Jaweni na Upendo kwa Ajili ya Mungu | Muziki wa Akapela "Yasifu Maisha Mapya"

Haleluya! Twakushukuru na kukusifu Wewe, Mwenyezi Mungu! Kristo wa siku za mwisho ameonekana, akifanya kazi na kuzungumza miongini mwa wanadamu. Neno lake hutuhukumu, kutuadibu na kututakasa, likituongoza kwenye njia sahihi ya maisha ya binadamu.

Ukaribisheni Urejeaji wa Bwana Yesu | Sifa na Ibada “Mungu Ameleta Utukufu Wake Mashariki”

Mungu aliipa Israeli utukufu Wake kisha Akauhamisha mbali na pale, na kuwaleta Waisraeli na kuwaleta watu wote Mashariki. Mungu amewaelekeza wote kwenye mwanga ili waweze kuungana tena na kuwa pamoja na mwanga, wasilazimike kuutafuta tena, kuutafuta mwanga.

Je, Biblia ndiye Bwana, au ni Mungu? | “Bwana Wangu Ni Nani” ( Filamu za Injili )

Liu Zhizhong ni mzee katika kanisa moja la mtaani la nyumba nchini China. Amekuwa muumini kwa zaidi ya miaka 30, na amesisitiza bila kukoma kwamba “Biblia ni ufunuo wa Mungu,” “Biblia inamwakilisha Mungu, kuamini katika Mungu ni kuamini katika Biblia, kuamini katika Biblia ni kuamini katika Mungu.”

Karibu Kurudi kwa Bwana Yesu | Drama ya Muziki “ Kwaya ya Injili ya Kichina Onyesho la 19” | Haleluya

Mungu ametutunza daima–Yeye amesikiliza maombi yetu! Anajua tumekuwa tukitamani kurejea Kwake! Sasa kwa hakika Amerejea! Tunasubiri nini bado? Tafadhali endelea kutazama drama yenye muziki ya Kanisa la Mwenyezi Mungu—Kila Taifa Humwabudu Mungu wa Vitendo!

NYENDO ZA MATESO YA KIDINI NCHINI CHINA (Christian Videos) swahili

Wakristo wanaoteswa katika filamu hii ni watu kutoka kwa vikundi vya kidini na madhehebu tofauti ambao walitafuta ukweli, na ambao waliisikia sauti ya Mungu na hivyo wakarudi kwa Mwenyezi Mungu.

Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Injili. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Injili. Onyesha machapisho yote

Jumamosi, 15 Juni 2019

Kuzaliwa Upya Kupitia Neno la Mungu

Ushuhuda wa Maisha, Wakristo, Kanisa la Mwenyezi Mungu

Wang Gang Mkoa wa Shandong
Mimi ni mkulima na kwa sababu familia yangu ni maskini, daima ilinibidi nisafiri kwenda kote kutafuta kazi za muda ili kupata pesa; nilidhani kuwa ningeweza kujipatia maisha mazuri kupitia kazi yangu ya kimwili. Hata hivyo, kwa uhalisi, niliona kuwa hapakuwa na hakikisho la haki za kisheria za wafanyakazi wahamiaji kama mimi; mshahara wangu mara nyingi ulizuiliwa bila sababu yoyote. Mara kwa mara nilidanganywa na kutumiwa na wengine kwa faida yao. Baada ya kazi ngumu ya mwaka mmoja, sikupokea kile nilichopaswa kupokea. Nilihisi kwamba ulimwengu huu kwa kweli ulikuwa wa giza! Watu hutendeana kama wanyama ambapo wenye nguvu huwawinda walio dhaifu; wao hushindana wenyewe kwa wenyewe, kupigana kwa kukaribiana sana, na sikuwa na mahali pa usalama kwendelea kuishi jinsi hii. Katika maumivu mno na mfadhaiko wa roho yangu, na wakati nilipokuwa nimepoteza imani katika maisha, rafiki yangu alishirikiana wokovu wa Mwenyezi Mungu nami. Tangu wakati huo, nilikutana mara kwa mara, kusali na kuimba pamoja na ndugu wa kiume na wa kike; tuliwasiliana ukweli, na tulitumia uwezo wetu ili kufidia udhaifu wa mwingine. Nilijihisi mwenye furaha sana na aliyekombolewa. Katika Kanisa la Mwenyezi Mungu, niliona kwamba ndugu wa kiume na wa kike hawakujaribu kushindana kwa akili au kufanya utofautishaji wa kijamii; wote walikuwa wazi kabisa na walipatana wenyewe kwa wenyewe. Kila mtu alikuwa hapo kutafuta ukweli kwa bidii ili kuziacha tabia zao potovu, na kuishi kama wanadamu na kupata wokovu. Hili liliniwezesha kupitia furaha katika maisha na kuelewa umuhimu na thamani ya maisha. Kwa hiyo, niliamua kuwa ni lazima nieneze injili na kuwaruhusu watu zaidi wanaoishi gizani kuja kwa Mungu ili kupokea wokovu Wake na kuona mwanga tena. Kwa hiyo, nilijiunga na wale wa kutangaza injili na kumshuhudia Mungu. Lakini bila kutarajia, nilikamatwa na serikali ya CCP kwa kuhubiri injili na kupitia unyama mno wa mateso, utendewaji wa kikatili na kifungo cha jela.
Ilikuwa wakati wa alasiri katika majira ya baridi ya mwaka wa 2008, wakati dada wawili na mimi tulipokuwa tukiishuhudia kazi ya Mungu katika siku za mwisho kwa mlengwa wa injili, tuliripotiwa na watu waovu. Maafisa sita wa polisi walitumia udhuru wa haja ya kuangalia vibali vya makazi yetu ili kuingia kwa nguvu katika nyumba ya mlengwa wa injili. Walipokuwa wakiingia mlangoni, walisema kwa sauti kubwa: “Msisonge!” Wawili wa wale polisi waovu walionekana kuwa wazimu kabisa waliponirukia; mmoja wao alikamata kwa nguvu nguo juu ya kifua changu na mwingine akamata mikono yangu kwa nguvu na kutumia nguvu zake zote ili kuikaza nyuma yangu, kisha akaniuliza kwa ukali: “Unafanya nini? Unatoka wapi? Jina lako ni nani?” Nikauliza kwa kujibu: “Unafanya nini? Unanikamatia nini?” Waliposikia nikisema hivi, walikasirika kweli na wakasema kwa ukali: “Haijalishi sababu ni nini, wewe ndiwe tunayetafuta na unakuja nasi!” Baadaye, wale polisi waovu wakanichukua pamoja na wale dada wawili, wakatusukuma ndani ya gari la polisi na kutupeleka kwa kituo cha polisi cha mahali pale pale.
Baada ya kufika kwa kituo cha polisi, wale polisi waovu walinichukua na kunifungia ndani ya chumba kidogo; waliniamuru nichutame sakafuni na kunipangia watu wanne wanichunge. Kwa sababu nilikuwa nimechuchumaa kwa muda mrefu, nikawa nimechoka sana kiasi kwamba sikuweza kustahimili. Papo hapo nilijaribu kusimama, wale polisi waovu walinijia mbio mbio na kugandamiza kichwa changu chini ili kunizuia kusimama. Ilikuwa tu hadi wakati wa usiku walipokuja kunipekua na kuniruhusu kusimama; walipokosa kupata chochote katika utafutaji wao, wote waliondoka. Muda mfupi baadaye, nikasikia mayowe yenye kutia hofu ya mtu aliyekuwa akiteswa katika chumba cha pili, na wakati huo, niliogopa sana: Sijui ni mateso gani na matendo katili watakayotumia kwangu baadaye! Nilianza kumwomba Mungu kwa moyo wangu kwa dharura: “Ee Mwenyezi Mungu, ninaogopa sana hivi sasa, naomba Unipe imani na nguvu, nifanye imara na jasiri ili niweze kuwa shahidi Kwako. Kama siwezi kuvumilia mateso yao na matendo ya ukatili, kama itanilazimu kujiua kwa kuuma ulimi wangu, sitawahi kukusaliti Wewe kama Yuda!” Baada ya kuomba, niliyafikiria maneno ya Mungu, “Msiogope, Mwenyezi Mungu wa majeshi hakika atakuwa pamoja nawe; Yeye anawasaidia na Yeye ni ngao yenu” (“Sura ya 26” ya Matamko ya Kristo Mwanzoni katika Neno Laonekana katika Mwili). Naam, Mwenyezi Mungu ndiye tegemeo langu na Yeye yu pamoja nami; ni nini kingine cha kuogopwa? Ninahitaji kumtegemea Mungu ili kupigana na Shetani. Maneno ya Mungu yaliondoa woga kutoka moyoni mwangu, na moyo wangu uliwekwa huru.
Usiku huo, polisi wanne wa kishetani walinijia na mmoja wao akanielekeza na kuguta: “Bila shaka tulishika samaki mkubwa! Ninyi waumini wa Mwenyezi Mungu mnavuruga utaratibu wa jamii, na mnavunja sheria za kitaifa….” Aliguta alipokuwa akinisukuma ndani ya chumba cha mateso kwa ghorofa ya pili, akiniamuru nichuchumae. Chumba cha mateso kiliandaliwa na aina zote za vyombo vya mateso kama vile kamba, vijiti vya mbao, virungu, mijeledi, bunduki, nk. Vilikuwa vimepangwa kwa machafuko. Akiwa na uso uliojikunja na macho yaliyowaka kwa hasira, polisi mmoja mwovu alizishika nywele zangu kwa mkono mmoja, na kirungu cha umeme, ambacho kilitoa sauti za dhoruba za “kushambulia na kuzibua” kwa ule mkono mwingine, na akafanya madai ya kuitishia habari: “Ni watu wangapi walio katika kanisa lenu? Eneo la mkutano wenu liko wapi? Ni nani anayesimamia? Ni watu wangapi walio katika sehemu hiyo wakihubiri Injili? Ongea! Vinginevyo, utapata kinachokuja!” Nikaangalia hatari iliyotisha ya kirungu cha umeme na nikaangalia tena kwa chumba kilichojaa vyombo vya mateso; sikuweza kujizuia kuhisi fadhaa na kuogopa. Sikujua kama ningeweza kuyashinda mateso haya. Katika tu wakati huu muhimu, nilifikiria maneno ya Mwenyezi Mungu yakisema: “Lazima pia unywe kutoka kwenye kikombe kikali nilichonywea Mimi (hili ndilo alilomwambia baada ya kufufuka), lazima wewe pia utembee njia niliyotembea Mimi …” (“Namna Petro Alivyopata Kumjua Yesu” katika Neno Laonekana katika Mwili). Nilitambua kwamba hiki kilikuwa kitu ambacho Mungu alituaminia na ilikuwa ni njia ya maisha ambayo Mungu binafsi alituanzishia. Katika kuitembea njia ya kumwamini Mungu na kutafuta ukweli, bila shaka ni lazima mtu apitie mateso na kuvunjika moyo. Hili ni jambo lisiloepukika, na mwishowe, shida hizi huleta baraka kutoka kwa Mungu. Ni kwa njia ya mateso tu watu wanapoweza kupokea njia ya ukweli iliyotolewa na Mungu, na ukweli huu ni uzima wa milele, ambao hutolewa na Mungu. Napaswa kutembea katika nyayo za Mungu na kukabiliana na jambo hili kwa ujasiri; sipaswi kuwa na woga au hofu. Katika kufikiria jambo hili, moyo wangu mara moja ulizalisha aina fulani ya nguvu na nikasema kwa sauti kubwa: “Ninaamini tu katika Mwenyezi Mungu, sijui chochote kingine!” Wakati polisi muovu aliposikia jambo hili, alivurugika na kunidukua kwa nguvu kwa upande wa kushoto wa kifua changu na kirungu hicho cha umeme. Alinishtua kwa karibu dakika moja. Mara moja nilisikia kama damu katika mwili wangu ilikuwa imechemshwa; nilikuwa na maumivu yasiyovumilika kutoka kwa kichwa hadi kwa mguu na nikabiringika nikipiga mayowe sakafuni. Bado hakutaka kuniacha na ghafla akaanza kunivuta na akatumia kirungu kuniinua kwa kidevu changu, akiguta: “Sema! Hutakiri chochote?” Aliguta na kunidukua upande wa kulia wa kifua changu na kirungu cha umeme, nilichomwa na umeme vibaya sana kiasi kwamba nilikuwa nikitetemeka kutoka kichwa hadi mguu. Baadaye mwili uliuma vibaya sana kiasi kwamba nilizirai kama nimelala sakafuni bila kujongea. Sikujua ni muda gani uliokuwa umepita, lakini niliamka yule polisi muovu akisema: “Je! Unajifanya kuwa mfu? Unajifanya! Endelea kujifanya!” Walinidukua tena na kirungu kwa uso na kunipiga teke kwa paja. Baadaye, waliniburuta na kuniuliza kwa ukali: “Je, utaniambia!?” Bado sikujibu. Kisha hao polisi waovu walinipiga kikatili kwa uso wangu kwa ngumi zao na jino langu moja liling’olewa, jino jingine liligongwa hadi likalegea. Mara moja mdomo wangu ulianza kuvuja damu. Katika kukabiliwa na mateso ya kichaa ya pepo hawa, niliogopa tu kwamba ningemsaliti Mungu kwa sababu ya kutoweza kuyahimili mateso yao. Wakati huu, nilifikiri tena juu ya maneno ya Mungu, “Kutoka kwa nje, wale walio na mamlaka wanaweza kuonekana kuwa waovu, lakini msiogope, kwa kuwa hii ni kwa sababu mna imani kidogo. Almuradi imani yenu ikue, hakuna kitu kitakachokuwa kigumu mno” (“Sura ya 75” ya Matamko ya Kristo Mwanzoni katika Neno Laonekana katika Mwili). Maneno ya Mungu yalinipa imani na nguvu tena, na niligundua kuwa ingawa hawa polisi waovu mbele yangu walikuwa na kichaa na bila nidhamu, walipangwa na mkono wa Mungu. Wakati huo, Mungu alikuwa akiwatumia kupima imani yangu. Alimradi niliegemea imani na kumtegemea Mungu na sikukubali kushindwa nao, bila kuzuilika wangeshindwa kwa aibu. Katika kufikiri juu ya hili, nilikusanya nguvu zangu zote za mwili wangu na nikajibu kwa sauti kuu: “Kwa nini mmenileta hapa? Kwa nini mnanishtua kwa umeme kwa kirungu cha umeme? Ni kosa gani nimelifanya?” Yule polisi muovu kwa ghafla akawa mtu aliyeshtuka kiasi cha kutowaza na kukandamizwa sana na dhamiri ya hatia. Alianza kugugumiza: “Mimi … mimi … Sikupaswa kukuletea hapa?” Kisha akaondoka kwa aibu. Katika kuona hali ya aibu ya mtanziko wa Shetani, niliguswa hadi nikalia. Katika mashaka haya, kwa kweli nilipitia nguvu na mamlaka ya maneno ya Mwenyezi Mungu. Alimradi neno la Mungu linawekwa katika vitendo na kufuatwa, basi Mungu atakutunza na kukukinga na nguvu za Mungu zitaandamana nawe. Wakati huo huo, nilijihisi ninawiwa na Mungu kwa sababu ya jinsi nilivyokuwa na imani kidogo. Baadaye, afisa mmoja mrefu wa polisi aliingia na kunijia na akasema: “Unapaswa tu kutuambia ni wapi familia yako huishi na ni watu wangapi walio katika familia yako, na tutakuachilia mara moja.” Alipoona kwamba singesema chochote, alivurugika na kukamata mkono wangu kwa nguvu na kuulazimisha mkono wangu kutia alama kwa ungamo la mdomo walilokuwa wameandika. Niliona kwamba huo ungamo la mdomo halikuwa vile niliyowaambia, lilikuwa ni ushahidi ghushi na wa bandia. Nilijawa na hasira ya haki na kulishika na kulirarua vipande vipande. Yule polisi muovu mara moja aliingiwa na hasira na kunipiga na ngumi yake upande wa kushoto wa uso wangu. Kisha akanipiga makofi mara mbili katika uso kwa nguvu sana kiasi kwamba nilishikwa na kizunguzungu. Baadaye, walinipeleka kwa chumba kidogo nilichokuwemo awali.
Baada ya kurudi kwa kile chumba kidogo, nilichubuliwa na kugongwagongwa sana, maumivu yalikuwa yasiyovumilika. Moyo wangu haukuweza kujizuia kuzalisha hisia ya huzuni na udhaifu: Kwa nini waumini wanapaswa kuteseka jinsi hii? Nilihubiri Injili na nia njema za kuwaruhusu watu kuutafuta ukweli na kuokolewa, na bila kutarajia nimepitia mateso haya. Katika kufikiri juu ya hili, nilihisi zaidi kuwa nilikuwa nimekosewa. Katika maumivu yangu, nilifikiria maneno ya Mungu: “Kama binadamu, unapaswa kutumia rasilmali kwa ajili ya Mungu na kuvumilia kila mateso. Unapaswa kukubali kwa furaha na kwa hakika mateso kidogo unayopitia leo na kuishi maisha yenye maana, kama Ayubu, kama Petro. … Ninyi ni watu mnaofuatilia njia sahihi, wale wanaotafuta maendeleo. Ninyi ni watu ambao huinuka katika nchi ya joka kuu jekundu, wale ambao Mungu huwaita wenye haki. Je, hayo si maisha yenye maana zaidi?” (“Utendaji (2)” katika Neno Laonekana katika Mwili). Maneno ya Mwenyezi Mungu yalivutia hisia kubwa kutoka kwa wangu. Ndio, Mungu alininyunyizia na kunipa maneno Yake makarimu ya uzima, Ameniruhusu kufurahia neema Yake nyingi bure na kuniruhusu kujua siri za ukweli ambazo hakuna mtu yeyote tangu vizazi vya zamani amezielewa. Hii ni baraka maalum ambayo Mungu amenipa. Napaswa kushuhudia kwa Mungu na kuvumilia maumivu yote kwa ajili ya Mungu. Kiasi chochote cha maumivu ni cha kufaa, kwa sababu ni jambo la thamani na la maana sana! Leo, ninateswa kwa kuhubiri injili na siko tayari kupitia maumivu yoyote ya kimwili kwa ajili ya injili; ninahisi kukosewa na kutokuwa tayari. Si nimemhuzunisha Mungu kwa kufanya hivi? Si nimekosa dhamiri? Ningewezaje kustahili baraka za huruma za Mungu na utolewaji wa maisha? Vizazi vya watakatifu wamebeba ushuhuda wa nguvu na mkubwa kwa Mungu kwa sababu walifuata njia ya Mungu; waliishi maisha yenye maana. Leo nina maneno haya yote kutoka kwa Mungu, kwa hiyo mimi si ni lazima hata zaidi nitoe ushuhuda mzuri kwa ajili ya Mungu? Kwa kutafakari jambo hili, mwili wangu haukujihisi kama mchungu, nilijua sana kuwa ni neno la Mwenyezi Mungu ambalo lilinipa uwezo wa uzima, likiniruhusu kuushinda udhaifu wa mwili.
Siku iliyofuata, hao polisi waovu hawakuwa na mkakati mwingine ulioachwa kujaribu. Walinitishia wakisema: “Hutasema chochote? Basi tutakufunga gerezani!” Baadaye, walinipeleka kwa kituo cha kizuizi. Katika kituo cha kizuizi, hao polisi waovu waliendelea kutumia njia zote za mateso kwangu na mara nyingi waliwahimiza wafungwa kunipiga. Katika baridi kali ya majira ya baridi, waliwaagiza wafungwa kunimwagilia ndoo za maji baridi na kunilazimisha kuoga na maji baridi. Nilikuwa nikitetemeka kwa baridi kutoka utosini hadi kidoleni. Hapa, wafungwa walikuwa mashine ya kutengeneza pesa kwa serikali na hawakuwa na haki yoyote ya kisheria. Hawakuwa na chaguo jingine ila kuvumilia kuminywa na kutumiwa na wengine kwa faida yao kama watumwa. Gereza lilinilazimisha kuchapisha pesa za karatasi zilizotumika kama sadaka za kuteketezwa kwa wafu mchana kutwa na kunilazimisha nifanye kazi ya ziada usiku. Kama ningesimama ili kupumzika, basi mtu fulani angekuja na kunipiga sana. Mara ya kwanza, waliweka sheria kwamba nilipaswa kuchapisha vipande 2,000 vya karatasi kwa siku, kisha wakaongeza viwe vipande 2,800 kwa siku, na hatimaye hadi vipande 3,000. Kiasi hiki kilikuwa hakiwezekani kwa mtu mwenye ujuzi kukamilisha sembuse mtu asiye na ujuzi kama mimi kukamilisha. Kwa kweli, walipanga hivyo kwa makusudi ili nisiweze kukamilisha yote ili waweze kuwa na udhuru wa kunitesa na kunidhuru. Alimradi sikuweza kufikia kiasi hicho, hao polisi waovu wangeniwekea pingu za miguu kwa miguu yangu ambazo zilikuwa na uzito wa zaidi ya kilo 5, na kuifunga mikono na miguu pamoja kwa pingu. Yote niliyoweza kufanya ni kuketi pale, kuinamisha kichwa changu na kugeuza kiuno changu, vinginevyo sikuweza kusonga. Aidha, hawa polisi wakatili na wasio na hisia hawakuuliza au kujali kuhusu mahitaji yangu ya msingi. Ingawa choo kilikuwa ndani ya seli ya gereza, sikuweza kabisa kutembea na kukitumia; niliweza tu kuwaomba wenzangu katika seli kuniinua na kuniwekelea kwa choo. Kama walikuwa wafungwa bora zaidi kidogo, basi wangeweza kuniinua; kama hakuna mtu aliyenisaidia, basi singekuwa na chaguo jingine ila kujinyia katika suruali yangu. Wakati wa maumivu mno ulikuwa wakati wa chakula, kwa sababu mikono na miguu yangu ilikuwa imefungwa pamoja. Niliweza tu kuteremsha kichwa changu kwa nguvu zangu zote na kuinua mikono na miguu yangu. Ni kwa njia hii tu nilivyoweza kuiweka skonsi kinywani mwangu. Nilitumia nguvu nyingi sana kwa kila umo. Pingu zilisugua mikono na miguu yangu na zikisababisha maumivu makubwa. Baada ya muda mrefu, vifundo vya mikono yangu na vya miguu vilikuwa vimekuza sagamba nyeusi na ngumu zilizong’aa. Mara nyingi sikuweza kula wakati nilipokuwa nimefungiwa, na mara chache, wafungwa wangenipa skonsi mbili ndogo. Mara nyingi wangekula sehemu yangu na yote niliyopata ilikuwa tumbo tupu. Nilipokea hata kinywaji kidogo zaidi; awali, kila mmoja alipewa tu bakuli mbili za maji kwa siku, lakini nilikuwa nimefungiwa na sikuweza kusogea, hivyo ni kwa nadra sana niliweza kunywa maji yoyote. Mateso hayo ya kinyama yalikuwa yasiyosemeka. Kwa ujumla, niliteseka hivi mara nne na kila mara nilikuwa nimefungiwa kwa siku zisizopungua tatu na zisizozidi nane. Kila wakati ambapo njaa haikuvumilika, ningefikiria maneno ambayo Mungu aliyasema zamani: “Mwanadamu hatadumu kwa mkate pekee, lakini kwa kila neno linalotoka kinywani mwa Mungu” (Mathayo 4:4). Hatua kwa hatua nilianza kutambua kwamba Mungu anataka kutimiliza ukweli kwamba “Neno Lake lakuwa uhai wa mwanadamu” kwangu kupitia mateso ya Shetani. Katika kuelewa mapenzi ya Mungu, moyo wangu uliokolewa na nikamwomba Mungu kwa amani na kujaribu kuyaelewa maneno ya Mungu. Pasipo kujua, sikuhisi uchungu sana tena au njaa. Hili kwa hakika lilinifanya nisihisi kuwa neno la Mungu ni ukweli, njia, na uzima na bila shaka ni msingi ambao napaswa kutegemea ili kuishi. Kwa hiyo, imani yangu kwa Mungu iliongezeka bila kujua. Nakumbuka wakati mmoja polisi wa gerezani kwa makusudi walinitesa na kunifunga pingu. Kwa siku tatu mchana na usiku sikunywa hata tone la maji. Mfungwa aliyekuwa amefungwa pingu karibu na mimi akasema: “Kulikuwa na mtu fulani wa umri mdogo kabla ambaye alifungwa pingu na kunyimwa chakula jinsi hii hadi kufa. Naona kuwa hujala chochote kwa siku kadhaa na bado una uchangamfu.” Katika kusikia maneno yake, nilifikiri kwamba ingawa sikuwa nimekula au kunywa chochote kwa siku tatu mchana na usiku, sikuhisi kero ya njaa. Nilihisi sana kwamba hii ilikuwa ni nguvu ya uzima katika maneno ya Mungu ikinisaidia na kunisababisha kwa hakika kuona Mungu akionekana kwangu katika maneno Yake. Moyo wangu ulikuwa na msisimko daima; katika mazingira haya ya mateso niliweza kwa kweli kupitia uhalisi wa ukweli kwamba “Mwanadamu hataishi kwa mkate pekee, lakini kwa kila neno linalotoka kinywani mwa Mungu.” Huu kwa kweli ni utajiri wa thamani zaidi wa maisha ambao Mungu ameniridhia, na pia ni zawadi yangu ya pekee. Aidha, singeweza kamwe kuupata katika mazingira ambayo sikuhitaji kuwa na wasiwasi juu ya chakula au nguo. Sasa, mateso yangu yalikuwa na maana nyingi sana na thamani! Wakati huu, sikuweza kujizuia kufikiria maneno ya Mungu: “Kile ambacho umerithi wakati huu, kimepiku walichorithi mitume na manabii na ni kikuu zaidi kuliko alichopokea Musa na Petro. Baraka haziwezi zikapokewa kwa siku moja au mbili; sharti zipatikane kwa kujitolea kwingi. Yaani, lazima uwe na upendo uliosafishwa, imani kuu, na ukweli mwingi ambao Mungu Anakuagiza uufikie; zaidi ya hayo, sharti uelekeze uso wako kwa haki wala usikubali kushindwa, na lazima uwe na upendo usiofikia kikomo kwa ajili ya Mungu. Azimio linahitajika kutoka kwako, na vilevile mabadiliko katika tabia ya maisha yako. Upotovu wako lazima utibiwe, na lazima ukubali mipango ya Mungu pasipo kulalamika, na hata uwe mtiifu hadi kifo. Hicho ndicho unachopaswa kutimiza. Hili ndilo lengo la Mungu la mwisho, na matakwa ya Mungu kwa watu wa kundi hili” (“Je, Kazi ya Mungu Ni Rahisi Jinsi Mwanadamu Anavyodhania?” katika Neno Laonekana katika Mwili). Katika kujaribu kuyaelewa maneno ya Mungu, nilitambua kwamba baada ya mateso na majaribu baraka huja kutoka kwa Mungu, na huu ndio ugavi wa mahitaji na umwagiliwaji wa maji kwangu kutoka kwa Mungu. Sasa, ingawa maneno ambayo Mungu amenipa yamepita vizazi vya watakatifu, bado nahitaji kuwa na imani na uvumilivu ili kuwa na uwezo wa kutokukubali kushindwa wakati wa majaribu na mateso yangu, kuitii mipango ya Mungu, na kupokea wokovu wa Mungu. Kisha nitaweza kuuingia uhalisi wa neno la Mungu na kuweza kuona matendo ya ajabu ya Mungu. Kama haingekuwa kwa gharama ya shida hii, singestahili kupokea ahadi na baraka za Mungu. Kupokea nuru ya Mungu kulinielekeza kuwa na udhabiti na nguvu zaidi ndani; niliweka azimio: Shirikiana na Mungu kwa bidii na kuyaridhisha mahitaji ya Mungu katikati ya mazingira haya machungu, kumshuhudia Mungu ili niweze kuwa na mavuno makubwa mno.
Mwezi mmoja baadaye, polisi wa CCP walinishtaki na “kushukiwa kuvuruga utaratibu wa jamii na kuharibu utekelezaji wa sheria”; nilihukumiwa mwaka mmoja wa mageuzi kupitia kazi. Nilipoingia kambi ya kazi, wale polisi waovu walieneza uvumi na upuuzi miongoni mwa wafungwa, wakisema kuwa nilikuwa muumini katika Mwenyezi Mungu, jambo ambalo ni baya kuliko mauaji na wizi, na waliwachochea wafungwa kunitesa. Kwa hiyo mara nyingi nilipigwa na kuwekwa katika hali ngumu na wafungwa bila sababu yoyote. Hili lilinifanya nione kweli kwamba China ni nchi ya mateso na maumivu inayoongozwa kwa uthabiti na Shetani, pepo. Kuna giza kutoka kila pembe, na hakuna mwanga unaoruhusiwa kuwepo; hakuna mahali kabisa pa waumini wa Mwenyezi Mungu kuishi. Wakati wa mchana, hao polisi waovu walinilazimisha kufanya kazi katika karakana. Kama sikufikia kiasi nilichopaswa kufikia, wangewaacha wafungwa wanipige wakati niliporudi kwa seli yangu gerezani na kutangaza “mfanyeni mfano ili kuwaogofya wengine.” Nilipokuwa katika karakana nikihesabu mifuko, ningehesabu mifuko 100 na kisha kuifunga pamoja. Wafungwa wangekuja daima na kutoa mfuko moja au kadhaa kutoka kwa ile niliyokuwa nimehesabu, kisha wangesema kwamba sikuhesabu vizuri na kuchukua hiyo kama fursa ya kunipiga ngumi na mateke. Wakati msimamizi huyo aliponiona nikipigwa, angekuja na kuniuliza kwa unafiki kilichokuwa kikiendelea na wafungwa wangewasilisha ushahidi wa uongo kwamba sikuwa nimehesabu mifuko ya kutosha. Kisha ningelazimika kustahimili mfululizo wa ukosoaji mkali kutoka kwa msimamizi. Aidha, wangeniamuru nikariri “amri za maadili mema” kila asubuhi, na kama sikuzikariri, ningepigwa; pia wangenilazimisha kuimba nyimbo zilizokisifu chama cha Kikomunisti. Kama waliona kwamba sikuwa nikiimba au kwamba midomo yangu haikuwa ikisonga, basi usiku bila shaka ningepigwa. Pia waliniadhibu kwa kunifanya nipanguse sakafu, na kama sikupangusa kwa matarajio yao, basi ningepigwa kwa nguvu nyingi. Wakati mmoja, kwa ghafla wafungwa fulani walianza kunigonga na kunipiga mateke. Baada ya kunipiga, waliniuliza: “Kijana, unajua kwa nini unapigwa? Ni kwa sababu hukusimama na kumsalimu msimamizi wakati alipokuja!” Baada ya kila wakati nilipopigwa, nilikuwa na hasira lakini sikuthubutu kusema chochote; niliweza kulia tu na kumwomba Mungu kimyakimya, nikimwambia Yeye juu ya chuki na malalamiko moyoni mwangu kwa sababu ya mahali hapa palipo na utovu wa sheria, na kukosa mantiki. Hapakuwa na busara hapa, palikuwa na vurugu tu. Kulikuwa hakuna watu hapa, kulikuwa na pepo wenye wazimu na nge tu! Nilihisi maumivu mengi sana na shinikizo nikiishi katika shida hii; sikuwa tayari kukaa hata dakika moja zaidi. Kila wakati nilipotumbukia katika hali ya udhaifu na maumivu, ningefikiri juu ya maneno ya Mwenyezi Mungu: “Mmewahi kuzikubali baraka mlizopewa? Mmewahi kutatufa ahadi mlizopewa? Hakika, chini ya mwongozo wa mwangaza Wangu, mtapenya utawala wa nguvu za giza. Hakika, katikati ya giza, hamtaupoteza mwangaza unaowaongoza, katikati ya giza. Hakika mtakuwa bwana wa viumbe vyote. Hakika mtakuwa washindi mbele ya Shetani. Hakika, wakati wa maangamizi ya ufalme wa joka kubwa jekundu, mtasimama miongoni mwa umati mkubwa kushuhudia ushindi Wangu. Hakika mtakuwa shujaa na imara katika nchi ya Sinimu. Kupitia mateso mnayoyavumilia, mtarithi baraka zinazotoka Kwangu, hakika mtaangaza ndani ya ulimwengu wote kwa utukufu Wangu” (“Sura ya 19” ya Maneno ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima katika Neno Laonekana katika Mwili). Maneno ya Mungu yalinitia moyo. Bila kujali kama kile Mungu alichokuwa akinifanyia kilikuwa neema na baraka au majaribu na usafishwaji, yote ilikuwa ili kunikimu na kuniokoa; ilikuwa ni kuweka ukweli ndani yangu na kufanya ukweli kuwa maisha yangu. Leo, Mungu aliruhusu mateso haya na taabu zinijie. Ingawa jambo hili lilisababishia mateso mengi, liliniruhusu kuweza kwa kweli kuwa na uzoefu kwamba Mungu yu pamoja nami; lilinifanya kwa kweli nifurahie maneno ya Mungu kuwa mkate wa maisha yangu na taa ya miguu yangu na mwanga kwa njia yangu, likiniongoza hatua kwa hatua kupitia mahali hapa padhalimu na pasipovumilika. Huu ndio upendo na ulinzi wa Mungu ambao nilifurahia na kupata wakati wa mchakato wa mateso yangu. Wakati huu, niliweza kuona kwamba nilikuwa kipofu sana na wa ubinafsi na nilikuwa mwenye uroho mno. Katika kumwamini Mungu, nilijua tu jinsi ya kufurahia neema na baraka za Mungu na sikutafuta ukweli na uhai kwa kiwango hata kidogo. Mara mwili wangu uliopitia shida kidogo, ningenung’unika bila kukoma; sikuelewa kabisa mapenzi ya Mungu na sikutafuta kuielewa kazi ya Mungu. Daima ningemfanya Mungu ahisi huzuni na maumivu juu yangu. Kwa kweli nilikuwa bila dhamiri! Kwa majuto na kujilaumu, niliomba kimya kimya kwa Mungu: “Ewe Mwenyezi Mungu, naweza kuona kwamba kila kitu unachokifanya ni kuniokoa na kunipata. Ninachukia tu kwamba mimi ni mkaidi sana, ni kipofu na sina ubinadamu. Daima nimekuelewa visivyo na sijakuwa wa kufikiria mapenzi Yako. Ee Mungu, leo neno Lako limeuamsha moyo wangu wenye ganzi na roho yangu na limenisababisha kuyaelewa mapenzi Yako. Siko tayari tena kuwa na tamaa na mahitaji yangu mwenyewe; nitatii tu mipango Yako. Hata kama ni lazima nipitie matatizo yote, bado nitaendelea kushirikiana na Wewe kwa bidii na nitatoa ushahidi mkubwa sana Kwako muda wote wa mateso ya Shetani. Nitatafuta kujitenga na ushawishi wa Shetani na kuishi kwa kudhihirisha mfano wa mtu halisi ili kukuridhisha.” Baada ya kuomba, nilielewa nia njema za Mungu, na nilijua kwamba kila mazingira ambayo Mungu aliniruhusu kupitia yalikuwa ni upendo na wokovu mkubwa wa Mungu kwangu. Kwa hiyo, singefikiria tena kujikunyata au kumwelewa Mungu visivyo. Ingawa hali ilikuwa bado ni ile ile, moyo wangu kwa kweli ulijaa furaha na ridhaa; nilihisi kuwa ni heshima na fahari kuweza kupitia shida na mateso kwa sababu ya imani yangu kwa Mwenyezi Mungu, na ilikuwa ni zawadi ya pekee kwangu, mtu mpotovu; ilikuwa baraka maalumu na neema za Mungu kwangu.
Baada ya kuwa na uzoefu wa mwaka mmoja wa shida katika jela, naona kwamba mimi ni mdogo sana wa kimo na kwamba nakosa ukweli mwingi sana. Mwenyezi Mungu kwa kweli amefidia upungufu wangu kupitia mazingira haya ya kipekee na ameniruhusu kukua. Katika dhiki yangu, Amenifanya kupata utajiri wa thamani mno katika maisha na kuelewa ukweli mwingi ambao sikuufahamu katika siku za nyuma na kuona kwa dhahiri sura mbaya kwa Shetani, pepo, na kiini cha kupinga maendeleo cha upinzani wake kwa Mungu. Nilitambua uhalifu wake muovu wa kumtesa Mwenyezi Mungu na kuwaua Wakristo. Nilipitia kwa dhati wokovu na huruma kubwa Mwenyezi Mungu aliyokuwa nayo kwangu, mtu mpotovu, na nimehisi kwamba nguvu na maisha katika maneno ya Mwenyezi Mungu yanaweza kunipa mwanga na kuwa maisha yangu na kunielekeza kumshinda Shetani na kwa ushupavu kutoka nje ya bonde la uvuli wa mauti. Vivyo hivyo, pia niligundua kwamba Mwenyezi Mungu ndiye anayeniongoza kwenye njia sahihi ya uzima. Ni njia ng’avu ya kupata ukweli na uzima! Kuanzia sasa na kwendelea, bila kujali ni mateso yapi, dhiki au majaribu hatari yanayonikabili, niko tayari kutafuta ukweli kwa bidii na kupata njia ya uzima wa milele ambayo Mwenyezi Mungu amenipa.
Chanzo: Kanisa la Mwenyezi Mungu | Ushuhuda wa Kuipitia Hukumu ya Kristo

Ijumaa, 24 Mei 2019

Maneno ya Mungu Yaliniongoza Kutoka Katika Matatizo

Maneno ya Mungu Yaliniongoza Kutoka Katika Matatizo

Xiao Rui Mji wa Panzhihua, Mkoa wa Sichuan
Nilipokuwa nikihubiri injili nilikutana na viongozi wa dini ambao walisema uongo ili kupinga na kuvuruga, na kuwaita polisi. Hili lilisababisha wale niliokuwa nikihubiria kutothubutu kuwasiliana nasi, na wale ambao walikuwa tu wameikubali injili kutoweza kuwa na imani katika kazi ya Mungu. Nilipofanya kazi kwa bidii sana lakini matokeo yalikuwa duni, nilifikiri: kazi ya Kiinjili ni ngumu sana kutekeleza. Lingekuwa jambo la kustaajabisha sana kama Mungu angeonyesha miujiza kiasi na kuwaadhibu wale ambao husema uongo pamoja na wale ambao kwa uzito kabisa humpinga Mungu kuwaonyesha wale ambao wamedanganywa. Basi si kazi ya injili ingetekelezwa kwa haraka zaidi? Haingekuwa vigumu sana kwetu kuhubiri injili.... Ndiyo maana tumaini hili lilikuja moyoni mwangu kila wakati nilipokutana na aina hizi za matatizo. Baadaye, nilisoma kitabu cha mifano ya adhabu na wakati wa ushirika nikasikia ushahidi wa baadhi ya ishara na maajabu ya Mungu, na nilifurahi sana moyoni mwangu. Nilitumaini hata zaidi kwamba Mungu angefanya mambo fulani katika maeneo ambayo nilifanyia kazi ili kwamba mashaka ya kazi yetu ya injili yangeweza kutatuliwa kwa haraka zaidi. Lakini bila kujali jinsi nilivyotarajia, bado sikuona Mungu akifanya miujiza yoyote hapa au kuwaadhibu watu waovu. Watu wa dini walikuwa bado wanampinga Mungu kabisa, na matatizo katika kazi ya kiinjili yalikuwa bado ni makubwa. Nikawa hasi juu ya hili: Kwa nini Mungu hafungui njia kwa ajili yetu? Ingewezekana kuwa imani yetu haitoshi?
Baadaye, wakati wa sala zangu nikaona maneno haya ya Mungu: “Sasa, kama Mungu angetekeleza ishara na maajabu ya miujiza, basi, bila kulazimika kuanza kazi yoyote kubwa, Angemlaani tu mtu kufa kwa kinywa Chake Mwenyewe, mtu huyo angekufa papo hapo, na kwa njia hii kila mwanadamu angeridhishwa; lakini hili halingetimiza lengo la Mungu katika kuwa mwili. Kama Mungu angefanya hili kweli, ubinadamu haungeweza kamwe, kwa akili zao za kufahamu, kuamini kuweko Kwake, haungeweza kamwe kuamini kweli, na zaidi ya hayo ungedhania kwamba shetani ni Mungu. Hata la muhimu zaidi, ubinadamu haungejua tabia ya Mungu kamwe: Je, hiki si kipengele kimoja cha maana ya Mungu kuwa ndani ya mwili? Kama ubinadamu hauwezi kumjua Mungu, basi daima itakuwa Mungu asiye dhahiri, Mungu wa miujiza, ambaye Ana utawala mkubwa katika ufalme wa binadamu: Hili halingekuwa suala la fikira za mwanadamu kummiliki mwanadamu? Au, kulitamka hili tena kwa dhahiri zaidi, Shetani, ibilisi, hangekuwa ana utawala mkubwa? "Kwa nini Nasema Narejesha mamlaka Yangu? Kwa nini Nasema kwamba kupata mwili kuna maana nyingi sana?" Wakati ambapo Mungu hupata mwili, huo ndio wakati ambapo Hurejesha mamlaka Yake; pia ni wakati ambapo uungu Wake hujitokeza moja kwa moja kufanya kazi Yake. Hatua kwa hatua, kila mwanadamu huja kumjua Mungu wa vitendo, na kwa ajili ya hili nafasi inayoshikiliwa na Shetani ndani ya moyo wa mwanadamu hukandamizwa kabisa huku nafasi ya Mungu ikikuzwa” (“Ufafanuzi wa Tamko la Sita” katika Neno Laonekana katika Mwili). Wakati nikijaribu kuyaelewa maneno ya Mungu, moyo wangu ghafla ukachangamka: Inaonekana kwamba madhumuni ya kazi ya Mungu katika mwili sio kutumia mamlaka Yake kuwaogopesha watu ili kiutii, lakini ni kuifungua kabisa tabia Yake kwa wanadamu kupitia kazi halisi na maneno, na kwa njia hii kufukuza picha iliyo katika mioyo ya wanadamu ya Mungu asiye yakini. Ni kuwaruhusu watu kulegeza vikwazo vya mawazo yao, kutambua kwa kweli tabia na kazi ya Mungu, kuwaruhusu watu kuwa na ukweli na ufahamu, na hivyo kuwashinda na kuwachuma. Kazi ya Mungu kwa kweli ni ya vitendo mno, na hekima Yake ni isiyoeleweka kwa wanadamu! Hebu ifikirie kwa manini—kazi hii ambayo Mungu anafanya haingezaa matunda kama ingefanywa kupitia ishara na maajabu. Kama tu vile katika Enzi ya Sheria, Mungu aliwaonyesha Waisraeli miujiza mingi sana na kuwaadhibu wengi sana wa wale waliomkataa Yeye, lakini Waisraeli bado hawakumtambua Mungu na hatimaye walienda kufa jangwani. Katika Enzi ya Neema, Mungu pia alionyesha ishara nyingi mno na maajabu kati ya Wayahudi, lakini bado walimsulubisha akiwa hai kwa sababu hawakumtambua Yeye. Hili lote lasema kwamba ishara za Mungu na maajabu vyaweza tu kuwaogofya watu kwa muda mfupi, lakini sio msingi wa imani yao kwa Mungu. Hata hivyo, ingawa nimemfuata Mungu hadi sasa, sijawa na ufahamu hata chembe wa asili ya Mungu, na nimeelewa hata machache ya malengo na umuhimu wa kazi ya Mungu katika mwili. Mimi bado nimeamini katika mamlaka Yake na kwamba yeyote ambaye humpinga Mungu ataadhibiwa, hivyo nimefuatilia kikamilifu kuona ishara za Mungu na maajabu. Si aina hii ya imani hasa kama Mafarisayo, wakiishi katikati ya hali ya mashaka, wakiamini katika Mungu wa miujiza wakati ule ule wakimpinga Mungu wa vitendo? Kama ukimbizaji wangu wa Mungu ungeendelea kwa njia hii, ningewezaje kulingana na Mungu wa kweli? Kwa kweli ilikuwa ni hatari sana! Baada ya hapo, Niliona zaidi ya maneno ya Mungu: “Ni vigumu kabisa kwa Mungu kutekeleza kazi yake katika nchi yenye joka kuu jekundu, lakini ni kupitia ugumu huu ndipo Mungu Hupiga hatua katika kazi Yake ili kudhihirisha hekima Yake na matendo Yake ya ajabu. Mungu Huchukua fursa hii kuwakamilisha watu hawa wa kikundi hiki. Kwa ajili ya mateso ya watu, tabia yao na hulka ya kishetani ya watu katika nchi hii najisi, Mungu Anafanya kazi Yake ya kutakasa na ushindi, ili, kutokana na hili, apokee utukufu na kuwapata wale wote wanaoshuhudia matendo Yake. Huu ndio umuhimu wa kujitoa kwa Mungu kwa ajili ya kikundi hiki cha watu. Ina maana kuwa Mungu hufanya kazi ya ushindi kupitia wale wanaompinga. Kwa hiyo, kufanya vile kunadhihirisha nguvu za Mungu. Kwa maneno mengine, ni wale tu walio katika nchi najisi ndiyo wanaostahili kuurithi utukufu wa Mungu na ni hili tu ambalo litafanya nguvu kuu za Mungu kuwa maarufu. Ndiyo maana Nasema kuwa utukufu wa Mungu unapatikana katika nchi najisi na kwa wale wanaoishi humo. Haya ndiyo mapenzi ya Mungu. Hii ni kama tu ilivyokuwa katika kazi ya Yesu; Angetukuzwa tu kati ya Wafarisayo waliomdhihaki. Isingelikuwa mateso na usaliti wa Yuda, Yesu asingelidhihakiwa na kudharauliwa, na hata zaidi kusulubiwa, na hivyo asingelipokea utukufu” (“Je, Kazi ya Mungu ni Rahisi Jinsi Mwanadamu Anavyodhania?” katika Neno Laonekana katika Mwili). Kwa wakati huu, kutoka kwa maneno ya Mungu nilikuwa na ufahamu zaidi kwamba bila kujali ni kazi gani Mungu hufanya, yote ina maana. Akikamilisha kazi ya kufichua miujiza kiasi au kugawa adhabu kiasi, ina maana, ina kanuni. Asipokamilisha kazi ya kufichua miujiza au kugawa adhabu, basi ina hata zaidi ya hekima ya Mungu. Sasa, Mungu hayatumii mamlaka Yake kuwaondoa wale wanaosema uongo au kumpinga Yeye kwa uzito; kuna zaidi ya ukarimu wa Mungu. Mungu hutumia matatizo haya kutuwezesha kuonja shida za kazi Yake mwenyewe, hivyo kutambua wema na uzuri wa Mungu. Mungu pia hutumia matatizo haya kukamata ushahidi wa watu wakifanya mema au maovu, na hatimaye kuwapa hatima inayofaa ili tuwe na uhakika kabisa, ili tuweze kuona haki na utakatifu wa Mungu. Zaidi ya hayo, Mungu hutumia matatizo haya kufichua kwamba nimepungukiwa na ukweli wa maono, kwamba asili yangu ni vivu sana, oga, jinga, na ya kipumbavu, na kwamba kwa njia ya mateso yangu, jitihada, na ushirikiano na Mungu, Atatutolea ufahamu , imani, upendo, hekima, na ujasiri, na hata zaidi Atatupa ukweli wa kazi ya Mungu, na hivyo kutukamilisha, kutupata. Kazi ya Mungu kwa kweli ni yenye busara, ya ajabu sana! Lakini mimi ni kipofu sana—sina ufahamu wa umuhimu wa kazi ya Mungu na nia Zake nzuri. Yote ninayoogopa ni mateso ya kimwili na sitaki kushirikiana na Mungu. Mimi kwa kweli ni muumini ambaye hatekelezi kazi ya kufaa na ambaye husherehekea katika faraja!
Shukrani iwe kwa kunurishwa kwa maneno ya Mungu ambayo yalinipa utambuzi kiasi wa madhumuni na hekima katika kazi ya Mungu katika mwili na pia yakaniruhusu kuona kwamba imani yangu katika Mungu ilikuwa ikiishi katika hali ya mashaka, kwamba kutomtambua Mungu ni hatari sana! Kuanzia siku hii kwendelea, ninahiari kujiandaa na ukweli wa maono, kufuatilia kuwa mtu anayeitambua kazi ya Mungu na tabia, kwa kweli kumiliki hiari ya kuteseka, kutekeleza wajibu wangu kwa lile linalowezekana ili kuufariji moyo wa Mungu.
Chanzo: Chanzo: Kanisa la Mwenyezi Mungu | Ushuhuda wa Kuipitia Hukumu ya Kristo

Jumamosi, 5 Januari 2019

Mmempa Mungu Nini Kama Malipo?

I
Mungu amekuwa kati yenu
kwa majira kadhaa ya kupuputika na ya kuchipua.
Ameishi nanyi kwa muda mrefu.
Mbele Yake ni matendo yenu mangapi maovu yamenyiririka?
Maneno ya dhati mnayoyasema, yanarudisha mwangwi katika masikio ya Mungu.

Jumamosi, 29 Desemba 2018

29. Mungu Ameonekana Mashariki mwa Dunia na Utukufu

I
Mungu anafanya kazi ulimwenguni kote.
Kelele za radi ya Mashariki hazipungui,
Zikitikisa madhehebu na makundi yote.
Ni sauti ya Mungu iliyoleta vyote wakati wa sasa.
Ni sauti Yake ndiyo itashinda kila kitu.
Wanaanguka katika mtiririko huu, na kumtii Yeye.

Jumamosi, 22 Desemba 2018

"Nimewahi Treni ya Mwisho" (4) : Hukumu Mbele ya Kiti Kikuu Cheupe cha Mungu Imeanza

"Nimewahi Treni ya Mwisho" (4) : Hukumu Mbele ya Kiti Kikuu Cheupe cha Mungu Imeanza

Unajua jinsi hukumu ya kiti cha enzi kikuu cheupe iliyotabiriwa katika Ufunuo inatimizwa? Je, hukumu ya kiti cha enzi kuu cheupe iko mbinguni, au duniani? Je, inafanywa na Mungu aliyepata mwili, au kwa Roho?

Jumatano, 12 Desemba 2018

Best Swahili Full Christian Movie | "Wimbo wa Ushindi" | Preaching the Gospel of the Last Days

Best Swahili Full Christian Movie | "Wimbo wa Ushindi" | Preaching the Gospel of the Last Days

Kazi ya hukumu ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho imevuma katika kila farakano na kikundi. Kufuatia kuenea kwa injili ya ufalme, maneno ya Mwenyezi Mungu yanakubaliwa na kuenezwa na watu zaidi na zaidi, waumini wa kweli katika Mungu ambao wana kiu ya Yeye kuonekana wamekuwa wakirudi mmoja kwa mmoja mbele ya kiti cha enzi cha Mungu. Kwa sasa, serikali ya China na wachungaji na wazee wa kanisa wa kidini wamelizuia na kulitesa Kanisa la Mwenyezi Mungu bila kukoma tangu mwanzo hadi mwisho.

Jumanne, 11 Desemba 2018

Sauti na maneno ya Roho Mtakatifu | "Unapaswa Kushughulikiaje Wito Wako wa Mustakabali?"

Sauti na maneno ya Roho Mtakatifu | "Unapaswa Kushughulikiaje Wito Wako wa Mustakabali?"

Mwenyezi Mungu anasema, "Hata ingawa wamenusurika mpaka siku hii, ni nani angefikiri kuwa wamepewa sumu na yule mwovu kwa muda mrefu? Je, umesahau kuwa wewe ni mmoja wa waathiriwa? Kwa ajili ya upendo wako kwa Mungu, una nia ya kufanya kila uwezalo kuwaokoa walionusurika?

Ijumaa, 7 Desemba 2018

Maneno ya Roho Mtakatifu kwa makanisa | "Enzi ya Ufalme Ndiyo Enzi ya Neno" (Official Video)

Maneno ya Roho Mtakatifu kwa makanisa | "Enzi ya Ufalme Ndiyo Enzi ya Neno" (Official Video)

Mwenyezi Mungu anasema, "Katika Enzi ya Ufalme, Mungu anatumia neno ili kukaribisha enzi mpya, ili kubadilisha mbinu za kazi Yake, na kuweza kufanya kazi katika enzi nzima. Hii ndiyo kanuni ambayo Mungu hufanyia kazi katika Enzi ya Neno.

Jumatano, 24 Oktoba 2018

Swahili Christian Skit | "Baba Yangu, Mchungaji" | A Debate on the Bible in a Family


Utambulisho


Swahili Christian Skit | "Baba Yangu, Mchungaji" | A Debate on the Bible in a Family

Chi Shou, mchungaji wa dini ambaye amekuwa muumini wa Bwana kwa miaka arubaini, daima ameshikilia mitazamo kwamba "maneno na kazi yote ya Bwana yako ndani ya Biblia," na kwamba "imani katika Bwana haiwezi kuacha Biblia, na kuiamini Biblia humaanisha kumwamini Bwana."

Jumatano, 3 Oktoba 2018

Dondoo za Filamu za Injili "Sauti Nzuri Ajabu" (1) - Je, Ni Vipi Unabii wa Kurudi kwa Bwana Yesu Unatimia?


🎬👀~~~~🌻🌻🌻🌻🌻******     💓💓💓

Dondoo za Filamu za Injili "Sauti Nzuri Ajabu" (1) - Je, Ni Vipi Unabii wa Kurudi kwa Bwana Yesu Unatimia?

Watu wengi katika ulimwengu wa kidini hufuata unabii unaosema kwamba Bwana atashuka akiwa juu ya wingu na wanamsubiria Yeye kuja kwa njia hiyo kisha kuwanyakua hadi kwenye ufalme wa mbinguni, lakini wanapuuza unabii mbalimbali wa Bwana kuhusu kuja kwa siri: "Tazama, mimi nakuja kama mwizi" (Ufunuo 16:15). "

Jumanne, 25 Septemba 2018

Kuuonja Upendo wa Mungu Katikati ya Dhiki(I)

Kuuonja Upendo wa Mungu Katikati ya Dhiki(I)

Chen Lu Wilaya ya Tonglu, Mkoa wa Zhejiang
Nilizaliwa miaka ya 1980 katika kijiji—tulikuwa tumekuwa familia ya wakulima kwa vizazi vingi. Nilijiingiza katika masomo yangu ili niweze kuhitimu kuingia katika chuo na kuepuka maisha ya kijijini ya umasikini na hali ya kuwa nyuma. Nilipoanza shule ya upili, nilikutana na Historia ya Sanaa ya Magharibi, na wakati nilipoona picha nyingi za kupendeza kama vile "Mwanzo," "Bustani ya Edeni," na "Mlo wa Mwisho," ni hapo tu nilipojua kwamba kulikuwa na Mungu katika ulimwengu aliyeumba vitu vyote. Sikuweza kujizuia kuwa na moyo uliojaa hamu ya Mungu.

Jumapili, 23 Septemba 2018

ushuhuda wa Kanisa la Mwenyezi Mungu | Kuinuka Kupitia Ukandamizaji wa Giza(I)

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Mateso ya Kidini

Kuinuka Kupitia Ukandamizaji wa Giza(I)

Mo Zhijian Mkoa wa Guangdong
Nilizaliwa katika eneo maskini, la mbali lenye milima ambako tumefukiza na kumwabudu Budha kwa vizazi vingi. Kuna hekalu za Budha sehemu hiyo kote ambako familia zote zingekwenda kuchoma uvumba; hakuna mtu yeyote aliyewahi kumwamini Mungu kamwe. Katika mwaka wa 1995, mimi na mke wangu tulikuwa katika sehemu nyingine ya nchi ambapo tulimwamini Bwana Yesu; baada ya sisi kurudi tulianza kushiriki injili na idadi ya watu ambao waliikubali ilikua polepole hadi watu zaidi ya 100.

Ijumaa, 7 Septemba 2018

Swahili Praise and Worship Song "Ushuhuda wa Maisha" | Overcomers' Testimonies


Utambulisho


Swahili Praise and Worship Song "Ushuhuda wa Maisha" | Overcomers' Testimonies

Siku moja huenda nikakamatwa na kuteswa na CCP,
kuteseka huku ni kwa ajili ya haki, ambayo najua moyoni mwangu.
Maisha yangu yakitoweka mara moja ghafla bin vu,
bado nitasema kwa fahari kwamba nimemkubali Kristo wa siku za mwisho.

Jumapili, 5 Agosti 2018

Upendo wa Mungu ni wa Kweli Kabisa

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Upendo wa Mungu,

Upendo wa Mungu ni wa Kweli Kabisa


🌻🌻🌻🌻🌻🌻🌻   *************         🌺🌺🌺🌺
Wenzhong , Beijing
Agosti 11, mwaka wa 2012
Usiku wa Julai 21, mwaka wa 2012, tulikuwa na mafuriko makubwa hapa, ambayo hutokea kwa nadra. Ningependa kumwambia kila mtu aliye na kiu ya Mungu kile nilichokipitia kwa kweli na kukiona wakati huo.
Siku hiyo mume wangu nami tuliutunza uga wa chakula kikavu cha mifugo wa dada yangu. Wakati wa usiku mvua nzito iliendelea kunyesha, na tulienda kulala mapema sana. Saa nne kasorobo usiku ndugu mkwe wangu wa kiume aliita akisema:

Jumanne, 24 Julai 2018

Shahidi uzoefu wa Kanisa la Mwenyezi Mungu | Mabadiliko ya Mtu Aliyeanguka(1)

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, wokovu,

Shahidi uzoefu wa Kanisa la Mwenyezi Mungu | Mabadiliko ya Mtu Aliyeanguka

Tong Xin    Mkoa wa Fujian
💓💓💓💓    *************         🌺🌺🌺🌺

Nilizaliwa vijijini. Nilitoka kwa nasaba ya wakulima wanyenyekevu na zaidi ya hayo familia yetu ilikuwa na watu wachache, kwa hiyo mara nyingi tulikuwa tunadhulumiwa. Nilipokuwa na umri wa miaka 13, kulikuwa na mtoto aliyepigwa na mtu fulani kutoka nje ya kijiji chetu. Wanakijiji walimlaumu kwa uongo baba yangu kwa kuchochea hilo na wakasema walitaka kupekua nyumba yetu na kuchukua ngawira mali yetu, kuchukua nguruwe wetu na hata kumpiga baba yangu. Kulikuwa na wakati pia ambapo mwanakijiji mwingine alichukua wavu wetu wa uvuvi na kuuweka kama wake mwenyewe.

Ijumaa, 6 Julai 2018

Vigezo vya Mtu Mwema Kwa Dhati

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Injili

Vigezo vya Mtu Mwema Kwa Dhati

Moran   Mji wa Linyi, Mkoa wa Shandong
Tangu nilipokuwa mtoto, siku zote nilishikiza umuhimu mkubwa kwa jinsi watu wengine walivyoniona na ukadiriaji wao kwangu. Ili niweze kupata sifa kutoka kwa wengine kwa kila kitu nilichokifanya, sikubishana na yeyote asilani wakati wowote kitu chochote kilichoibuka, ili kuepuka kuharibu picha nzuri watu wengine walikuwa nayo kwangu. Baada ya kuikubali kazi ya Mungu katika siku za mwisho, niliendelea kwa njia hii, nikizingatia kwa kila njia iwezekanayo picha nzuri ambayo ndugu zangu wa kiume na wa kike walikuwa nayo kwangu. Hapo awali, wakati nilipokuwa ninasimamia kazi, kiongozi wangu mara nyingi angesema kwamba utendaji wangu ulikuwa kama “bwana ndiyo,” wala sio utendaji wa mtu ambaye huweka ukweli katika vitendo. Sikuathiriwa nalo asilani, lakini kwa kinyume kama watu wengine walinifikiria kuwa mtu mzuri, basi nilihisi kuridhika.

Jumatatu, 2 Julai 2018

Sura ya 32. Ni Watu wa Aina Gani Watakaoadhibiwa

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Mwenyezi Mungu

Sura ya 32. Ni Watu wa Aina Gani Watakaoadhibiwa

Mwenyezi Mungu alisema, Kukufuru na kashfa dhidi ya Mungu ni dhambi ambayo haitasamehewa kwa enzi hii na enzi ijayo na wale wanaofanya dhambi hii hawatazaliwa upya kamwe. Hili linamaanisha kwamba tabia ya Mungu haiwezi kuvumilia kosa la wanadamu. Watu wengine wanaweza kusema maneno yasiyofaa au maneno mabaya wakati hawaelewi, au wanapodanganywa, kuwekewa vikwazo, kudhibitiwa, au kukandamizwa na wengine.

Jumanne, 19 Juni 2018

Umeme wa Mashariki | Kuona Uhalisi Wangu Kwa Dhahiri



Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Injili

Umeme wa Mashariki | Kuona Uhalisi Wangu Kwa Dhahiri

Xiaoxiao Jijini Xuzhou, Mkoani Jiangsu
Kwa sababu ya mahitaji ya kazi ya kanisa, nilihamishwa mpaka mahali pengine ili kutimiza wajibu wangu. Wakati huo, kazi ya injili mahali pale ilikuwa katika hali duni, na hali ya akina kaka na dada kwa kawaida haikuwa nzuri. Lakini kwa kuwa nilikuwa nimeguswa na Roho Mtakatifu, bado nilijitwisha kila kitu nilichoaminiwa nacho kwa matumaini kamili. Baada ya kukubali kuaminiwa, nilihisi uwajibikaji kamili, kupata nuru kamili, na hata nikafikiri kwamba nilikuwa na uamuzi kiasi fulani. 

Jumamosi, 16 Juni 2018

Sura ya 27. Ni Nini Maana ya “Kumkosea Mungu”

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Mwenyezi Mungu

Sura ya 27. Ni Nini Maana ya “Kumkosea Mungu

Mwenyezi Mungu alisema, Ukilibadilisha au kulikanganya neno la Mungu Mwenyewe, basi hiyo ni sawa na uasi wa Mungu, kukufuru dhidi Yake na usaliti. Hii ni sawa tu na malaika mkuu kusema:"Mungu, Unaweza kuumba mbingu na ardhi na vitu vyote na Unaweza kufanya miujiza, lakini pia mimi ninaweza. Unapanda juu kwenye kiti cha enzi, na hivyo hivyo mimi pia napanda. Unatawala mataifa yote, Ninatawala mataifa yote pia.

Jumatatu, 4 Juni 2018

Umeme wa Mashariki | Kuvunja Pingu

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Injili


Umeme wa Mashariki | Kuvunja Pingu 

Zhenxi Jijini Zhenzhou, Mkoani Hena

Miaka kumi iliyopita, nikiendeshwa na asili yangu ya kiburi, sikuweza kamwe kutii kikamilifu mipangilio ya kanisa. Ningetii ikiwa ilinifaa, lakini iwapo haingenifaa ningechagua iwapo ningetii au la. Hili lilisababisha kukiuka sana mipangilio ya kazi wakati wa kutimiza wajibu wangu. Nilifanya jambo langu mwenyewe na kuichukiza tabia ya Mungu, na hivyo baada ya hapo nilitumwa nyumbani.