Jumamosi, 12 Januari 2019

Mabadiliko Katika Tabia Hayatengani na Maisha Halisi

Katika kumwamini Mungu,
ikiwa mtu anatamani kuwa na mabadiliko,
basi haipaswi kujitenga mwenyewe
kutoka kwa maisha halisi ambayo yeye yumo ndani.
I
Ikiwa unalenga nadharia
na sherehe ya dini,
bila kuingia katika maisha halisi,
huwezi kuingia katika uhalisi,
hutawahi kujijua mwenyewe,
wala hutawahi kujua ukweli au Mungu,
daima utakuwa mjinga,
utakuwa daima kipofu.
Katika maisha halisi, ujijue mwenyewe,
ujiache na utende ukweli,
ujifunze sheria na akili ya kawaida
ya tabia binafsi katika kila kitu,
hivyo basi unaweza kufikia
mabadiliko ya taratibu,
mabadiliko ya taratibu.
II
Wale wasiomtii Mungu
hawawezi kuingia katika maisha halisi.
Wote wanazungumza kuhusu ubinadamu,
lakini wao ni kama pepo.
Wote wanazungumza kuhusu ukweli,
lakini badala yake wanaishi kwa kudhihirisha mafundisho.
Wale ambao hawawezi kuishi ukweli katika maisha halisi
hukataliwa na Mungu.
Katika maisha halisi, ujijue mwenyewe,
ujiache na utende ukweli,
ujifunze sheria na akili ya kawaida
ya tabia binafsi katika kila kitu,
hivyo basi unaweza kufikia
mabadiliko ya taratibu,
mabadiliko ya taratibu.
III
Tenda uingiaji wako mwenyewe,
jua upungufu wako na kutotii kwako,
jua ubinadamu wako usio wa kawaida,
jua udhaifu na kutojua kwako.
Hivyo maarifa yako
yanajumuishwa na hali yako ya kweli.
Maarifa haya tu ndiyo ya kweli,
yanakuruhusu kuelewa hali yako
na kufanikisha mbadiliko.
Katika maisha halisi, ujijue mwenyewe,
ujiache na utende ukweli,
ujifunze sheria na akili ya kawaida
ya tabia binafsi katika kila kitu,
hivyo basi unaweza kufikia
mabadiliko ya taratibu,
mabadiliko ya taratibu.
kutoka katika "Kujadili Maisha ya Kanisa na Maisha Halisi" katika Neno Laonekana katika Mwili
kutoka kwa Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya
Sikiliza nyimbo: nyimbo za injili, Nyimbo ya Msifuni Mwenyezi Mungu 

0 意見:

Chapisha Maoni