumishi waovu (watenda huduma) wataondolewa. Kwa sababu wana Wangu wazaliwa wa kwanza watakuwa wakitawala pamoja nami na watakuwa wametimiza makusudi Yangu, Nitawasukuma watenda huduma mmoja baada ya mwingine kwenye ziwa la moto na kibiriti: Kwa vyovyote vile wanapaswa kwenda! Ninafahamu kikamilifu kwamba aina ya Shetani pia anataka kufurahia baraka Zangu, na hataki kurudi chini ya miliki ya Shetani, lakini Nina amri Zangu ya utawala ambazo kila mtu lazima azingatie na ambazo zinapaswa kutekelezwa, na hakuna mtu anayeachiliwa. Baadaye, Nitawaambieni amri Zangu za utawala moja baada ya nyingine, msije kukosea.

Jumatano, 2 Oktoba 2019

Sauti ya Mungu: Sura ya 88

 Sauti ya Mungu: Sura ya 88

Watu hawawezi tu kuwaza kiasi ambacho mwendo Wangu umezidisha kasi: Ni ajabu ambayo imetokea isiyoeleweka kwa mwanadamu. Tangu uumbaji wa dunia, mwendo Wangu umeendelea na kazi Yangu haijawahi kusimama. Ulimwengu wote hubadilika siku kwa siku na watu pia wanabadilika mara kwa mara. Hizi zote ni kazi Zangu, mipango Yangu yote na hata zaidi, usimamizi Wangu—hakuna mtu anayejua au kuelewa hivi vitu.

Jumapili, 29 Septemba 2019

Maneno ya Mungu : Sura ya 89

Maneno ya Mungu : Sura ya 89

Sio rahisi kuwa sawa na makusudi Yangu kwa kila kitu unachofanya; sio jambo la kujilazimisha kudanganya, lakini inategemea ikiwa Nilikujalia na akili Yangu kabla ya kuumbwa kwa dunia, ambalo lilikuwa jukumu Langu. Hiki sio kitu watu wanachoweza kufanya.

Jumamosi, 14 Septemba 2019

Maneno ya Mungu : Sura ya 90

Maneno ya Mungu : Sura ya 90

Wote walio vipofu lazima waondoke kutoka Kwangu na wasiwepo kwa muda zaidi hata kidogo, kwani wale ambao Nataka ni wale ambao wanaweza kunijua, wanaoweza kuniona na wanaoweza kupata vitu vyote kutoka Kwangu. Na wanaoweza kweli kupata vitu vyote kutoka Kwangu ni nani? Hakika kuna wachache sana wa mtu wa aina hii na hakika watapata baraka Zangu.

Jumatano, 11 Septemba 2019

Sauti ya Mungu : Sura ya 91

Sauti ya Mungu : Sura ya 91

Roho Wangu huongea na kutamka sauti Yangu daima—wangapi kati yenu wanaweza kunijua Mimi? Kwa nini lazima Nipate mwili na kuja kati yenu? Hili ni fumbo kubwa. Ninyi mnanifikiria kuhusu Mimi na kunitamani sana siku nzima, na mnanisifu, kunifurahia na kunila na kuninywa kila siku, na ilhali leo bado hamnijui Mimi.

Jumapili, 8 Septemba 2019

Sauti ya Mungu : Sura ya 92

Sauti ya Mungu : Sura ya 92

Kila mmoja anaweza kuuona uweza Wangu na hekima Yangu ndani ya maneno Ninayoyazungumza na mambo Ninayoyatenda. Popote Ninapokwenda, kazi Yangu iko pale. Hatua Zangu haziko nchini China pekee, bali muhimu zaidi, ziko katika mataifa yote ya dunia. Ya kwanza kulipokea jina hili, hata hivyo, ni mataifa saba tu ambayo yamezungumziwa hapo awali, kwani hizi ni hatua za kazi Yangu, na hivi karibuni mtaweza kufahamu kabisa kuihusu na mtaielewa kabisa.

Alhamisi, 5 Septemba 2019

Sauti ya Mungu : Sura ya 93

Sauti ya Mungu : Sura ya 93

Ukweli unatimizwa mbele ya macho ya mtu na mambo yote yametimizwa. Kazi Yangu inapata hatua, ikipanda juu kama roketi iliyofyatuliwa, ambayo hakuna mtu aliwahi kutarajia. Ni baada ya vitu kufanyika ndipo mtaelewa maana ya kweli ya maneno Yangu. Watoto wa joka kubwa jekundu si wa pekee na lazima wafanywe kushuhudia matendo Yangu ya ajabu kwa macho yao wenyewe.

Jumatatu, 2 Septemba 2019

Maneno ya Mungu : Sura ya 94

Maneno ya Mungu : Sura ya 94

Narudi Sayuni pamoja na wazaliwa Wangu wa kwanza—kweli mnaelewa maana ya kweli ya maneno haya? Nimewakumbusha tena na tena kwamba Mimi nataka mkue haraka ili mtawale na Mimi. Je, mnakumbuka? Vitu hivi vyote vinahusiana moja kwa moja na kupata mwili Kwangu. Kutoka Sayuni Nilikuja duniani katika nyama ili Nipate kupitia nyama kundi la watu ambao ni wa akili moja na Mimi, na kisha turudi Sayuni.

Ijumaa, 30 Agosti 2019

Sauti ya Mungu : Sura ya 95

Sauti ya Mungu : Sura ya 95

Watu hufikiri kila kitu kuwa rahisi sana, wakati kwa kweli hali siyo hivyo. Ndani ya kila kitu kuna siri zilizofichwa, na vile vile hekima Yangu na mipango Yangu. Hakuna utondoti usioangaliwa, na yote yanapangwa na Mimi Mwenyewe. Hukumu ya siku kuu inawafikia wale wote wasionipenda kwa kweli (kumbuka, hukumu ya siku kuu inalenga kila mtu anayepokea jina hili) na kuwasababisha kulia na kusaga meno.

Jumanne, 27 Agosti 2019

Sauti ya Mungu : Sura ya 96

Sauti ya Mungu : Sura ya 96

Nitamwadibu kila mtu aliyezaliwa kutoka Kwangu ambaye bado hanijui ili kuonyesha ghadhabu Yangu yote, kuonyesha nguvu Zangu kuu, na kuonyesha hekima Yangu kamili. Ndani Yangu kila kitu ni chenye haki na bila shaka hakuna udhalimu, hakuna udanganyifu, na hakuna upotovu; yeyote ambaye ni mpotovu na mdanganyifu lazima awe ni mwana wa jahanamu—lazima amezaliwa huko kuzimu. Ndani Yangu kila kitu ni cha wazi; chochote Ninachosema kukamilisha kinakamilika na chochote Ninachosema kuanzisha kinaanzishwa, na hakuna mtu anayeweza kubadilisha au kuiga mambo haya kwa sababu Mimi ndimi Mungu Mwenyewe wa pekee.

Jumamosi, 3 Agosti 2019

Maneno ya Mungu | Sura ya 97

Maneno ya Mungu | Sura ya 97

Nitafanya kila mtu aone matendo Yangu ya ajabu na kusikia maneno Yangu ya hekima. Ni lazima iwe kila mtu na ni lazima iwe juu ya kila suala. Hii ni amri Yangu ya utawala na ni ghadhabu Yangu. Nitahusisha kila mtu na kila jambo ili watu wote kutoka mwisho mmoja wa ulimwengu hadi mwingine wataona kwa macho yao wenyewe, la sivyo Sitaacha kamwe.

Jumapili, 28 Julai 2019

Sauti ya Mungu | Sura ya 98

Sauti ya Mungu | Sura ya 98

Mambo yote yatakuja juu ya kila mmoja wenu, na yatawawezesha kujua zaidi juu Yangu na kuwa na uhakika zaidi juu Yangu. Yatawawezesha kunijua, Mungu mmoja Mwenyewe, kunijua Mimi Mwenye uweza, kunijua Mimi Mungu Mwenyewe mwenye mwili. Baadaye, Nitatoka katika mwili, Nirudi Sayuni, Nirudi katika nchi nzuri ya Kanaani, ambayo ni makazi Yangu, ndiyo hatima Yangu, na ndio msingi ambao niliumba vitu vyote.

Jumatatu, 22 Julai 2019

Sauti ya Mungu | sura ya 99

Sauti ya Mungu | sura ya 99

Kwa sababu mwendo wa kazi Yangu unaongeza kasi, hakuna anayeweza kuenda mwendo sawa na nyayo Zangu, na hakuna anayeweza kupenya akili Yangu, lakini hii ndiyo njia tu ambayo lazima isafiriwe. Hii ni “wafu” yaani wakati Ninapoongea kuhusu kufufuliwa kutoka kwa wafu (inarejelea kukosa uwezo wa kufahamu mapenzi Yangu, kukosa uwezo wa kuelewa kile Ninachomaanisha kutoka kwa maneno Yangu. Haya ni maelezo mengine ya “wafu”, na hayamaanishi kutelekezwa na Roho Wangu).

Ijumaa, 19 Julai 2019

Maneno ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 100

Maneno ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 100

Ninawachukia wale wote ambao hawajajaaliwa na kuchaguliwa na Mimi. Kwa hiyo ni lazima Niwafukuze watu hawa kutoka katika nyumba Yangu mmoja baada ya mwingine, hivyo hekalu Langu litakuwa takatifu na bila doa, nyumba Yangu itakuwa mpya daima na haitakuwa nzee kamwe, jina Langu takatifu litaenezwa milele na watu Wangu watakatifu watakuwa wapendwa Wangu. Aina hii ya mandhari, aina hii ya nyumba, aina hii ya ufalme ni lengo Langu, makao Yangu nayo ni msingi wa uumbaji Wangu wa vitu vyote.

Jumanne, 16 Julai 2019

Maneno ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 101

Maneno ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 101

Sitakuwa mwenye huruma kwa yeyote anayeingilia usimamizi Wangu ama anayejaribu kuiharibu mipango Yangu. Kila mtu anapaswa kuelewa kile Ninachomaanisha kutoka kwa maneno Ninayosema na lazima aelewe vizuri kile Ninachozungumzia. Kwa kuzingatia hali iliyopo, kila mtu anapaswa kujichunguza: Ni wajibu gani unaotekeleza? Unaishi kwa ajili Yangu, au unamtumikia Shetani? Je, kila moja ya matendo yako hutoka

Jumamosi, 13 Julai 2019

Maneno ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 102

Maneno ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 102

Nimeongea hadi kwa kiwango fulani na kufanya kazi hadi kwa kiwango fulani; ninyi nyote mnapaswa kuelewa mapenzi Yangu na kwa viwango tofauti muweze kuzingatia mzigo Wangu. Sasa ndicho kipindi muhimu kutoka katika mwili kuingia katika dunia ya roho, na ninyi ndio watangulizi kwa kutagaa enzi, wanadamu wa ulimwengu wanaovuka miisho ya ulimwengu. Ninyi ni wapendwa Wangu zaidi; ninyi ndio Ninaowapenda.

Jumatano, 10 Julai 2019

Maneno ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 103

Maneno ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 103

Sauti ya mngurumo inatoka, ikiutetemesha ulimwengu mzima, ikiwahanikiza watu, na kuwafanya wachelewe kukwepa, na wengine wanauawa, baadhi wanaangamizwa, na wengine wanahukumiwa. Kweli ni kioja ambacho hakuna yeyote amewahi kukiona awali. Sikiliza kwa makini, milio ya radi inafuatana na sauti za kuomboleza, na sauti hii inatoka kuzimu, sauti hii inatoka jahanamu. Ni sauti yenye uchungu ya wale wana wa uasi ambao wamehukumiwa nami.

Jumamosi, 6 Julai 2019

Maneno ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 104

Maneno ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 104

Watu, matukio na vitu vyote nje Yangu vitakufa na kuwakatika hali ya kutokuwepo, ilhali watu, matukio na vitu vyote vilivyo ndani Yangu vitapata kila kitu kutoka Kwangu na kuingia katika utukufu pamoja na Mimi, kuingia katika Mlima Wangu Sayuni, makazi Yangu, na kuishi pamoja kwa amani nami milele. Niliumba vitu vyote mwanzoni na Nitamaliza kazi Yangu mwishowe, na pia Nitatawala milele kama Mfalme.

Ijumaa, 5 Julai 2019

Maneno ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 105

Maneno ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 105

Kwa sababu ya kanuni za maneno Yangu, kwa sababu ya utaratibu wa kazi Yangu, watu hunikana; hili ndilo kusudi Langu la kuzungumza kwa muda mrefu (imezungumzwa kuhusu wazao wote wa joka kubwa jekundu). Ni njia ya hekima ya kazi Yangu; ni hukumu Yangu ya joka kubwa jekundu; huu ni mkakati Wangu, hakuna mtu hata mmoja anayeweza kuuelewa kikamilifu. Katika kila kipindi muhimu, yaani, katika kila awamu ya mpito ya mpango Wangu wa usimamizi, baadhi ya watu lazima waondolewe; wanaondolewa kulingana na utaratibu wa kazi Yangu.

Alhamisi, 4 Julai 2019

Maneno ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 106

Maneno ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 106

Wale wasioyajua maneno Yangu, wale wasioujua ubinadamu Wangu wa kawaida, na wale wanaokataa uungu Wangu wote wataangamizwa hadi wasikuwepo. Hakuna atakayeachiliwa kutokana na hili, na wote lazima wapitie hili kwa sababu ni amri Yangu ya utawala, na ndicho kifungu kikali zaidi cha amri Yangu. Wale wasioyajua maneno Yangu ni wale ambao wamesikiliza yale ambayo Nimesema wazi, ilhali bado hawayajui, kwa maneno mengine wale ambao hawaelewi masuala ya kiroho (kwa kuwa Sijaumba sehemu hii ya mwili kwa ajili ya wanadamu, Sihitaji mengi kutoka kwao; Nahitaji tu kwamba wasikilize maneno Yangu na kisha wayaweke katika matendo).