Jumanne, 25 Septemba 2018

Kuuonja Upendo wa Mungu Katikati ya Dhiki(I)

Kuuonja Upendo wa Mungu Katikati ya Dhiki(I)

Chen Lu Wilaya ya Tonglu, Mkoa wa Zhejiang
Nilizaliwa miaka ya 1980 katika kijiji—tulikuwa tumekuwa familia ya wakulima kwa vizazi vingi. Nilijiingiza katika masomo yangu ili niweze kuhitimu kuingia katika chuo na kuepuka maisha ya kijijini ya umasikini na hali ya kuwa nyuma. Nilipoanza shule ya upili, nilikutana na Historia ya Sanaa ya Magharibi, na wakati nilipoona picha nyingi za kupendeza kama vile "Mwanzo," "Bustani ya Edeni," na "Mlo wa Mwisho," ni hapo tu nilipojua kwamba kulikuwa na Mungu katika ulimwengu aliyeumba vitu vyote. Sikuweza kujizuia kuwa na moyo uliojaa hamu ya Mungu. Baada ya kuhitimu kutoka chuo, nilipata kazi nzuri kwa urahisi sana, na kisha nikampata patna mzuri. Hatimaye nilikuwa nimefanikisha matarajio yangu mwenyewe na yale ya mababu zangu. Nilikuwa nimeepuka nasaba ya mababu zangu ya kuuweka uso wao chini na mgongo kuangalia mbinguni, na mwaka wa 2008, kuzaliwa kwa mtoto kuliongeza furaha zaidi kwa maisha yangu. Nikiangalia kila kitu nilichokuwa nacho katika maisha yangu, niliamini kuwa nilistahili niwe na maisha ya furaha, ya kustarehesha. Hata hivyo, wakati nilipokuwa nikifurahia maisha hayo ya kufanikiwa sana, mazuri, sikuweza kamwe kukatisha hisia zisizo yakini za utupu ndani ya moyo wangu. Hili lilinifanya kujihisi kuchanganyikiwa hasa na nisiyejiweza.
Mnamo Novemba ya mwaka wa 2008, familia yangu ilinizungumza kuhusu injili ya siku za mwisho ya Mwenyezi Mungu. Kupitia maneno ya Mungu hatimaye nilielewa kwamba Yeye ndiye chanzo cha maisha ya wanadamu, na kwamba maneno Yake ni msukumo na nguzo za maisha yetu. Tukiacha riziki na chakula cha Mungu kwa maisha yetu, roho zetu zitakuwa tupu na peke yake, na bila kujali ni furaha yakinifu gani tulizo nazo sisi hatutaweza kamwe kuyaridhisha mahitaji ya roho zetu. Kama vile tu Mwenyezi Mungu alivyosema: “Mwanadamu, hata hivyo, ni mwanadamu. Nafasi na maisha ya Mungu hayawezi kubadilishwa na mwanadamu yeyote. Mwanadamu hahitaji tu jamii iliyo na haki, ambapo kila mtu analishwa vyema na ana uhuru na usawa, lakini wokovu wa Mungu na Yeye kuwapa uhai. Wakati tu mwanadamu atapokea wokovu wa Mungu na kupatiwa uhai na Yeye ndipo mahitaji, hamu ya kuchunguza, na utupu wa kiroho wa mwanadamu utaweza kutatuliwa” (“Mungu Anaongoza Majaliwa ya Wanadamu Wote” katika Neno Laonekana katika Mwili). Maneno Yake yaliathiri nafsi yangu ghafla kama chemchemi jangwani, na yaliondoa mchafuko ndani ya moyo wangu. Kuanzia wakati huo kwendelea, nilisoma maneno ya Mungu kwa njaa na kiu kubwa, na daima kulikuwa na hisia zisizoelezeka za utulivu moyoni mwangu kwamba roho yangu hatimaye ilikuwa imekuja nyumbani. Baada ya muda mfupi, kanisa liliwapangia ndugu fulani wa kiume na wa kike kukutana nami, na walifanya hivyo kwa uendelevu bila kujali jinsi hali ya hewa ilivyokuwa kali. Wakati huo, kulikuwa na vitu vingi ambavyo sikuvielewa na hawa ndugu wa kiume na wa kike waliwasiliana nami kwa uvumilivu. Hakukuwa na hata kiasi kidogo cha kuudhika au hata kufurahisha tamaa zangu, na kupitia hili nilihisi kwa kina uaminifu na upendo wa ndugu hawa wa kiume na wa kike. Nilipoelewa zaidi kuhusu ukweli, nilianza kuelewa hamu ya haraka ya Mungu ya kuwaokoa wanadamu, na niliona kuwa ndugu hawa wa kiume na wa kike walijitumia kwa hamu na kuhubiri injili kwa niaba ya Mungu. Nilitaka pia kutimiza wajibu wangu mwenyewe, lakini mtoto wangu alikuwa mdogo na sikuwa na mlezi mwingine, kwa hiyo nilimwomba tu Mungu anipe suluhisho. Baadaye, nilipata habari kwamba kulikuwa na dada mmoja aliyekuwa anasimamia shule ya malezi, hivyo nilimpeleka mtoto wangu kwake. Aliahidi kunisaidia kumtunza mtoto wangu bila kusita, na hata hangekubali karo au gharama za vyakula. Kuanzia wakati huo kwendelea, huyo dada alinisaidia tu kumtunza mtoto wangu wakati wa mchana, lakini wakati mwingine alisaidia usiku pia. Vitendo vya huyo dada vilinigusa kwa undani, na nilijua kuwa haya yote yalitoka kwa upendo wa Mungu. Ili kufidia upendo Wake, nilijiunga na safu ya wale waliohubiri injili bila kusita. Nilipokuwa nikihubiri injili, niliona hali za huzuni za mtu baada ya mtu ambao hawakuwa wameangaziwa na uzuri wa Mungu. Nilisikia vilio vya nyendo zao chungu katika maisha, na pia niliona nyuso zao zilizojaa shangwe na furaha baada ya kupata wokovu wa Mungu wa siku za mwisho. Hili lilisisimua shauku yangu ya uinjilisti hata zaidi, na nikaamua kuleta injili ya Mungu hata kwa watu zaidi walioishi katika giza ambao waliona kiu kwa mwanga! Lakini wakati huo tu, serikali ya CCP ilianza kuwakandamiza sana na kuwafuatilia ndugu wa kiume na wa kike, na pia nilipitia janga hili.
Hiyo ilikuwa asubuhi ya Desemba 21, mwaka wa 2012. Zaidi ya dazeni moja ya ndugu wa kiume na wa kike walikuwa wakikutana nyumbani mwa mwenyeji mmoja kulipokuwa ghafla na mshindo wa kubisha na kupiga kelele mlangoni: "Fungua mlango! Fungua mlango! Ukaguzi wa nyumba!" Dada mmoja alipokuwa akifungua mlango, polisi sita au saba waliokuwa wamebeba virungu walijilazimisha ndani. Kwa ukali walitumamanua na kisha wakaanza kupekua watoto wa meza. Dada mmoja kijana alikuja na kuwauliza: "Tunapanga kwa rafiki yetu na hatukuvunja sheria. Kwa nini mnapekua nyumba?" Polisi walijibu kwa ukali: "Shika adabu! Tukikuambia usimame hapo, simama hapo. Tusipokwambia uzungumze, funga kinywa chako!" Kisha wakamtupa kwa ukatili sakafuni, na wakasema kwa sauti kubwa ya ujeuri: "Ukitaka kubisha tutakupiga!" Ukucha wake wa kidole ulikuwa umevunjika na kidole chake kilikuwa kinavuja damu. Kuona nyuso mbovu za polisi, nilihisi chuki na hofu, kwa hiyo nikamwomba Mungu kimya kimya anipe nguvu na ujasiri, anilinde ili niwe shahidi. Baada ya kuomba, moyo wangu ulitulia sana. Polisi walichukua ngawira vifaa vingi vya kiinjilisti na mkusanyiko wa maneno ya Mungu, kisha wakatuingiza kwa magari ya polisi.
Mara tu tulipofika kituoni, walichukua ngawira kila kitu tulichokuwa tumebeba na kutuhoji ili kujua majina yetu, anwani, na viongozi wetu wa kanisa walikuwa akina nani. Niliogopa kuihusisha familia yangu hivyo sikusema chochote; dada mwingine hakusema chochote pia, kwa hiyo polisi walituona kama viongozi wa waasi na kutayarisha kusikiza kesi yetu mmoja kwa utenganisho. Niliogopa sana hapo—nilikuwa nimesikia kwamba polisi walikuwa hasa katili kwa watu ambao hawakuwa wenyeji, na nilikuwa nimelengwa kuhojiwa. Hilo bila shaka lingemaanisha ukatili zaidi, bahati kidogo. Nilivyokuwa tu katika hali ya kuogofya na kuishi katika hofu, nikamsikia dada yangu aliyekuwa karibu nami akisali: "Ee Mungu, Wewe ni mwamba wetu, kimbilio letu. Shetani yuko chini ya miguu Yako, na niko tayari kuishi kulingana na maneno Yako na kuwa shahidi ili kukuridhisha Wewe!" Baada ya kusikia hayo, moyo wangu ukachangamka. Niliwaza: Ni kweli—Mungu ni mwamba wetu, Shetani yuko chini ya miguu Yake, kwa hiyo ninaogopa nini? Alimradi ninategemea Mungu na kushirikiana na Yeye, Shetani anaweza kushindwa! Ghafla sikuwa na hofu tena, lakini pia nilihisi aibu. Nilifikiria ukweli kwamba wakati huyo dada alipokabiliwa na hili, aliweza kuishi kulingana na maneno ya Mungu na siyo kupoteza imani kwa Mungu, lakini nilikuwa mwepesi wa kutishwa na mwoga. Sikuwa na ujasiri hata kidogo wa mtu ambaye humwamini Mungu. Kwa sababu ya upendo wa Mungu na kupitia sala ya huyo dada ambavyo vilikuwa vimenimotisha na kunisaidia, sikuwa tena na woga wa nguvu za udhalimu za polisi. Niliamua kwa utulivu: Ingawa nimekamatwa leo, nimedhamiria kuwa shahidi ili kumridhisha Mungu. Kabisa sitakuwa mwoga ambaye humsikitisha Mungu!
Takribani saa nne asubuhi, polisi wawili walinitia pingu na kunipeleka kwa chumba fulani ili kunihoji peke yangu. Mmoja wa wale polisi alinena nami kwa lugha ya mahali pale pale. Sikuelewa, na nilipomuuliza alichokuwa amesema, bila kutarajiwa swali hili liliwakasirisha. Mmoja wa polisi aliyekuwa amesimama karibu akasema kwa sauti kubwa: "Wewe hutuheshimu!" Alipokuwa anaongea alikimbia na kuzishika nywele zangu, akanirusha huku na huko. Nilikuwa na kizunguzungu na kutupwa pande zote, na ngozi ya kichwa changu ilihisi kama ilikuwa inaambuliwa na nywele zangu kung'olewa. Baada tu ya hayo, askari mwingine alinijia mbio na kusema kwa sauti kubwa: "Kwa hiyo tunapaswa kuwa wagumu? Sema! Ni nani aliyewafanya mhubiri injili?" Nilijaa hasira na nikajibu: "Kuhubiri injili ni wajibu wangu." Niliposema hivi tu, yule polisi wa kwanza tena akanishika kwa nywele na kunipiga kofi usoni, kunigonga na kusema kwa sauti: "Nitakufanya uhubiri zaidi! "Nitakufanya uhubiri zaidi! Aliugonga uso wangu mpaka ukawa mwekundu kama kiazichekundu kwa maumivu, na ukaanza kuvimba. Alipochoka kunipiga, aliniacha niende, kisha wakachukua simu ya mkononi na kicheza kanda cha MP4 walivyopata nikiwa navyo na kuniuliza habari kuhusu kanisa. Nilitegemea hekima ili kushughulika nao. Kwa Ghafla, askari mmoja akauliza: "Wewe hujatoka hapa. Unazungumza Kimandarini vizuri sana—waziwazi wewe si mtu wastani. Sema ukweli! Kwa nini umekuja hapa? Nani aliyekutuma hapa? Ni nani kiongozi wako? Uliwasilianaje na kanisa hapa? Unaishi wapi?" Kusikia kwamba polisi hawa waliniona kama mtu muhimu na walisisitiza kukusanya taarifa juu ya kanisa kutoka kwangu, nilifadhaika na kumwomba Mungu anipe ujasiri na nguvu. Kupitia sala, moyo wangu polepole ulitulia, na nikajibu: "Sijui chochote." Waliposikia nikisema hayo, waliponda meza kwa ukali na kupaaza sauti: "Wewe subiri tu, tutaona jinsi unavyohisi hivi punde!" Kisha wakachukua kicheza kanda changu cha MP4 na kukichezesha. Niliogopa mno. Sikujua wangetumia mbinu gani kunishughulikia, kwa hiyo kwa haraka nikatoa kilio kwa Mungu. Sikuwa nimewaza ya kwamba kile kilichochezwa kilikuwa ni maneno yaliyorekodiwa ya ushirika juu ya kuingia katika maisha: "Je, unadhani mtu wa aina hiyo anaweza kuokolewa? Yeye hana moyo wa ibada kwa Kristo; yeye si wa wazo moja na Kristo. Anapokabiliwa na matatizo yeye huachana na Kristo na kwenda njia yake mwenyewe. Yeye humkana Mungu, hivyo kumfuata Shetani. … Wakati wa utawala wa joka kubwa jekundu, wakati unapopitia kazi ya Mungu, ikiwa unaweza kulikana joka kubwa jekundu na kusimama upande wa Mungu, bila kujali jinsi linavyokutesa, kukufuatilia, au kukudhulumu, unaweza kabisa kumtii Mungu na unaweza kujitolea kwa Mungu hadi kifo. Ni mtu wa aina hii tu anayestahili kuitwa mshindi, anayestahili kuitwa mtu aliye na mawazo sawa na Mungu" ("Mambo Kumi ya Uhalisi ya Maneno ya Mungu Yanayotakiwa Kuingiwa Ili Kuokolewa na Kufanywa Mkamilifu" katika Mahubiri na Ushirika Juu ya Kuingia Katika Maisha (IV)). Niliposikia maneno "huachana," nilihisi mchomo wa maumivu katika moyo wangu. Sikuweza kujizuia kufikiria kwamba wakati Bwana Yesu alipokuwa akifanya kazi, wale waliomfuata Yeye na kufurahia neema Yake walikuwa wengi, lakini wakati alipotundikwa msalabani na askari wa Kirumi walikuwa wakiwakamata Wakristo kutoka pande zote, watu wengi walikimbia kwa sababu ya hofu. Hili lilimletea Mungu uchungu mkubwa! Lakini basi, kuna tofauti gani kati yangu na wale watu wasio na shukrani? Wakati nilipofurahia neema na baraka za Mungu, nilikuwa na ujasiri mkubwa katika kumfuata Mungu, lakini nilipokabiliwa na taabu ambazo zilinihitaji kuteseka na kulipa gharama, nilikuwa mwepesi wa kutishwa na mwenye kuogopa. Je, hilo lingeufarijije moyo wa Mungu? Nilifikiria ukweli kwamba Mungu alijua wazi kwamba kuwa mwili nchini China, hii nchi iliyotawaliwa na wakana Mungu, kungedhihirisha hatari kubwa, lakini ili kutuokoa sisi watu wapotovu, bado Alikuja mahali hapa pa pepo bila kusita, akivumilia ufuatiliaji wao na ukimbizaji, na Yeye mwenyewe alituongoza kwenye njia ya ukimbizaji wa ukweli. Nikiona nia ya Mungu ya kujitolea kila kitu, kuacha kila kitu ili kutuokoa, ningekosaje, kama mtu aliyefurahia neema ya wokovu Wake, kulipa gharama ndogo kwa ajili Yake? Katika dhamiri yangu nilihisi kukemewa na nilichukia kwamba nilikuwa na ubinafsi sana, duni sana. Nilihisi sana kwamba Mungu alijaa tumaini kwangu na kunijali. Nilihisi kwamba Alijua vizuri kwamba nilikuwa mchanga kwa kimo na niliogopa mbele ya udhalimu wa Shetani; Aliniruhusu kulisikia hili kwa njia ya polisi kucheza maneno yaliyorekodiwa, akiniruhusu kuelewa mapenzi Yake, ili katikati ya dhiki na ukandamizaji ningeweza kuwa shahidi kwa Mungu na kumridhisha. Kwa muda mfupi, niliguswa sana na upendo wa Mungu kiasi kwamba machozi yalinitiririka usoni mwangu, na nikamwambia Mungu kimya kimya: "Ewe Mungu! Sitaki kuwa mtu anayeachana na Wewe na ambaye hukuumiza Wewe; ninataka kukaa na Wewe kupitia furaha na huzuni. Bila kujali jinsi Shetani anavyonisumbua, nimeamua kuwa shahidi na kuufariji moyo Wako."
Kisha kulikuwa na mshindo wa ghafla polisi alipozima kile kicheza kanda, kisha akakurupua kunielekea na kusema kwa chuki: "Hiyo ni kweli, mimi ni joka kubwa jekundu, na leo nimekuja kukuumiza vibaya!" Kisha wakaniamuru nisimame sakafuni miguu mitupu na wakautia mkono wangu wa kulia pingu wakiuunganisha na uzingo wa chuma katikati ya kipande cha saruji. Ilinibidi kusimama kama nimeinama kwa sababu hicho kipande cha saruji kilikuwa kidogo sana. Hawakuniruhusu nichuchumae, wala hawakuniruhusu nitumie mkono wangu wa kushoto ili kuiegemeza miguu yangu. Sikuweza kuendelea kusimama baada ya muda na nilitaka kuchuchumaa, lakini polisi walinijia na kupiga kelele: "Hakuna kuchuchumaa! Ikiwa unataka kuteseka kidogo, fanya haraka na ukiri!" Yote niliyoweza kufanya ilikuwa ni kuyakereza meno yangu na kuvumilia. Sijui ni muda kiasi gani uliopita. Nyayo zangu zilikuwa kama barafu, miguu yangu ilikuwa inauma na yenye ganzi, na wakati kwa hakika sikuweza tena kukaa nimesimama, nilichuchumaa. Polisi waliniinua, wakaleta kikombe cha maji baridi, na wakayamimina kwa shingo yangu. Nilikuwa nahisi baridi sana kiasi kwamba nilianza kutetemeka. Kisha walizifungua pingu zangu, wakanisukuma kwa kiti cha mbao, wakaifunga mikono yangu pingu kwa miisho mkabala ya kiti kile, na kufungua madirisha na kuwasha kiyoyozi. Kulikuwa na dharuba ya ghafla ya upepo iliyonigonga na nilikuwa nikitetemeka kutokana na baridi. Sikuweza kujizuia kuwa na udhaifu katika moyo wangu, lakini katikati ya mateso haya nilikuwa nikisali bila kukoma, nikimwomba Mungu anipe ari na nguvu ya kuyahimili maumivu haya, kuniruhusu kuushinda udhaifu wa mwili. Wakati huo huo, wimbo wa maneno ya Mungu ukaniongoza kutoka ndani: “Hata wakati mwili wako unavumilia mateso, usichukue ushauri kutoka kwa Shetani. … Imani ni kama daraja moja la gogo la mti, wale ambao hushikilia maisha kwa unyonge watakuwa na ugumu katika kulivuka, lakini wale ambao wako tayari kujitolea wenyewe wanaweza kulivuka bila wasiwasi” (“With True Faith Comes Witness” katika Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya). Maneno ya Mungu yalinifanya nielewe kwamba Shetani alitaka kuutesa mwili wangu ili kunifanya nimsaliti Mungu, na kama ningeupuuza mwili ningeshikwa na udanganyifu wake. Nilizichunguza hizi sentensi mbili akilini mwangu, nikijiambia kuwa nilibidi kutahadhari dhidi ya udanganyifu wa Shetani na kuyakataa mawazo yake. Baadaye, polisi walichukua sufuria kubwa ya maji baridi na kuyamwaga yote kwa shingo yangu. Nguo zangu zote zilitota kabisa. Wakati huo nilihisi kama kwamba nilikuwa nimeanguka katika sanduku la barafu. Kuwaona hao polisi, wenye kustahili dharau sana, waovu sana, nilijaa chuki. Niliwaza: Hili kundi la pepo litatumia mbinu zozote ili nimsaliti Mungu—siwezi kuruhusu hila zao kufanikiwa! Wakiona nikitetemeka sana, hao polisi walishika konzi ya nywele zangu na wakakilazimisha kichwa changu kuangalia angani kupitia dirisha, kisha wakasema kwa mzaha: "Je, si wewe unahisi baridi? Basi, mwache Mungu aje akuokoe!" Waliona kwamba sikuwa naonyesha hisia, kwa hiyo polisi mara nyingine tena wakanimwagilia sufuria kubwa ya maji baridi na kuweka kiyoyozi kwenye hali yake ya baridi mno, kisha wakanipulizia moja kwa moja. Dharuba baada ya dharuba ya hewa kali baridi niliyopuliziwa ilinigonga pamoja na upepo baridi. Nilikuwa nahisi baridi sana kiasi kwamba nilikuwa nimejikunyata mithili ya mpira na nilikuwa nimeganda kama jiwe. Nilihisi kwamba mwili wangu wote ulikwisha kuwa mgumu. Imani yangu ilianza kufifia kidogo kidogo, na sikuweza kujizuia kufikiri mawazo ya ujinga: Siku ya baridi hivi, lakini wananilowesha na maji baridi na kuwasha kiyoyozi. Je, wanajaribu kunigandisha nikiwa hai? Kama nitafia hapa, ndugu zangu hata hawatajua kulihusu. Nilipokuwa tu nikizama katika giza, nilifikiria ghafla mateso ambayo Yesu alivumilia alipokuwa akitundikwa msalabani ili kuwakomboa wanadamu. Alikuwa amesema: “Msiwe na hofu ya wao wanaoua mwili, lakini hawana uwezo wa kuifisha roho: ila heri uwe na hofu ya yeye anayeweza kuiangamiza roho pamoja na mwili katika kuzimu” (Mathayo 10:28). Kisha, nilifikiria maneno ya Mungu katika wimbo huu: “… kwa ajili ya kumpenda Mungu, Haijalishi ni lini au vipi Mungu anakufanya upatwe na majaribu Yake, unaweza kutojali ikiwa unaishi au unaangamia, kuachana na kila kitu kwa furaha kwa ajili ya Mungu, na kuvumilia chochote kwa furaha kwa ajili ya Mungu” (“Sitapumzika Mpaka Nimpate Mungu” katika Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya). Maneno haya kutoka kwa Mungu kwa kweli yaliniamsha—ndiyo! Siku hiyo kuweza kushuhudia kwa Mungu ilikuwa ni Yeye akiniinua—ningewezaje kuupuuza mwili? Hata kama ingemaanisha kupoteza maisha yangu, nilikuwa nimeamua kuwa mwaminifu kwa Mungu. Ghafla, kulikuwa na mfuro ndani ya moyo wangu na nikahisi kutiwa moyo sana. Kimya kimya niliomba kwa Mungu: "Ewe Mungu! Umenipa pumzi hii, afadhali nife kuliko kutenda kama msaliti kwako!" Polepole, sikuhisi hasa baridi tena, jambo ambalo liliniruhusu kwa kweli kuhisi urafiki wa Mungu na faraja. Kuanzia adhuhuri hadi takribani saa moja usiku, polisi waliendelea kunihoji. Waliona kwamba singefungua kinywa changu kabisa, kwa hiyo walinifungia katika chumba cha kuhojiwa na kwendelea kunipulizia hewa baridi.
kutoka kwa Ushuhuda wa Kuipitia Hukumu ya Kristo

Tazama zaidi: ushuhuda wa Umeme wa Mashariki

0 意見:

Chapisha Maoni