Jumatatu, 21 Januari 2019

Nyimbo za dini | Muige Bwana Yesu

Nyimbo za diniMuige Bwana Yesu

I
Yesu alikamilisha misheni ya Mungu,
kazi ya ukombozi ya kila mwanadamu
kwa kutoa kujali Kwake kwa mapenzi ya Mungu,
bila madhumuni au mipango ya ubinafsi.
Katikati Aliweka mpango wa Mungu.
Aliomba kwa Baba wa mbinguni,
akitafuta mapenzi ya Baba wa mbinguni.
Angemtafuta na kila mara Angeomba.
Ikiwa kama Yesu utamjali Mungu kabisa
na kuupa mwili kisogo,
Mungu atakuamini na kazi muhimu
kukuwezesha kumtumikia.
II
Aliomba na kusema, "Mungu Baba!
Kamilisha kile ambacho ni mapenzi Yako.
Usitende kulingana na nia Zangu,
tenda ili mpango Wako utimizwe.
Kwa nini Umjali mwanadamu ambaye ni dhaifu,
ambaye ni kama siafu mkononi Mwako?
Ningependa tu kufanya mapenzi Yako.
Fanya ndani Yangu kama Unavyotaka."
Ikiwa kama Yesu utamjali Mungu kabisa
na kuupa mwili kisogo,
Mungu atakuamini na kazi muhimu
kukuwezesha kumtumikia.
III
Katika barabara ya kwenda Yerusalemu,
Moyo wa Yesu ulihisi uchungu.
Hata hivyo, Aliweka ahadi Yake, akaendelea mbele
kuelekea pale ambapo Angesulubiwa.
Mwishowe Alisulubiwa msalabani,
Akawa mfano wa mwili wa dhambi,
Akikamilisha kazi ya ukombozi,
Akashinda pingu za kifo.
Ikiwa kama Yesu utamjali Mungu kabisa
na kuupa mwili kisogo,
Mungu atakuamini na kazi muhimu
kukuwezesha kumtumikia.
IV
Yesu aliishi kwa miaka thelathini na mitatu,
akifanya yote kumridhisha Mungu,
kamwe kutofikiria hasara au faida
bali mapenzi ya Mungu Baba.
Huduma ya Bwana Yesu
ilikuwa daima kulingana na mapenzi ya Mungu.
Hivyo mzigo wa ukombozi
Alikuwa na sifa za kutimiza.
Maumivu yasiyo na mwisho Alivumilia,
na mara nyingi Shetani alimjaribu.
Hata hivyo Hakufa moyo kamwe.
Kwa imani na upendo, Mungu Alimpa kazi hii.
Ikiwa kama Yesu utamjali Mungu kabisa
na kuupa mwili kisogo,
Mungu atakuamini na kazi muhimu
kukuwezesha kumtumikia.
(Kumaliza)
Na ni nyakati kama hizi tu
ndipo utathubutu kusema unafanya mapenzi Yake,
unakamilisha agizo Lake,
kwamba kweli unamtumikia Mungu.
kutoka katika "Jinsi ya Kuhudumu kwa Upatanifu na Mapenzi ya Mungu" katika Neno Laonekana katika Mwili

kutoka kwa Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya

Kuhusu Sisi: Umeme wa Mashariki Hutoka wapi?

0 意見:

Chapisha Maoni