Jaweni na Upendo kwa Ajili ya Mungu | Muziki wa Akapela "Yasifu Maisha Mapya"

Haleluya! Twakushukuru na kukusifu Wewe, Mwenyezi Mungu! Kristo wa siku za mwisho ameonekana, akifanya kazi na kuzungumza miongini mwa wanadamu. Neno lake hutuhukumu, kutuadibu na kututakasa, likituongoza kwenye njia sahihi ya maisha ya binadamu.

Ukaribisheni Urejeaji wa Bwana Yesu | Sifa na Ibada “Mungu Ameleta Utukufu Wake Mashariki”

Mungu aliipa Israeli utukufu Wake kisha Akauhamisha mbali na pale, na kuwaleta Waisraeli na kuwaleta watu wote Mashariki. Mungu amewaelekeza wote kwenye mwanga ili waweze kuungana tena na kuwa pamoja na mwanga, wasilazimike kuutafuta tena, kuutafuta mwanga.

Je, Biblia ndiye Bwana, au ni Mungu? | “Bwana Wangu Ni Nani” ( Filamu za Injili )

Liu Zhizhong ni mzee katika kanisa moja la mtaani la nyumba nchini China. Amekuwa muumini kwa zaidi ya miaka 30, na amesisitiza bila kukoma kwamba “Biblia ni ufunuo wa Mungu,” “Biblia inamwakilisha Mungu, kuamini katika Mungu ni kuamini katika Biblia, kuamini katika Biblia ni kuamini katika Mungu.”

Karibu Kurudi kwa Bwana Yesu | Drama ya Muziki “ Kwaya ya Injili ya Kichina Onyesho la 19” | Haleluya

Mungu ametutunza daima–Yeye amesikiliza maombi yetu! Anajua tumekuwa tukitamani kurejea Kwake! Sasa kwa hakika Amerejea! Tunasubiri nini bado? Tafadhali endelea kutazama drama yenye muziki ya Kanisa la Mwenyezi Mungu—Kila Taifa Humwabudu Mungu wa Vitendo!

NYENDO ZA MATESO YA KIDINI NCHINI CHINA (Christian Videos) swahili

Wakristo wanaoteswa katika filamu hii ni watu kutoka kwa vikundi vya kidini na madhehebu tofauti ambao walitafuta ukweli, na ambao waliisikia sauti ya Mungu na hivyo wakarudi kwa Mwenyezi Mungu.

Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Kazi-ya-Mungu. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Kazi-ya-Mungu. Onyesha machapisho yote

Jumapili, 20 Oktoba 2019

Maneno ya Roho Mtakatifu | “Kiini Cha Kristo Ni Utiifu kwa Mapenzi ya Baba wa Mbinguni” (Dondoo 1)

Maneno ya Roho Mtakatifu | “Kiini Cha Kristo Ni Utiifu kwa Mapenzi ya Baba wa Mbinguni” (Dondoo 1)


Mwenyezi Mungu anasema, “Mungu mwenye mwili Anaitwa Kristo, na Kristo ni mwili uliovishwa na Roho wa Mungu. Mwili huu ni tofauti na wa mwanadamu yeyote aliye wa nyama. Tofauti hii ni kwa sababu Kristo sio wa mwili na damu bali ni mwili wa Roho. Anao ubinadamu wa kawaida na uungu kamili. Uungu Wake haujamilikiwa na mwanadamu yeyote. Ubinadamu Wake wa kawaida unaendeleza shughuli Zake zote za kawaida katika mwili, wakati uungu Wake unafanya kazi ya Mungu Mwenyewe. Basi iwe ubinadamu Wake au uungu, yote hujiwasilisha kwa mapenzi ya Baba wa mbinguni. Kiini cha Kristo ni Roho, yaani, uungu. Kwa hivyo, chemichemi Yake ni ile ya Mungu Mwenyewe; Dutu hii haitapinga kazi Yake Mwenyewe, na Yeye hangeweza kufanya kitu chochote kinachoharibu kazi Yake Mwenyewe, wala milele Yeye kutamka maneno yoyote ambayo yanakwenda kinyume na mapenzi Yake Mwenyewe. Kwa hiyo, Mungu mwenye mwili kamwe hangefanya kazi yoyote ambayo inasumbua usimamizi Wake Mwenyewe. Hili ndilo ambalo binadamu wote wanapaswa kuelewa. Kiini cha kazi ya Roho Mtakatifu ni kuokoa binadamu na ni kwa ajili ya usimamizi wa Mungu Mwenyewe. Vile vile, kazi ya Kristo ni kuokoa binadamu na ni kwa ajili ya mapenzi ya Mungu. Kutokana na kwamba Mungu Anapata mwili, Anatambua dutu Yake ndani ya mwili Wake, kama kwamba mwili Wake ni wa kutosha kufanya kazi Yake. Kwa hivyo, kazi zote za Roho wa Mungu zinabadilishwa na kazi ya Kristo wakati wa kupata mwili, na kwenye msingi wa kazi zote wakati wa kupata mwili ni kazi ya Kristo. Haiwezi kuchanganyika na kazi yoyote ile kutoka enzi nyingine yoyote. Na kwa kuwa Mungu Anakuwa mwili, Yeye Anafanya kazi katika utambulisho wa mwili Wake; kwa kuwa Yeye hukuja katika mwili, kisha Yeye humaliza katika mwili kazi hiyo Anayoazimia kufanya. Iwe ni Roho wa Mungu au ni Kristo, wote ni Mungu Mwenyewe, na Anafanya kazi hiyo Anayoazimia kufanya na hufanya huduma hiyo Anayopaswa kufanya.”
Tazama Video: Wimbo wa Kuabudu "Viumbe Wote Lazima Waje Chini ya Utawala wa Mungu" | Manifestation of Power of God

Alhamisi, 17 Oktoba 2019

Wimbo wa Kusifu na Kuabudu | “Matendo Ya Mungu Yanajaza Ulimwengu Mzima Tupu” | Kenyan gospel music

Wimbo wa Kusifu na Kuabudu | “Matendo Ya Mungu Yanajaza Ulimwengu Mzima Tupu” | Kenyan gospel music
I Mungu anatazama chini juu ya vitu vyote kutoka juu, na Anatawala vitu vyote kutoka juu. Wakati huo huo, Mungu ametuma wokovu Wake juu ya dunia. Mungu anaangalia kutoka mahali Pake pa siri kila wakati, kila hatua ya mwanadamu, kila kitu anachosema na kufanya. Mungu anamjua mwanadamu kama kiganja cha mkono Wake. Mahali pa siri ni makao ya Mungu, anga ndicho kitanda Mungu akilaliacho. Nguvu ya Shetani haiwezi kumfikia Mungu, kwani Yeye amejawa na utukufu, haki, na hukumu. II Mungu amekanyaga vitu vyote na miguu Yake, Yeye ananyosha mtazamo Wake juu ya ulimwengu. Na Mungu ametembea kati ya wanadamu, ameonja utamu na uchungu, ladha zote za dunia ya mwanadamu; lakini wanadamu, kamwe hawakumtambua Mungu kweli, wala hawakumwona Mungu alipokuwa akitembea ughaibuni. Kwa sababu Mungu alikuwa kimya, na hakufanya matendo yasiyo ya kawaida, hivyo, hakuna aliyemwona kweli. Vitu haviko vilivyokuwa awali: Mungu anaenda kufanya vitu ambavyo, katika enzi zote, ulimwengu haujawahi kuona, Mungu anaenda kunena maneno ambayo, katika enzi zote, wanadamu hawajawahi kusikia, kwa sababu Yeye anawataka binadamu wote waje kumjua Mungu katika mwili. kutoka katika Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya
Tazama Video: Wimbo wa Injili | Mungu Hutumaini Mtu Anaweza Kumjua na Kumwelewa | Mahitaji ya Mungu kwa Wanadamu

Jumatatu, 14 Oktoba 2019

Maneno ya Roho Mtakatifu | “Matamshi ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima Tamko la Kumi na Tisa”


Maneno ya Roho Mtakatifu | “Matamshi ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima Tamko la Kumi na Tisa”
Ni wajibu wa mwanadamu kuchukua maneno Yangu kama msingi wa maisha yake. Mwanadamu lazima aanzishe fungu lake binafsi katika kila sehemu ya maneno Yangu; kutofanya hivyo kutakuwa kuuliza matata, kutafuta maangamizo yake mwenyewe. Binadamu haunijui, na kwa sababu ya hili, badala ya kuleta maisha yake Kwangu badala, anachofanya ni kujipanga tu mbele Yangu na takataka mikononi mwake, na hivyo kujaribu kuniridhisha.

Ijumaa, 11 Oktoba 2019

Neno la Mungu | “Matamshi ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima Tamko la Ishirini na Tisa” (Dondoo 1)

Neno la Mungu | “Matamshi ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima Tamko la Ishirini na Tisa” (Dondoo 1)

Mwenyezi Mungu anasema, “Mimi Natawala katika ufalme, na zaidi ya hapo, Ninatawala katika ulimwengu mzima; Mimi ni Mfalme wa ufalme na pia Mkuu wa ulimwengu. Kutoka wakati huu na kuendelea, Nitawakusanya wote wasio wateule na Nitaanza kufanya kazi Yangu katika mataifa, Na Nitatangaza amri Yangu ya utawala kwa ulimwengu mzima, ili kwa mafanikio Niweze kuingia katika hatua ifuatayo ya Kazi Yangu. Mimi nitatumia kuadibu ili kueneza kazi Yangu katika Mataifa, ambayo ni kusema, Nitatumia nguvu dhidi ya wale wote walio watu wa Mataifa. Kwa kawaida, kazi hii itafanyika kwa wakati mmoja na ile Kazi Yangu miongoni mwa wale waliochaguliwa. Wakati watu Wangu wanatawala na kushika madaraka duniani ndio pia itakuwa siku ambayo watu wote duniani watakuwa wameshindwa, na zaidi ya hayo, utakuwa wakati Wangu wa mapumziko—na hapo tu ndipo Nitawaonekania wale walioshindwa. Mimi huonekana kwa ufalme mtakatifu, na kujificha kutoka kwa nchi ya uchafu. Wote walioshindwa na kuwa watiifu mbele Yangu wana uwezo wa kuuona uso Wangu kwa macho yao wenyewe, na uwezo wa kusikia sauti Yangu kwa masikio yao wenyewe. Hii ni baraka ya wale waliozaliwa katika siku za mwisho, hii ni baraka Niliyoamua kabla, na hii haiwezi kubadilishwa na mwanadamu yeyote. Leo, Ninafanya kazi kwa namna hii kwa ajili ya kazi ya baadaye. Kazi Zangu zote zinahusiana, katika yote kuna wito na mwitikio: Kamwe hakuna hatua yoyote iliyokoma kwa ghafla, na kamwe hakuna hatua yoyote iliyofanywa kwa kujitegemea kivyake. Je, hivi sivyo ilivyo? Je, kazi ya siku za nyuma siyo msingi wa kazi ya leo? Je, maneno ya zamani si utangulizi wa maneno leo? Je, hatua za zamani si asili ya hatua za leo? Wakati Ninafungua rasmi hati ya kukunjwa ndio wakati watu ulimwenguni kote wanaadibiwa, wakati watu wote duniani wanakabiliwa na majaribu, na ndicho kilele cha Kazi Yangu; watu wote wanaishi katika nchi bila mwanga, na watu wote wanaishi huku kukiwa na tishio la mazingira yao. Kwa maneno mengine, ni maisha ambayo mwanadamu hajawahi kupitia kutoka wakati wa uumbaji mpaka siku ya leo, na hakuna yeyote katika enzi zote aliyeweza ‘kustarehe’ na aina hii ya maisha, na hivyo Ninasema kwamba Ninafanya kazi ambayo haijawahi kufanyika mbeleni. Hii ndiyo hali halisi ya mambo, na hii ni maana ya ndani. Kwa sababu siku Yangu inakaribia kwa wanadamu wote, kwa sababu haionekani kuwa mbali, lakini iko mbele ya macho ya mwanadamu, ni nani asiyeweza kuwa na uoga kwa sababu ya jambo hili? Ni nani asiyekuwa na furaha katika hili? Mji mchafu wa Babeli hatimaye umefika mwisho wake; mwanadamu amekutana na dunia mpya kabisa, na mbingu na dunia zimebadilishwa na kufanywa mpya.”

Iliyotazamwa Mara Nyingi: Wimbo wa Kuabudu 2019 | "Mungu Anashuka na Hukumu" | Christ of the Last Days Has Appeared

Jumamosi, 5 Oktoba 2019

Neno la Mungu: Sura ya 87

Neno la Mungu: Sura ya 87

Lazima uharakishe hatua na ufanye kile Nataka kufanya. Hii ni kusudi Langu lenye hamu kwenu. Inawezekana kuwa kwa wakati huu bado hamjaelewa maana ya maneno Yangu? Inawezekana kuwa bado hamjui kusudi Langu? Nimezungumza wazi zaidi na zaidi, na kusema mengi zaidi, lakini, je, ninyi hamjajitahidi kujaribu kuelewa maana ya maneno Yangu? Shetani, usifikiri kwamba unaweza kuharibu mpango Wangu! Wale wanaomtumikia Shetani, yaani, uzao wa Shetani (hii inahusu wale ambao wanamilikiwa na Shetani.Wale wanaomilikiwa na Shetani kwa hakika wana uhai wa Shetani, na kwa hivyo wanaitwa kuwa uzao wa Shetani) wanaomba rehema miguuni Pangu, wanalia na kusaga meno yao, lakini Siwezi kufanya kitu kama hicho cha kijinga! Ninaweza kumsamehe Shetani? Ninaweza kuleta wokovu kwa Shetani? Haiwezekani! Ninafanya kile Ninachosema na Siwezi kujuta kamwe!
Chochote Ninachosema kinakuja kutukia, si hivyo? Lakini ninyi bado kila mara hamniamini, mnashuku maneno Yangu, na kufikiri kwamba Ninawafanyia mzaha. Hiyo kwa kweli ya dhihaka. Mimi ni Mungu Mwenyewe! Mnaelewa? Mimi ni Mungu Mwenyewe! Ikiwa Sina hekima na sina nguvu, Ninaweza tu kufanya na kusema kama inavyonipendeza? Lakini bado hamniamini. Nimesisitiza mara kwa mara kwenu, na Nimewaambia mara kwa mara. Ni kwa nini wengi wenu bado hawaamini? Kwa nini bado mna mashaka? Kwa nini mnamshikilia kabisa mawazo yenu wenyewe? Yanaweza kukuokoa? Ninatenda kile ninachosema. Nimewaambia mara nyingi: Angalieni maneno Yangu kuwa ni ya kweli na msishuku. Je, mmechukulia maneno Yangu kwa uzito? Wewe peke yako huwezi kufanya chochote, lakini huwezi kuamini katika kile Ninachotenda. Ni nini kinaweza kusemwa juu ya mtu kama huyo? Kusema wazi wazi, ni kama kwamba Sikuwahi kuwaumba kamwe, ambayo ni kusema, wewe hujahitimu katika kila hali kuwa mtumishi Wangu. Kila mtu lazima aamini maneno Yangu! Wote wanapaswa kupitia jaribio—Sitamuacha mtu yeyote kukwepa. Bila shaka, hii ni isipokuwa wale wanaoamini. Watu wanaoamini maneno Yangu kwa hakika watapata baraka Yangu, ambayo utapewa kulingana na kile unachoamini, na itatimizwa ndani yako. Wana Wangu wazaliwa wa kwanza! Sasa, Ninaanza kuwapa baraka Zangu zote. Mtaanza kuvitupa vifungo vyote vinavyochukiza vya mwili kidogo na kidogo: ndoa, familia, kula, kuvaa, kulala, majanga yote ya asili (upepo, jua, mvua, dhoruba inayouma, shida ya kuanguka kwa theluji, na mambo mengine yote mnayochukia). Ninyi mtasafiri baharini, ardhini, na angani bila kuathiriwa na vizuio vya anga, wakati, au jiografia, kujifurahisha kikamilifu katika kumbatio Langu la upendo, mkiwa na wajibu juu ya kila kitu chini ya utunzaji Wangu wa upendo.
Ni nani asiyejivunia wana Wangu wazaliwa wa kwanza ambao Nimewafanya wakamilifu? Ni nani asiyelisifu jina Langu kwa ajili ya wana Wangu wazaliwa wa kwanza? Kwa nini sasa Ninataka kuwaonyesha siri nyingi sana? Mbona si katika wakati uliopita, lakini leo? Hii yenyewe pia ni siri, wewe unajua? Kwa nini Sikusema hapo nyuma kuwa China ni taifa Nilililolilaani? Na kwa nini Sikuwafichua wale wanaonitumikia? Leo Nawaambieni hili: Leo, kwa maoni Yangu, kila kitu kimetimilika—Ninasema hili kuhusu wana Wangu wazaliwa wa kwanza. (Kwa kuwa leo wana Wangu wazaliwa wa kwanza wametawala pamoja nami, sio tu kuoneka, lakini kwa kweli wanatawala pamoja nami. Kwa sasa, ni kwa yeyote ambaye Roho Mtakatifu anafanya kazi ndani yake ambaye kwa hakika anatawala pamoja nami, na hii inafichuliwa sasa, sio jana, wala kesho.) Leo Ninafichua siri zangu Zangu zote katika ubinadamu wa kawaida kwa sababu wale watu ambao Nataka kuwafichua wamefichuliwa, na hii ni hekima Yangu. Kazi Yangu imeendelea hadi hatua hii: Yaani, kwa wakati huu ni lazima Nitekeleze mpango wa maagizo ya utawala Niliyoamua juu ya wakati huu. Kwa hiyo, Ninawatunukia wana Wangu wazaliwa wa kwanza, wana, watu, na watumishi wa huduma muhuri unaofaa tu, kwa sababu Nina mamlaka na Nitahukumu na kutatawala kwa ukali. Ni nani anayethubutu kutonifanyia huduma kwa utii? Ni nani anayethubutu kunilalamikia? Ni nani anayethubutu kusema kwamba Mimi si Mungu wa haki? Najua, asili yenu ya kipepo imefichuliwa kwa muda mrefu mbele Yangu: Kwa yeyote Ninayekuwa mwema kwake, ninyi mnamwonea wivu na mnamchukia. Hii ni asili ya Shetani kabisa! Mimi ni mwema kwa wana Wangu—je, unathubutu kusema kuwa Mimi si mwenye haki? Naweza kukufukuza kabisa. Kwa bahati nzuri wewe unanifanyia huduma na sasa sio wakati; vinginevyo, Ningekuwa nimekufukuza!
Aina ya Shetani! Acheni kuwa washenzi! Msiseme tena! Msitende tena! Kazi Yangu imeanza kufanywa kati ya wana na watu Wangu waliochaguliwa, na tayari inaenea katika mataifa yote, makundi yote, madhehebu yote, na kazi zote za maisha nje ya China. Ni kwa nini wale wanaonipa huduma kila mara huzuiwa kiroho? Ni kwa nini hawaelewi kamwe mambo ya kiroho? Ni kwa nini kila mara Roho Yangu haifanyi kazi kwa watu hawa? Kwa ujumla, Siwezi kutumia nguvu nyingi sana juu ya wale ambao Sikuwaamulia kabla au kuwagua. Mateso Yangu yote ya awali, bidii Yangu ya kazi ya ulinzi imekuwa kwa wana Wangu wazaliwa wa kwanza na sehemu ndogo ya wana na watu, na zaidi ya hayo, pia wamekuwa kwa niaba ya kukamilika kwa ufanisi wa kazi Yangu ya baadaye, ili mapenzi Yangu yasizuiliwe. Kwa sababu Mimi ni Mungu Mwenye busara Mwenyewe, Nimepanga vizuri kila hatua. Mimi sijitahidi kwa vyoyote kubaki na mtu yeyote (hii inaelekezwa kwa wale ambao hawakuchaguliwa au kuamuliwa kabla), na Sitamuangusha mtu yeyote kwa bahati (hii inaelekezwa na waliochaguliwa na kuamuliwa kabla): Hii ni amri Yangu ya utawala, ambayo hakuna mtu anayeweza kuibadilisha! Kwa wale ambao Ninawachukia, Mimi ni mkatili; kwa wale Ninaowapenda, Ninawalinda na kuwahifadhi. Kwa hiyo, Ninatenda kile Ninachosema (Ninaowachagua, wamechaguliwa; Ninaowaamulia kabla, wameamuliwa kabla; haya ni mambo Yangu ambayo Nimeyapanga kabla ya uumbaji).
Nani anaweza kubadilisha moyo Wangu? Isipokuwa Mimi kufanya kulingana na mipango Ninayofanya Nitakavyo, ni nani anathubutu kutenda kwa pupa na kutotii amri Yangu? Hizi ni amri Zangu za utawala, na ni nani anayethubutu kuondoa moja yao kutoka Kwangu? Wote lazima wawe katika amri Yangu. Watu wengine wanasema, mtu huyo ameteseka sana, na ni mwaminifu na anafikiria moyo Wangu kabisa, lakini kwa nini hakuchaguliwa? Hii pia ni amri Yangu ya utawala. Nikisema mtu anaupendeza moyo Wangu, basi mtu huyo anaupendeza moyo Wangu na ni yule Ninayempenda; Nikisema kwamba mtu ni mtoto wa Shetani, basi mtu huyo ni yule Ninayemchukia. Usimpendekeze mtu yeyote! Je, unaweza kumng’amua? Haya yote yanaamuliwa na Mimi. Mwana ni mwana daima, na Shetani ni Shetani daima, ambayo ni kusema, asili ya mwanadamu haibadiliki. Isipokuwa Mimi Niwafanye wabadilike, wote watafuata aina yao wenyewe na hawawezi kamwe kubadilika!
Ninafichua siri Zangu kwenu kazi Yangu inavyoendelea. Leo, kazi Yangu imeendelea hadi hatua gani, je, mnajua kwa kweli? Je, mtafuata kwa kweli uongozi wa Roho Wangu kufanya kile Ninachofanya na kusema kile Ninachosema? Ni kwa nini Nasema kuwa China ni taifa ambalo Nimelilaani? Kwanza, Niliwaumba Wachina wa leo kwa sura Yangu. Hawakuwa na roho, na mwanzoni wao walipotoshwa na Shetani na hawangeweza kuokolewa. Kwa hivyo Niliwakasirikia watu hawa na nikawalaani. Ninawachukia watu hawa zaidi, na Ninakasirika wanapotajwa kwa sababu ni watoto wa joka kubwa jekundu. Kutokana na hili mtu anaweza kufikiria wakati ambapo nchi za dunia zimetwaa kwa nguvu China. Bado ni vivyo hivyo leo, na yote imekuwa laana Yangu—hukumu Yangu yenye nguvu zaidi dhidi ya joka kubwa jekundu. Hatimaye, Nikawaumba aina nyingine ya watu, ambao pamoja nao Niliwaamulia kabla wana Wangu wazaliwa wa kwanza, wana, watu, na wale wanaonifanyia huduma, kwa hivyo kile Ninachofanya leo Nilipanga kitambo kufanya. Kwa nini wale walio katika mamlaka nchini China wanatesa mara kwa mara na kuwadhulumu ninyi? Ni kwa sababu joka kubwa jekundu halifurahii laana Yangu na ananipinga. Lakini ni chini ya aina hii ya mateso na tishio hasa kwamba Mimi huwakamilisha wana Wangu wazaliwa wa kwanza kurudisha mashambulio dhidi ya joka kubwa jekundu na watoto wake. Baadaye Nitawaainisha. Baada ya kusikiliza maneno Yangu, je, mnaelewa umuhimu wa kuwaruhusu kutawala pamoja nami? Ninaposema kwamba joka kubwa jekundu limesononeshwa kabisa hadi kifo chake, pia ni wakati wana Wangu wazaliwa wa kwanza watawale pamoja nami. Mateso ya joka kubwa jekundu ya wana Wangu wazaliwa wa kwanza hutoa huduma sana Kwangu, na wakati wana Wangu wanapokua na wanaweza kusimamia masuala ya nyumba Yangu, basi watumishi waovu (watenda huduma) wataondolewa. Kwa sababu wana Wangu wazaliwa wa kwanza watakuwa wakitawala pamoja nami na watakuwa wametimiza makusudi Yangu, Nitawasukuma watenda huduma mmoja baada ya mwingine kwenye ziwa la moto na kibiriti: Kwa vyovyote vile wanapaswa kwenda! Ninafahamu kikamilifu kwamba aina ya Shetani pia anataka kufurahia baraka Zangu, na hataki kurudi chini ya miliki ya Shetani, lakini Nina amri Zangu ya utawala ambazo kila mtu lazima azingatie na ambazo zinapaswa kutekelezwa, na hakuna mtu anayeachiliwa. Baadaye, Nitawaambieni amri Zangu za utawala moja baada ya nyingine, msije kukosea.

Jumatano, 2 Oktoba 2019

Sauti ya Mungu: Sura ya 88

 Sauti ya Mungu: Sura ya 88

Watu hawawezi tu kuwaza kiasi ambacho mwendo Wangu umezidisha kasi: Ni ajabu ambayo imetokea isiyoeleweka kwa mwanadamu. Tangu uumbaji wa dunia, mwendo Wangu umeendelea na kazi Yangu haijawahi kusimama. Ulimwengu wote hubadilika siku kwa siku na watu pia wanabadilika mara kwa mara. Hizi zote ni kazi Zangu, mipango Yangu yote na hata zaidi, usimamizi Wangu—hakuna mtu anayejua au kuelewa hivi vitu.

Jumatatu, 23 Septemba 2019

Wimbo wa dini | "Ni Wakati Tu Ambapo Mungu Anakuwa Mwili Ndipo Mwanadamu Anaweza Kuwa Mwandani Wake"

Wimbo wa dini | "Ni Wakati Tu Ambapo Mungu Anakuwa Mwili Ndipo Mwanadamu Anaweza Kuwa Mwandani Wake"

Ni Wakati tu Mungu anapojinyenyekeza kwa kiwango fulani, kumaanisha Anakuwa mwili ili kuishi kati ya wanadamu, ndipo wataweza kuwa wasiri Wake, ndipo watakuwa marafiki Zake wa karibu. Mwanadamu anawezaje kupata sifa ya kuwa mwandani wa Mungu Wakati Mungu ni wa Roho, metukuka na mgumu kumwelewa? Ni kwa kuwa tu mwili ulioumbwa sawa na mwanadamu mwanadamu ataweza mapenzi Yake, na kupatwa na Yeye. Mungu hunena na kufanya kazi katika mwili, Akishiriki furaha, huzuni na dhiki ya mwanadamu, Akiishi katika dunia yao, Akiwalinda na kuwaongoza, hivyo Akiwatakasa wapate baraka Yake na wokovu. Mwanadamu anawezaje kupata sifa ya kuwa mwandani wa Mungu Wakati Mungu ni wa Roho, metukuka na mgumu kumwelewa? Ni kwa kuwa tu mwili ulioumbwa sawa na mwanadamu mwanadamu ataelewa mapenzi Yake, na kupatwa na Yeye. Kupitia haya, mwanadamu anaweza kuelewa mapenzi ya Mungu na kuwa mwandani Wake; hili tu ndo la utendaji. Kama Mungu angekuwa asiyeonekana na asiyeguswa na mwanadamu, mwanadamu angekuwaje mwandani Wake? Je, fundisho hili ni bure? Mwanadamu anawezaje kupata sifa ya kuwa mwandani wa Mungu Wakati Mungu ni wa Roho, metukuka na mgumu kumwelewa? Ni kwa kuwa tu mwili ulioumbwa sawa na mwanadamu mwanadamu ataelewa mapenzi Yake, na kupatwa na Yeye. Ni Wakati tu Mungu anapokuwa mwili, ndipo mwanadamu takuwa msiri Wake. kutoka katika Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya
Unaweza Pia Kupenda : Wimbo wa Kuabudu "Viumbe Wote Lazima Waje Chini ya Utawala wa Mungu" | Manifestation of Power of God

Ijumaa, 20 Septemba 2019

Wimbo Mpya wa Dini 2019 | “Zingatia Majaliwa ya Binadamu” | Wokovu wa Mungu (Lyrics Video)


Wimbo Mpya wa Dini 2019 | “Zingatia Majaliwa ya Binadamu” | Wokovu wa Mungu (Lyrics Video)


Mungu awahimiza makabila yote, mataifa na nyanja zote: Sikizeni sauti Yake, muione kazi Yake; mzingatie hatima ya wanadamu; mfanye Mungu Mtakatifu na Mheshimiwa, Mkuu na wa pekee wakuabudiwa, ulimwengu wote, na wanadamu, waishi chini ya baraka Yake Mungu, kama vizazi vya Ibrahimu, walivyoishi na ahadi ya Yehova, kama viumbe vya Mungu, Adamu na Hawa, walivyoishi bustani Edeni. Kazi ya Mungu ni kama mawimbi yavumayo hakuna wa kumzuia au kumsimamisha. Ni tu kwa kusikiza neno Lake na kumuandama, ndio nyayo Zake zinaweza kufuatwa na ahadi pokewa. Wengine wote watapata angamizwa, na kupokea adhabu wanayostahili. Mungu awahimiza makabila yote mataifa na nyanja zote: Sikizeni sauti Yake, muione kazi Yake; mzingatie hatima ya wanadamu. Zingatia hatima ya wanadamu wote u-u-u-u-uh! kutoka katika Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya
Iliyotazamwa Mara Nyingi : Wimbo wa Injili | Mungu Hutumaini Mtu Anaweza Kumjua na Kumwelewa | Mahitaji ya Mungu kwa Wanadamu

Jumanne, 17 Septemba 2019

Wimbo Mpya wa Kuabudu 2019 | “Kristo wa Siku za Mwisho Ameleta Enzi ya Ufalme” (Swahili Gospel Song)


Wimbo Mpya wa Kuabudu 2019 | “Kristo wa Siku za Mwisho Ameleta Enzi ya Ufalme” (Swahili Gospel Song)

Yesu alipokuja katika ulimwengu wa mwanadamu, Akatamatisha Enzi ya Sheria, Alileta Enzi ya Neema. Mungu mara nyingine akakuwa mwili katika siku za mwisho. Akitamatisha Enzi ya Neema, Alileta Enzi ya Ufalme. Wote wanaokubali kupata mwili kwa Mungu kwa mara ya pili wataongozwa katika Enzi ya Ufalme na kupokea uongozi Wake. Baada ya mwanadamu kusamehewa dhambi zake, Mungu alirudi mwilini kumwongoza. Atamwongoza mwanadamu kuingia katika enzi mpya. Ameanza kazi ya hukumu ili kumleta mwanadamu katika ulimwengu wa juu zaidi. Wote wanaotii utawala Wake watavuna ukweli wa juu na baraka kuu. Ee wataishi katika mwangaza! Na kupata njia, ukweli, na uzima! Yesu alifanya kazi nyingi kati ya wanadamu. Ukombozi wa wanadamu wote ndio kazi aliyomaliza pekee. Aligeuka sadaka ya mwanadamu ya dhambi, lakini hakumwondolea mwanadamu tabia yake yote potovu, upotovu wote wa mwanadamu. Kumwokoa mwanadamu kutoka kwa Shetani kulimaanisha Yesu alilazimika kuchukua dhambi za mwanadamu, lakini kazi kubwa zaidi ya Mungu ilihitaji kumwondolea mwanadamu upotovu wa Shetani. Baada ya mwanadamu kusamehewa dhambi zake, Mungu alirudi mwilini kumwongoza. Atamwongoza mwanadamu kuingia katika enzi mpya. Ameanza kazi ya hukumu ili kumleta mwanadamu katika ulimwengu wa juu zaidi. Wote wanaotii utawala Wake watavuna ukweli wa juu na baraka kuu. Ee wataishi katika mwangaza! Na kupata njia, ukweli, na uzima! kutoka katika Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya
Unaweza Pia Kupenda : Wimbo wa Injili "Kiini cha Kristo Ni Mungu" | Differences Between the True Christ and False Christs

Jumamosi, 14 Septemba 2019

Maneno ya Mungu : Sura ya 90

Maneno ya Mungu : Sura ya 90

Wote walio vipofu lazima waondoke kutoka Kwangu na wasiwepo kwa muda zaidi hata kidogo, kwani wale ambao Nataka ni wale ambao wanaweza kunijua, wanaoweza kuniona na wanaoweza kupata vitu vyote kutoka Kwangu. Na wanaoweza kweli kupata vitu vyote kutoka Kwangu ni nani? Hakika kuna wachache sana wa mtu wa aina hii na hakika watapata baraka Zangu.

Jumatano, 11 Septemba 2019

Sauti ya Mungu : Sura ya 91

Sauti ya Mungu : Sura ya 91

Roho Wangu huongea na kutamka sauti Yangu daima—wangapi kati yenu wanaweza kunijua Mimi? Kwa nini lazima Nipate mwili na kuja kati yenu? Hili ni fumbo kubwa. Ninyi mnanifikiria kuhusu Mimi na kunitamani sana siku nzima, na mnanisifu, kunifurahia na kunila na kuninywa kila siku, na ilhali leo bado hamnijui Mimi.

Jumapili, 8 Septemba 2019

Sauti ya Mungu : Sura ya 92

Sauti ya Mungu : Sura ya 92

Kila mmoja anaweza kuuona uweza Wangu na hekima Yangu ndani ya maneno Ninayoyazungumza na mambo Ninayoyatenda. Popote Ninapokwenda, kazi Yangu iko pale. Hatua Zangu haziko nchini China pekee, bali muhimu zaidi, ziko katika mataifa yote ya dunia. Ya kwanza kulipokea jina hili, hata hivyo, ni mataifa saba tu ambayo yamezungumziwa hapo awali, kwani hizi ni hatua za kazi Yangu, na hivi karibuni mtaweza kufahamu kabisa kuihusu na mtaielewa kabisa.

Alhamisi, 5 Septemba 2019

Sauti ya Mungu : Sura ya 93

Sauti ya Mungu : Sura ya 93

Ukweli unatimizwa mbele ya macho ya mtu na mambo yote yametimizwa. Kazi Yangu inapata hatua, ikipanda juu kama roketi iliyofyatuliwa, ambayo hakuna mtu aliwahi kutarajia. Ni baada ya vitu kufanyika ndipo mtaelewa maana ya kweli ya maneno Yangu. Watoto wa joka kubwa jekundu si wa pekee na lazima wafanywe kushuhudia matendo Yangu ya ajabu kwa macho yao wenyewe.

Jumatatu, 2 Septemba 2019

Maneno ya Mungu : Sura ya 94

Maneno ya Mungu : Sura ya 94

Narudi Sayuni pamoja na wazaliwa Wangu wa kwanza—kweli mnaelewa maana ya kweli ya maneno haya? Nimewakumbusha tena na tena kwamba Mimi nataka mkue haraka ili mtawale na Mimi. Je, mnakumbuka? Vitu hivi vyote vinahusiana moja kwa moja na kupata mwili Kwangu. Kutoka Sayuni Nilikuja duniani katika nyama ili Nipate kupitia nyama kundi la watu ambao ni wa akili moja na Mimi, na kisha turudi Sayuni.

Ijumaa, 30 Agosti 2019

Sauti ya Mungu : Sura ya 95

Sauti ya Mungu : Sura ya 95

Watu hufikiri kila kitu kuwa rahisi sana, wakati kwa kweli hali siyo hivyo. Ndani ya kila kitu kuna siri zilizofichwa, na vile vile hekima Yangu na mipango Yangu. Hakuna utondoti usioangaliwa, na yote yanapangwa na Mimi Mwenyewe. Hukumu ya siku kuu inawafikia wale wote wasionipenda kwa kweli (kumbuka, hukumu ya siku kuu inalenga kila mtu anayepokea jina hili) na kuwasababisha kulia na kusaga meno.

Jumanne, 27 Agosti 2019

Sauti ya Mungu : Sura ya 96

Sauti ya Mungu : Sura ya 96

Nitamwadibu kila mtu aliyezaliwa kutoka Kwangu ambaye bado hanijui ili kuonyesha ghadhabu Yangu yote, kuonyesha nguvu Zangu kuu, na kuonyesha hekima Yangu kamili. Ndani Yangu kila kitu ni chenye haki na bila shaka hakuna udhalimu, hakuna udanganyifu, na hakuna upotovu; yeyote ambaye ni mpotovu na mdanganyifu lazima awe ni mwana wa jahanamu—lazima amezaliwa huko kuzimu. Ndani Yangu kila kitu ni cha wazi; chochote Ninachosema kukamilisha kinakamilika na chochote Ninachosema kuanzisha kinaanzishwa, na hakuna mtu anayeweza kubadilisha au kuiga mambo haya kwa sababu Mimi ndimi Mungu Mwenyewe wa pekee.

Jumanne, 6 Agosti 2019

"Kwaya ya Kichina Onyesho la 13" Clip 1 Matukio ya Kuzimu | Kwaya za Injili

  "Kwaya ya Kichina Onyesho la 13" Clip 1 Matukio ya Kuzimu | Kwaya za Injili
Je, unafikiria kuna kuzimu? Je, kuzimu iko namna gani hasa? Tafadhali fuatilia dondoo hii ya video! Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu lilianzishwa kwa sababu ya kuonekana na kazi ya Mwenyezi Mungu, ujio wa pili wa Bwana Yesu, Kristo wa siku za mwisho. Linashirikisha wale wote ambao wanaikubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho na ambao wameshindwa na kuokolewa kwa maneno Yake.

Jumatano, 31 Julai 2019

Neno la Mungu | “Yule tu Anayepitia Kazi ya Mungu Ndiye Anayemwamini Mungu Kweli” (Dondoo)


Neno la Mungu | “Yule tu Anayepitia Kazi ya Mungu Ndiye

Anayemwamini Mungu Kweli” (Dondoo)

Mwenyezi Mungu anasema, “Kuchunguza kitu cha aina hii sio vigumu, lakini kunahitaji kila mmoja wetu ajue ukweli huu: Yeye Aliye mwili wa Mungu Atakuwa na dutu ya Mungu, na Yule Aliye Mungu katika mwili Atakuwa na maonyesho ya Mungu. Kwa maana Mungu Hupata mwili, Ataleta mbele kazi Anayopaswa kufanya, na kwa maana Mungu Amepata mwili, Ataonyesha kile Alicho na Ataweza kuuleta ukweli kwa mwanadamu, kumpa mwanadamu uhai, na Amwonyeshe mwanadamu njia.

Jumapili, 28 Julai 2019

Sauti ya Mungu | Sura ya 98

Sauti ya Mungu | Sura ya 98

Mambo yote yatakuja juu ya kila mmoja wenu, na yatawawezesha kujua zaidi juu Yangu na kuwa na uhakika zaidi juu Yangu. Yatawawezesha kunijua, Mungu mmoja Mwenyewe, kunijua Mimi Mwenye uweza, kunijua Mimi Mungu Mwenyewe mwenye mwili. Baadaye, Nitatoka katika mwili, Nirudi Sayuni, Nirudi katika nchi nzuri ya Kanaani, ambayo ni makazi Yangu, ndiyo hatima Yangu, na ndio msingi ambao niliumba vitu vyote.

Alhamisi, 25 Julai 2019

Wimbo Mpya wa Dini 2019 | "Upendo Safi Bila Dosari" (Lyrics Video)


 

Wimbo Mpya wa Dini 2019 | "Upendo Safi Bila Dosari" (Lyrics Video)

I Upendo ni hisia safi, safi bila dosari. Tumia moyo, tumia moyo, kupenda, kuhisi, kutunza. Upendo hauna masharti, vizuizi au kujitenga. Tumia moyo, Tumia moyo, kupenda, kuhisi, kutunza. Ukipenda hudanganyi, hulalamiki, hugeuki, hutazamii kupata kitu, cha malipo. Ukipenda utajitolea, ukubali taabu, kuwa kimoja, Mungu katika mapatano.