Jumanne, 5 Februari 2019

Kuteseka kwa Ajili ya Kutenda Ukweli ni kwa Maana Sana

I
Jua kwamba lengo lako ni
kuruhusu maneno ya Mungu kutenda kazi ndani yako,
na kuyajua kweli katika matendo.
Pengine unapambana kuelewa maneno ya Mungu,
lakini utendaji unasaidia kutoa dosari hii.
Lazima ujue ukweli mwingi,
na sio tu kujua lakini pia kutenda.
Hili lazima liwe lengo lako.
Kuna ukweli mwingi unapaswa kujua na pia kutenda.
Hili lazima liwe lengo lako.
II
Yesu aliteseka sana katika miaka Yake thelathini na mitatu na nusu
Alipotenda na kuishi kwa kudhihirisha ukweli.
Yeye alitekeleza mapenzi ya Mungu na kutenda ukweli,
na hii ndiyo sababu Aliteseka hivyo.
Kama Angejua ukweli lakini asitende ukweli,
Hangeteseka hivyo.
Kama Angewafuata Mafarisayo
na mafundisho ya Wayahudi,
Hangeteseka sana,
hapana, Hangeteseka sana.
III
Utendaji wa Yesu unaweza kuonyesha kitu ambacho unafaa kujua.
Ili kazi ya Mungu itimize matokeo,
inahitaji mwanadamu kushiriki.
Hili ni jambo unalopaswa kuelewa,
lazima uelewe, lazima uelewe.
Kama Yesu hangekuwa ametenda ukweli,
Hangeteseka msalabani.
Kama Hangetenda kulingana na mapenzi ya Mungu,
je, Angesema ombi kama hilo la huzuni?
Hivyo, hii ni aina ya uchungu ambao mtu anapaswa kuvumilia,
mtu anapaswa kuvumilia.
Kama Yesu hangekuwa ametenda ukweli,
Hangeteseka msalabani.
Kama Hangetenda kulingana na mapenzi ya Mungu,
je, Angesema ombi kama hilo la huzuni?
Hivyo, hii ni aina ya uchungu ambao mtu anapaswa kuvumilia,
mtu anapaswa kuvumilia.
kutoka katika "Tendeni Ukweli Mara Mnapouelewa" katika Neno Laonekana katika Mwili
kutoka kwa Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya

Tufuate: Asili ya Kanisa la Mwenyezi Mungu,  Sikiliza nyimbo nyimbo za dini

0 意見:

Chapisha Maoni