Ijumaa, 18 Januari 2019

Ni Wale Wanaokubali Ukweli Tu Ndio Wanaweza Kuisikia Sauti ya Mungu

I
Palipo na kuonekana kwa Mungu,
kuna maonyesho ya ukweli na sauti ya Mungu.
Ni wale tu wanaokubali ukweli
ndio wanaweza kusikia sauti ya Mungu na kushuhudia kuonekana Kwake.
Ondoa maoni ya "haiwezekani"!
Mawazo ya kutowezekana yanaweza kutokea.
Hekima ya Mungu inapaa juu kuliko mbingu.
Mawazo Yake na kazi Yake ni zaidi ya mawazo yote ya mwanadamu.
Kadiri kitu kisivyowezekana, ndivyo kulivyo na ukweli wa kutafuta zaidi.
Kadiri kinavyozidi dhana ya mwanadamu, ndivyo kilivyo na mapenzi ya Mungu zaidi.
Haijalishi ni wapi Anakoonekana, Mungu bado ni Mungu, Mungu bado ni Mungu.
Na kiini Chake hakitabadilika kamwe kwa sababu ya wapi au jinsi ambavyo Ameonekana.
Weka mawazo yako kando, utulize moyo wako, soma maneno haya.
Ukitamani sana ukweli, Mungu ataruhusu ujue mapenzi na maneno Yake.
II
Tabia ya Mungu inabaki vile vile.
Popote zilipo hatua Zake, Yeye ni Mungu wa wanadamu.
Yesu ni Mungu wa Waisraeli wote, Mungu wa Asia, Ulaya, na ulimwengu mzima.
Tafuta mapenzi ya Mungu kutoka kwa matamshi Yake,
gundua kuonekana Kwake, fuata nyayo Zake.
Mungu ni ukweli, njia, uzima.
Maneno Yake na kuonekana vipo kwa wakati mmoja.
Tabia na nyayo Zake daima huwekwa wazi kwa mwanadamu.
Ndugu, tumaini kuwa mnaweza kuona kuonekana kwa Mungu katika maneno haya.
Mfuate kuelekea enzi mpya, hadi katika mbingu na dunia mpya
ambazo zimeandaliwa kwa wale wote wanaongojea kuonekana kwa Mungu.
Weka mawazo yako kando, utulize moyo wako, soma maneno haya.
Ukitamani sana ukweli, Mungu ataruhusu ujue mapenzi Yake.
Weka mawazo yako kando, utulize moyo wako, soma maneno haya.
Ukitamani sana ukweli, Mungu ataruhusu ujue mapenzi na maneno Yake.
kutoka katika "Kuonekana kwa Mungu Kumeleta Enzi Mpya" katika Neno Laonekana katika Mwili


kutoka kwa Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya

Kuhusu Sisi: Umeme wa Mashariki Hutoka wapi? Sikiliza nyimbo nyimbo za dini

0 意見:

Chapisha Maoni