Jaweni na Upendo kwa Ajili ya Mungu | Muziki wa Akapela "Yasifu Maisha Mapya"

Haleluya! Twakushukuru na kukusifu Wewe, Mwenyezi Mungu! Kristo wa siku za mwisho ameonekana, akifanya kazi na kuzungumza miongini mwa wanadamu. Neno lake hutuhukumu, kutuadibu na kututakasa, likituongoza kwenye njia sahihi ya maisha ya binadamu.

Ukaribisheni Urejeaji wa Bwana Yesu | Sifa na Ibada “Mungu Ameleta Utukufu Wake Mashariki”

Mungu aliipa Israeli utukufu Wake kisha Akauhamisha mbali na pale, na kuwaleta Waisraeli na kuwaleta watu wote Mashariki. Mungu amewaelekeza wote kwenye mwanga ili waweze kuungana tena na kuwa pamoja na mwanga, wasilazimike kuutafuta tena, kuutafuta mwanga.

Je, Biblia ndiye Bwana, au ni Mungu? | “Bwana Wangu Ni Nani” ( Filamu za Injili )

Liu Zhizhong ni mzee katika kanisa moja la mtaani la nyumba nchini China. Amekuwa muumini kwa zaidi ya miaka 30, na amesisitiza bila kukoma kwamba “Biblia ni ufunuo wa Mungu,” “Biblia inamwakilisha Mungu, kuamini katika Mungu ni kuamini katika Biblia, kuamini katika Biblia ni kuamini katika Mungu.”

Karibu Kurudi kwa Bwana Yesu | Drama ya Muziki “ Kwaya ya Injili ya Kichina Onyesho la 19” | Haleluya

Mungu ametutunza daima–Yeye amesikiliza maombi yetu! Anajua tumekuwa tukitamani kurejea Kwake! Sasa kwa hakika Amerejea! Tunasubiri nini bado? Tafadhali endelea kutazama drama yenye muziki ya Kanisa la Mwenyezi Mungu—Kila Taifa Humwabudu Mungu wa Vitendo!

NYENDO ZA MATESO YA KIDINI NCHINI CHINA (Christian Videos) swahili

Wakristo wanaoteswa katika filamu hii ni watu kutoka kwa vikundi vya kidini na madhehebu tofauti ambao walitafuta ukweli, na ambao waliisikia sauti ya Mungu na hivyo wakarudi kwa Mwenyezi Mungu.

Inaonyesha machapisho ya hoja yaliyopangwa kwa uhusiano ukweli. Panga kwa tarehe Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho ya hoja yaliyopangwa kwa uhusiano ukweli. Panga kwa tarehe Onyesha machapisho yote

Jumapili, 3 Juni 2018

Sura ya 10. Wale Wanaopenda Ukweli Wana Njia ya Kufuata



Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Mungu

Sura ya 10. Wale Wanaopenda Ukweli Wana Njia ya Kufuata

1. Kama hali ya Watu Ni Ya Kawaida Inategemea na Kama Wanapenda Ukweli au La

Mwenyezi Mungu alisema, Watu wengi wameibua suala lifuatalo: Baada ya ushirika wa juu, wanahisi wazi kabisa, wanakuwa na nguvu zaidi, na hawana hisia hasi—lakini hali kama hiyo inabaki tu kwa karibu siku kumi, ambapo baadaye hawawezi kudumisha hali ya kawaida. Suala ni nini? Je mmewahi kujiuliza kinachosababisha hili? Mbona hali zenu ni nzuri sana katika siku hizo takriban kumi za kwanza? Wengine wanasema kuwa hili ni tokeo la kutolenga ukweli. Lakini hivyo ungeweza vipi kufikia kiwango hiki cha kawaida baada ya kusikia ushirika? Mbona ulikuwa na furaha sana baada ya kuusikia ukweli? Wengine wanasema ni kwa sababu ya kazi ya Roho Mtakatifu.

Jumapili, 26 Novemba 2017

Kukubali Ukweli kwa Hakika Ni Nini?

 Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, ukweli,

53. Kukubali Ukweli kwa Hakika Ni Nini?

Xiaohe Mji wa Puyang, Mkoa wa Henan
Hapo awali, kila wakati niliposoma maneno yaliyofichuliwa na Mungu kuhusu jinsi watu hawakubali ukweli, sikuamini kwamba maneno hayo yangetumika kwangu. Nilifurahia kula na kunywa neno la Mungu na kuwasiliana kuhusu neno la Mungu, na niliweza kukubali na kukiri kila kitu ambacho Mungu amesema kuwa ukweli—bila kujali jinsi kilivyoumiza moyo wangu au jinsi hakikuambatana na mawazo yangu. Aidha, bila kujali kiwango cha dosari kaka na dada zangu wangeonyesha, ningekikiri na kukikubali.

Ijumaa, 22 Juni 2018

59. Uzoefu wa Kutenda Ukweli

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Kanisa

59. Uzoefu wa Kutenda Ukweli

Hengxin     Jiji la Zhuzhou, Mkoa wa Hunan
Sio muda mrefu mno uliopita, nilisikia "Ushirika na Kuhubiri Kuhusu Kuingia kwa Maisha," jambo ambalo lilinielekeza kuelewa kwamba ni wale tu wanaotenda ukweli wanaoweza kupata ukweli na hatimaye kuwa wale ambao wanaomiliki ukweli na ubinadamu hivyo kupata kibali cha Mungu. Kuanzia hapo kwendelea, kwa makusudi nilifanya jitihada za kuunyima mwili wangu na kutenda ukweli katika maisha yangu ya kila siku. Wakati fulani baadaye, nilitambua kwa furaha kwamba ningeweza kutenda ukweli kiasi. Kwa mfano, siku za nyuma niliogopa kuonyesha upande wangu mwovu kwa wengine. Sasa kwa makusudi nilikuwa wazi na ndugu wa kiume na wa kike, nikichangua tabia yangu potovu.

Jumanne, 20 Februari 2018

Tendeni Ukweli Mara Mnapouelewa

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Mwenyezi Mungu,

Tendeni Ukweli Mara Mnapouelewa

Mwenyezi Mungu alisema, Kazi na neno la Mungu vina maana ya kuleta mabadiliko katika tabia zenu; lengo Lake si kuwafanya tu kulielewa au kulitambua na kufanya hilo kuwa mwisho wa jambo hilo. Kama mmoja wa uwezo wa kupokea, hampaswi kuwa na ugumu katika kuelewa neno la Mungu, kwa kuwa wingi wa neno la Mungu limeandikwa kwa lugha ya kibinadamu ambayo ni rahisi sana tu kuelewa.

Ijumaa, 23 Machi 2018

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Wale Waliofanywa Kuwa Watimilifu Ndio Tu Wanaoweza Kuishi Maisha Yenye Maana

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Mwenyezi Mungu,
Mwenyezi Mungu alisema, Kwa kweli, kazi inayofanywa sasa ni kuwafanya watu kumtoroka Shetani, kutoroka babu zao wa kale. Hukumu zote kwa neno zinalenga kufichua tabia potovu ya binadamu na kuwawezesha watu kuelewa kiini cha maisha. Hukumu hizi zote zilizorudiwa zinapenyeza mioyo ya watu.

Ijumaa, 11 Mei 2018

34. Kupata Ahueni kwa Njia ya Kumwamini Mungu

34. Kupata Ahueni kwa Njia ya Kumwamini Mungu

Zhuanbian     Mji wa Shanghai
Ingawa nilikuwa nikimfuata Mungu kwa miaka mingi, nilikuwa karibu sijafanya maendeleo yoyote na kuingia kwangu katika maisha, na hii ilinifanya nihisi kuwa na wasiwasi sana.

Jumanne, 5 Juni 2018

Sura ya 11. Kutatua Asili na Kutenda Ukweli

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Roho Mtakatifu

Sura ya 11. Kutatua Asili na Kutenda Ukweli

1. Uhusiano Kati ya Ubinadamu na Uwezo wa Kutenda Ukweli

Mwenyezi Mungu alisema, Watu husema kuwa kutenda ukweli ni vigumu kabisa. Basi mbona watu wengine wanaweza kutenda ukweli? Watu wengine husema ni kwa sababu kwa asili wanaipokea kazi ya Roho Mtakatifu ikifanya kazi juu yao, na pia kwa sababu ni wazuri kiasili. Hoja hii ina kiwango fulani cha mantiki. Watu wengine ni wazuri kiasili; wana uwezo wa kutenda ukweli. Ubinadamu wa watu wengine ni mnyonge, hivyo ni vigumu kwao kutenda ukweli; hii inamaanisha kuwa watakumbana na matatizo fulani.

Jumatatu, 3 Juni 2019

Uso halisi wa Mtu Anayedaiwa Kuwa Mtu Mzuri

Kemu Jiji la Zhumadian, Mkoa wa Henan
Katika mawazo yangu mwenyewe, daima nimejifikiria kuwa na ubinadamu mzuri. Nimefikiria hivi kwa sababu, majirani zangu mara nyingi walinisifu mbele ya wazazi wangu kwa kuwa mwenye busara na wa kuijali familia yetu; wakisema kuwa mimi nilikuwa kipenzi cha wazazi wangu. Baada ya kuolewa, wakwe zangu walinishukuru mbele ya majirani kwa kuwa wema na mtoto wao. Katika mahali pangu pa kazi, kiongozi wangu alinisifu kwa kuwa mwaminifu na mwenye ustadi. Na tangu nikubali kazi ya Mungu ya siku za mwisho, nimekuwa mtii kwa chochote kanisa huniomba kufanya. Huwa sipingani kamwe na kiongozi hata nikikemewa na kiongozi huyu kwa kutofanya kazi nzuri, na mara nyingi mimi huwasaidia ndugu wa kiume na wa kike walio na mahitaji. Kwa hivyo, ninaamini kuwa mimi ni wa maana, mwenye huruma, na mtu mwema mwenye ubinadamu. Sijawahi kujifikiria mwenyewe kwa njia ya maneno ambamo Mungu hufichua kuwa mwanadamu hana ubinadamu au kwamba mtu ana ubinadamu dhaifu. Wakati wa kuwasiliana maneno ya Mungu na ndugu wa kiume na wa kike, ingawa najua nahitaji kuwa na ufahamu wa asili yangu mwenyewe, bado mimi hudumisha mtazamo wangu mwenyewe, nikifikiria moyoni mwangu: Hata kama mimi si mtu wa ubinadamu mzuri, bado nina ubinadamu bora kiasi ukilinganisha na wengine. Aidha, bila kujali neno la Mungu linavyosema au kile ndugu wa kiume na wa kike wanavyosema, siko tayari kujitenga na wazo la kuwa mtu wa ubinadamu mzuri.
Siku moja, nilipokuwa nikila na kunywa neno la Mungu, kifungu kimoja kilivuta nadhari yangu. Mungu anasema, “Watu wengine ni wazuri kiasili; wana uwezo wa kutenda ukweli. Ubinadamu wa watu wengine ni mnyonge, hivyo ni vigumu kwao kutenda ukweli … Je, mnaweza kusema kuwa yule ambaye hatendi ukweli amewahi kuutafuta ukweli katika matendo yake? Hajautafuta kabisa. Fikira zake binafsi hutokea: ‘Njia hii ni nzuri, ni kwa faida yangu.’ Mwishowe, anatenda kulingana na mawazo yake binafsi. Hatafuti ukweli kwa sababu kuna kitu kisicho sawa na moyo wake, moyo wake hauko sawa. Hatafuti, hachunguzi, wala haombi mbele za Mungu; anatenda tu kwa ukaidi kulingana na matakwa yake. Mtu wa aina hii hana upendo wa ukweli kabisa. … Wale wasio na upendo kwa ukweli hawatautafuta katika wakati huo, wala hawatajichunguza baadaye. Kamwe hawachunguzi kama mambo wanayoyatenda ni sawa ama yenye makosa hatimaye, hivyo wanakiuka kanuni kila wakati, wanakiuka ukweli. … Mtu aliye na moyo anaweza kufanya makosa mara moja tu anapofuata utendaji, mara mbili kwa kiwango cha juu zaidi—mara moja ama mbili, sio mara tatu ama nne, hii ni akili ya kawaida. Kama anaweza kutenda makosa hayo sawa mara tatu ama nne, hii inathibitisha kuwa hana upendo wa ukweli, wala hautafuti ukweli. Mtu wa aina hii kwa waziwazi sio mtu mwenye utu” (“Kutenda Ukweli na Kutatua Asili” katika Kumbukumbu za Maongezi ya Kristo). Baada ya kusoma kifungu hiki cha maneno ya Mungu, nilikuwa na ufunuo wa ghafla. Inavyoelekea, ubinadamu mzuri au mbaya unahusiana kwa karibu na utekelezaji wa ukweli. Mtu wa ubinadamu mzuri atatafuta ukweli na kutenda ukweli katika kila kitu, na kujichunguza mwenyewe baadaye. Nimemejiona daima kuwa na ubinadamu mzuri, hivyo mimi ni mtu ambaye hutafuta na kutenda ukweli katika kila kitu? Nikifikiria nyuma, sikuomba au kutafuta ukweli kuhusu vitu vingi vilivyonikabili. Sikujichunguza au kujifahamu baadaye. Ingawa nilikuwa nimeonyesha tabia yangu potovu, sikutatua masuala yangu kwa kutafuta ukweli, lakini niliendelea kufanya kosa hilo hilo tena na tena. Wakati mwingine hata kama nilielewa kipengele kimoja cha ukweli, sikuonekana kutaka kukitenda. Nakumbuka mifano mingi ya jambo hili kwa dhahiri. Wakati mmoja, nakumbuka nikihisi hisi ya utengano na mtu niliyeshirikishwa naye. Nilikuwa na ufahamivu kuwa lingeathiri moja kwa moja matokeo yatakikanayo ya kazi ikiwa tatizo halikutatuliwa, lakini kwa sababu ya kiburi na majivuno yangu, nilikataa kuacha ubinafsi wangu na kuwa na mawasiliano ya wazi naye. Badala yake, nilistahimili jambo chungu lakini lisiloepukika na kuendelea kufanya kazi, na kusababisha kazi isiyofanikiwa sana. Wakati mwingine nilipoona ndugu wa kiume na wa kike wakifichua kipengele fulani cha hali yao potovu, sikujaribu kuwasiliana nao katika ukweli ili kuwasaidia kujijua, lakini badala yake niliwahukumu bila wao kujua. Sikutubu au kujaribu kubadilisha njia zangu hata baada ya kushughulikiwa mara chache, lakini badala yake niliendelea katika njia zangu za zamani. Sikujitahidi kupata matokeo mazuri mno katika kufanya kazi yangu, lakini daima nilikuwa mvivu na mjanja, nikishughulika na mambo kihobelahobela, daima nikimdanganya Mungu ili kudumisha nafasi yangu mwenyewe, bahati na hadhi. Sikuyapa umuhimu au kuwa na hisia ya hatia. Sikutafuta au kuchunguza mambo yalipotokea kazini mwangu, lakini nilifanya tu kama nilivyotaka. Hata kama ilileta hasara kubwa kwa kanisa, sikuhisi kama nilikuwa na deni kwa Mungu, wala sikuaibishwa na matendo yangu maovu. Hata kama Mungu alinikumbusha kupitia maneno Yake na kufichua upotovu wangu kwa njia ya kuwashughulikia na kuwapogoa ndugu, niliendelea kumpuuza Yeye, na kufanya makosa yale yale zaidi ya mara tatu au nne. Si vitendo hivi vinathibitisha kwamba nina ukosefu wa ubinadamu na mimi si mpenzi wa ukweli machoni pa Mungu? Bila kujali, sijajaribu kujijua kwa msingi wa asili yangu, lakini naendelea kuvaa laurusi ya “ubinadamu mzuri” juu ya kichwa changu. Nimekuwa mtovu wa haya jinsi gani!
Hivi sasa, moyo wangu umejaa hatia, na wakati huo huo umejaa shukrani kwa Mungu. Siwezi kujizuia kujimwaga mbele ya Mungu, “Mungu, asante kwa nuru Yako, kuniruhusu nijue kuwa mimi si mtu mwenye ubinadamu mzuri, kunisaidia kuelewa kuwa mtu mwenye ubinadamu wa kweli ni yule anayependa ukweli, ni mtu ambaye humsikiliza Mungu na kumtii Mungu, ni mtu ambaye yuko tayari kutenda ukweli na kufuatilia upendo wa Mungu. Mimi pia natambua ufahamu wangu juu yangu hautegemezwi kwa ukweli wa maneno ya Mungu, lakini umetegemezwa fikra zangu na dhana zangu, na vilevile maoni yangu ya kidunia. Ni upumbavu kabisa. Mungu, tangu sasa kuendelea, sitaki kujipima kulingana na mtazamo wa Shetani au mawazo yangu mwenyewe. Ninataka kujijua kwa msingi wa maneno Yako, na kufanya kila linalowezekana kufuatilia ukweli, ili hivi punde niweze kuwa mtu aliye na ukweli na ubinadamu ili kuufariji moyo Wako.”
Chanzo: Kanisa la Mwenyezi Mungu | Ushuhuda wa Kuipitia Hukumu ya Kristo

Jumanne, 1 Mei 2018

64. Huku Ni Kuweka Ukweli Katika Vitendo

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, hukumu

64. Huku Ni Kuweka Ukweli Katika Vitendo

Fan Xing    Mji wa Zhumadian, Mkoa wa Henan
Katika siku za nyuma, nilikuwa nimeunganishwa na dada mmoja kufanya kazi kwa wajibu fulani. Kwa sababu nilikuwa na majisifu na mwenye kiburi na sikutafuta ukweli, nilikuwa na mawazo kiasi ya kabla kuhusu dada huyu ambayo niliweka moyoni mwangu daima na sikuzungumza waziwazi naye. Tulipotengana, sikuwa nimeingia katika ukweli wa uhusiano wa kufanya kazi wenye kuridhisha.

Jumanne, 27 Machi 2018

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Unapaswa Kuzingatia Matendo Yako

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Mwenyezi Mungu,

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Mnapaswa Kuzingatia Matendo Yenu

Kulingana na vitendo na matendo katika maisha yenu, nyote mnahitaji kurasa za maneno ya kuwajaza na kuwajenga kila siku, kwani mko na upungufu mno, na ujuzi na maarifa yenu ya kupokea ni ya hali ya chini sana. Katika maisha yenu ya kila siku, mnaishi katika hali na mazingira yasiyo na ukweli ama fahamu nzuri.

Alhamisi, 10 Januari 2019

Umeme wa Mashariki | Njia ya Kutafuta Ukweli

I
Hali yako ina ushawishi katika jinsi unavyouelewa ukweli?
Wewe hushangaa katika mapambano ni ukweli upi ambao ni wa kweli?
Basi tafuta ukweli huu na utaona mapenzi ya Mungu katika yote ufanyayo.

Jumanne, 29 Mei 2018

Sura ya 21. Ukimbizaji Ukweli Tu Ndiyo Imani ya Kweli katika Mungu


Sura ya 21. Ukimbizaji Ukweli Tu Ndiyo Imani ya Kweli katika Mungu

Mwenyezi Mungu alisema, Kama huna uzoefu wa kitu, basi wewe hakika hutajua jinsi ya kukisimamia na utakisimamia vibaya. Hata kama unakisimamia, na ufikiri: “Mimi nimeeleza kiasi haya yote na nikasema mengi kulihusu. Wao pia wamelisikiza mara nyingi. Nimeongea sana kulihusu. Yote ambayo nimeshiriki kuhusu tatizo hili kimsingi ni kweli, sivyo?” lakini kwa kweli, yote tu ni mafundisho, na wewe unatumia mafundisho kutatua tatizo. Mbona unasema ni mafundisho? Kila neno unalosema ni sahihi, lakini kile unachosema hakijaelekezwa kwa tatizo na hakifikii kiini cha tatizo hili–ambapo tatizo hili lipo, shida yake ni nini, kwa nini hawa watu wanaweza kufanya mambo kama hayo au ni hali gani imejitokeza ndani yao. 

Jumapili, 20 Mei 2018

70. Kazi ya Mungu ni Ya Hekima Sana!

70. Kazi ya Mungu ni Ya Hekima Sana!

Shiji    Jiji la Ma’anshan , Mkoa wa Anhui
Wakati wa kufanya kazi kwangu kama kiongozi katika kanisa, kiongozi wangu mara nyingi angeshirikiana mifano ya kushindwa kwa wengine ili kutumikia kama somo kwetu. Kwa mfano: Viongozi wengine walizungumza tu kuhusu elimu na mafundisho lakini walikosa kutaja upotovu wao au kuwasiliana kwa karibu kuhusiana na ufahamu wao wa jinsi ukweli unavyotumika kwa ukweli. 

Jumanne, 14 Agosti 2018

Utakapouona Mwili wa Kiroho wa Yesu ndio Utakuwa Wakati Ambao Mungu Ametengeneza Upya Mbingu na Dunia

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Mwenyezi Mungu,,

Utakapouona Mwili wa Kiroho wa Yesu Ndio Utakuwa Wakati Ambao Mungu Ametengeneza Upya Mbingu na Dunia

Je, ungependa kumwona Yesu? Je, ungependa kuishi na Yesu? Je, ungependa kusikia maneno yaliyonenwa na Yesu? Iwapo ni hivyo, basi utakaribishaje, kurudi kwa Yesu? Je, uko tayari kabisa? Utakaribisha kurudi kwa Yesu kwa namna gani? Nafikiri kuwa kila ndugu na dada wanaomfuata Yesu wangependa kumpa Yesu makaribisho mazuri.

Ijumaa, 7 Juni 2019

Ni kwa Kuingia Katika Ukweli Mimi Mwenyewe tu Ndio Ninaweza Kuwasaidia Wengine

Ushuhuda wa Maisha, Wakristo, Kanisa la Mwenyezi Mungu

Du Fan Mkoa wa Jiangsu
Hivi karibuni, kanisa moja lilikuwa linakipiga kura ili kumchagua kiongozi mpya, lakini kiongozi aliyeongoza alienda kinyume na kanuni za kanisa, akitumia njia yake mwenyewe kutekeleza upigaji kura. Wakati ndugu fulani wa kiume na wa kike walipotoa maoni yao, sio tu kwamba hakuyakubali, lakini alisisitiza kushikilia njia yake mwenyewe. Baadaye kanisa lilitupwa katika mchafuko kwa ajili ya vitendo vya kiongozi huyo. Nilipopata kujua, nilikasirika kabisa: Mtu anawezaje kuwa mwenye kiburi mno na wa kujidai? Kutekeleza wajibu wa kiongozi wa kanisa bila Mungu ndani ya moyo wake, kuangalia kwa dharau mipango ya kazi, kupinga na kukataa mapendekezo ya ndugu wa kiume na wa kike—ni nani mwingine wa kulaumiwa kwa mchafuko wa kanisa ila wewe! Papo hapo nilimtuma mtu kuwasiliana kwa karibu na kiongozi wa kanisa na, wakati ule ule, nikapitia neno la Mungu kutafuta ukweli unaohusika ambao ningeuibua na kiongozi ili kumridhisha kuhusu makosa yake. Baadaye usiku huo, nilikwenda na kukutana na kiongozi. Wakati wa ushirika, nikamwambia kwa sauti ya mashtaka, nikishindwa kuzuia hasira yangu mwenyewe. Nilishangaa kuwa, dakika kumi katika mkutano wetu, kiongozi ghafla aliinuka na kutimua nje akiwa na machozi machoni mwake. Ndugu aliyekuwa ameenda kumfuata alirudi baadaye kidogo na kusema, “Amekwenda na anajua amefanya makosa.” Nilikuwa siachilii, nikiguta kwa hasira: “Kuhusu suala muhimu jinsi hii la kanuni, uko tayari kuacha mambo tu kama hayajatatuliwa? Jinsi wewe ulivyo mwenye kiburi mno na wa kujidai! Unaenda kinyume na kanuni za kanisa na humruhusu mtu mwingine awe na maoni. Je! Unapaswaje kupata kitu chochote kifanywe wakati ujao? Ni matarajio ya hatari kweli! Hili halitakuwa sawa hasa, kama utatoka nje kwa hasira bila kusema, itanilazimu kukuandikia barua tu.” Papo hapo, nikaketi na kumwandikia barua ambamo kwa ishara nilikubali kuwa mtazamo wangu katika ushirikiano haukuwa bora na nikauliza msamaha wake. Katika barua hiyo, nilizungumzia pia masuala yake, nikitoa mfano wa kanuni ili kutambua tatizo hilo. Nilidhani kwamba nilikuwa nimeyashughulikia mambo vizuri sana. Kwa upande mmoja, nilionyesha kuwa niliweza kuacha ubinafsi wangu mwenyewe na kupata ufahamu wa kina kujihusu, wakati huo huo nikitumia ukweli kutatua masuala. Baada ya kuona jinsi nilivyoshughulikia mambo, kiongozi huyu bila shaka angeridhika na kupata ufahamu mpya, nilifikiri.
Siku moja, nilipokuwa nikiwasiliana kwa karibu juu ya jambo hili na kiongozi wangu, kiongozi aliniuliza jinsi nilivyoingia katika ukweli wakati wa kutatua suala hili. “Niliingiaje katika ukweli? Nilifanya kazi mbaya? Je! Matendo yangu yalikuwa yasiyofaa?” Nilijihisi kuchanganyikiwa kidogo. Kiongozi huyo aliendelea: “Sio suala la jinsi ulivyotatua suala hili vizuri, lakini badala yake, katika kutatua suala hilo, je, ulilitumia hadhi yako na uwezo kuwashawishi wengine au ulitumia ukweli kumkuza na kumshuhudia Mungu, na kuwaruhusu wengine kupata kujijua kwa kina? Kwa juu, inaonekana kama kwamba wewe ulikuwa ukiwasiliana kwa karibu katika neno la Mungu, lakini kwa kweli ulikuwa unajaribu kumfanya ashindwe na mtazamo wako tu. Kwa nini aliishia kwenda? Ni wazi kuwa aliondoka kwa sababu hakuweza kukubali hoja yako, hakuridhika. Kama tunajishughulisha tu na kuwasiliana ukweli kwa karibu na wengine na kupuuza kuzingatia upotovu wetu wenyewe, kupuuza kujijua wenyewe, na kufanya kazi kwa ajili ya kuifanya tu, huenda tusijifunze chochote kipya na kutopata mabadiliko yoyote katika tabia yetu wenyewe. Kwa maana hii, si sisi ni kama Paulo, ambaye alitoa mwongozo kwa wengine lakini, ambaye, katika huduma ya Mungu, alijishikilia zaidi njia zake potovu? Katika kiburi chake, akawa mtu ambaye alimwamini Mungu na bado alimpinga Mungu, akifikia mwisho wake kwa kuangamia kabisa.” Ushirika huu ulikuwa kama wito ukinitikisa kutoka kwa usingizi mrefu. Kweli, wakati Mungu alileta hali hii kwangu, sikutafuta ukweli au kutafuta nia ya Mungu, sikufikiria jinsi ya kuingia katika ukweli mwenyewe au kutafakari juu ya majibu yangu mwenyewe yenye mhemko kwa hali hiyo. Yote niliyoweza kufanya ilikuwa ni kufikiria jinsi ya kutatua matatizo ya watu wengine. Kwa maana hii, nilikuwa nikizingatia hamu ya Mungu ya kuwaleta wengine mbele Yake? Au badala yake nilikuwa nikitumia hadhi yangu kuwalazimisha wengine kuukubali mtazamo wangu? Nilipotoshwa na Shetani, bila ukweli, ubinadamu au sababu. Mimi pia nilikuwa mwathiriwa. Nilikuwaje bora kuliko mtu mwingine yeyote? Sikuwa na maarifa ya binafsi, ufahamu wa ukweli. Bila kutambua, nilikuwa nimechukua sauti kali na kukasirika, nikiitukuza hadhi yangu katika kuwaonya wengine. Kiburi changu cha kishetani na majivuno vilikuwa vimefichuliwa! Wakati dada yangu alipotimua akilia, sikufikiria juu ya matendo yangu, badala yake nikimchukia na kukasirika sana. Je, si tabia yangu ilifanana na vitendo vya kikatili vya joka kubwa jekundu?
Namshukuru Mungu kwa ajili ya uongozi Wake. Uzoefu huu ulinipa nuru kwa umuhimu wa kuingia katika uhalisi wa ukweli. Ni kwa kuingia tu katika uhalisi wa ukweli tunapoweza kupokea ulinzi wa Mungu na kutompinga Mungu. Katika mahubiri ilisemwa: “Watu wengi hugeuka viongozi wa uongo au wapinga Kristo kwa sababu hawafuatilii ukweli kwa kweli na, kwa sababu hiyo, hawana uhalisi hata chembe wa ukweli. Mara tu wanapopata hadhi na kuwa na mamlaka fulani wao huanza kutenda kwa utukutu, kuwa juu zaidi ya wote, kujipa hadhi juu ya wengine na kutamani radhi ya hadhi. Mwishowe, watu kama hao huchukiwa sana na kukataliwa na wateule wa Mungu, hatimaye wakishindwa kabisa. Hili linaweza kuwa labda tukio adimu? Kwa nini watu hawawezi kujirudi? Kuna haja gani ya kumwamini Mungu ili kupata mamlaka tu, kushika madaraka na kutamani radhi ya hadhi? Hii ni tabia ya watu wa ubinafsi, duni na waovu, ni tamaa duni ya wale wanaoitembea njia ya mpinga Kristo” (“Unapaswa Kupata Uzoefu na Kuingia kwa Uhalisi wa Ukweli wa Neno la Mungu Ili Uweze Kupata Ukamilifu wa Mungu” katika Mkusanyiko wa Mahubiri—Ruzuku ya Maisha). Kupitia kifungu hiki niligundua kwamba wale ambao hawaingi katika ukweli, baada ya kupata hadhi, watajitangaza kuwa mfalme na kwa majivuno watatumia hadhi yao kuwakandamiza, kuwasingizia, na kuwadhibiti wengine. Hatimaye watakuwa viongozi wa uongo na wapinga Kristo. Sio mamlaka yaliyowaharibu watu hawa, lakini matokeo yasiyoepukika ya kushindwa kutafuta ukweli! Ingawa inaweza kuonekana kama uzoefu huu haukuwa mbaya sana, hali yangu ya akili na asili ya kweli katika kumpinga Mungu bila kukanushika inaashiria kwamba nilikuwa nikiitembea njia ya upinzani kwa Kristo. Kama sikuwa na mwelekeo wa Mungu, bila shaka singekuwa nimetambua upumbavu wangu na bado ningekuwa nikiishi katika hali ya kujidai. Kuendelea kupitia njia hiyo, hatimaye ningefichuliwa na kufutwa! Wakati ninapofikiria jinsi mambo yangeishia, jambo hili huniogofya. Jinsi niliyoitembelea nilivyopitia matatizo, nikimwamini Mungu kwa miaka mingi sana na bado kutoweza kujua jinsi ya kuingia katika uhalisi kama Paulo, ambaye aliishi ndani ya dhana ya kufikiriwa, lakini aliendelea kumwamini na kumtumikia Mungu kulingana na tabia yake ya kawaida na asili iliyopotoka. Nisipogeuza hali ya mambo ya leo, huenda nikajipata nimehukumiwa kwa laana ya milele. Katika siku zijazo, nahitaji kuweka umuhimu zaidi juu ya kuingia binafsi na ukimbizaji wa ukweli.
Muda mfupi baada ya haya yote kufanyika, nilipokea barua kutoka kwa dada ambayo ilianza kwa kusema kuwa alikuwa na shida kuelewa ukweli na kuomba mwongozo wangu. Baada ya kusoma barua hiyo, nilipandwa na hasira tena: Wewe ni mtu mwenye kiburi jinsi gani! Huwezi kushirikiana vizuri na hao viongozi wa kanisa na wafanyakazi. Kila wakati wanapokupa mapendekezo wewe hutoa tu udhuru, ukiendelea kufanya mambo kiholela. Kazi ya injili unayowajibikia haijafanikiwa na makanisa daima hutoa taarifa juu ya hali yako. Leo unaniandikia kuniuliza mwongozo: Una uhakika unaweza kukubali mwongozo wangu? Unafikiri kwamba kila kitu ambacho umekifanya kimekuwa cha kufaa na sawa na kushindwa kwako kote kumesababishwa na watu wengine kutoweza kutenda ukweli: Ni kiasi gani unajijua mwenyewe? … Jinsi nilivyozidi kufikiria, ndivyo nilivyozidi kukasirika, ningehisi miale ya ghadhabu ikiwaka moyoni mwangu: Si uliniomba nikupe mwongozo? Nimekuwa nikitaka kuzungumza nawe kwa muda sasa, leo hatimaye nina nafasi. Nikaandika kazi zangu za sasa na kuanza shughuli za kutafuta maneno ya Mungu yanayohusiana na hali yake ambayo ningeweza kudondoa ili kumshawishi. Ilielekea kwamba, nilivyozidi kutafuta vifungu vilivyofaa, ndivyo nilivyozidi kuvikosa—nilikanganyika na vilikopotelea vifungu vyote ambavyo kwavyo nilikuwa na ufahamu fulani. Nilipokuwa tu nimeanza kupata wasiwasi, ghafla nilihisi kufedheheka: Ni wapi unatafuta neno la Mungu? Hapa mtu huyu yuko mbele yako, huwa unaingiaje katika ukweli? Kwa nini daima unajaribu kutatua matatizo ya watu wengine? Umefichua nini ndani yako? Wakati huo, moyo wangu ulitulizwa na nikaanza kufikiria kwangu mwenyewe: Je! Umesahau tayari kilichotokea wakati wa mwisho? Usifanye kazi kwa ajili ya kufanya tu—tatua masuala yako mwenyewe kabla ya kujaribu kuwasaidia wengine. Wakati huu, nilifikiria nyuma kifungu hiki cha neno la Mungu: “Lazima kwanza utatue matatizo yote ndani yako kwa kumtegemea Mungu. Komesha tabia zako potovu na kuwa na uwezo wa kuelewa kweli hali zako mwenyewe na kujua jinsi unapaswa kufanya mambo; endelea kushiriki chochote ambacho hukielewi. Haikubaliki kwako kutojijua. Kwanza ponya ugonjwa wako mwenyewe, na kwa njia ya kula na kunywa maneno Yangu zaidi, kutafakari maneno Yangu, ishi maisha na fanya mambo kwa mujibu wa maneno Yangu; haijalishi ukiwa nyumbani au mahali pengine, unapaswa kumruhusu Mungu atwae nguvu ndani mwako. … Je, maisha ya mtu ambaye hawezi kuishi kwa kutegemea maneno ya Mungu yanaweza kukomaa? Hapana, hayawezi. Lazima uishi kwa kutegemea maneno Yangu kila wakati. Katika maisha, lazima maneno Yangu yawe kanuni yako ya vitendo. Yatakusababisha kuhisi kuwa kufanya mambo kwa njia fulani ni kile Mungu anafurahia, na kufanya mambo kwa njia nyingine ni kile Mungu anachochukia; polepole, utakuja kutembea katika njia sahihi” (“Sura ya 22” ya Matamko ya Kristo Mwanzoni katika Neno Laonekana katika Mwili). “Lazima uwe na ufahamu wa watu ambao huwa na ushirika nao na ushirika kuhusu masuala ya kiroho katika maisha, ni hapo tu unapoweza kuruzuku maisha kwa wengine na kufidia mapungufu yao. Hupaswi kuchukua sauti ya kuhubiri nao, ambao kimsingi ni msimamo mbaya kuwa nao. Katika ushirika ni lazima uwe na ufahamu wa mambo ya kiroho. Lazima uwe na hekima na kuwa na uwezo wa kuelewa ni nini kilicho katika mioyo ya watu wengine. Lazima uwe mtu mwafaka kama utawatumikia wengine na lazima ufanye ushirika na kile ulicho nacho” (“Sura ya 13” ya Matamko ya Kristo Mwanzoni katika Neno Laonekana katika Mwili). Maneno ya Mungu yalikuwa wazi kama ziwa la mlimani na yalinisaidia kutambua upungufu wangu mwenyewe: Wakati ninapokumbana na hali yoyote, huwa sina ufahamivu wangu kamwe na huwa siweki umuhimu wowote juu ya kile ninachokifichua ndani yangu. Kimsingi, sina Mungu ndani ya moyo wangu na sijui jinsi ya kumtegemea Yeye. Aidha, sielewi maneno mengi sana ya Mungu na siwezi kuona vitu au kutenda kulingana na maneno ya Mungu. Mungu hutaka kwamba tuishi kulingana na neno Lake wakati wote wa kila siku na kwamba tulichukue neno la Mungu kama mwongozo ambao tunapaswa kujiongozea. Yeye hutaka kwamba tufanye kile Anachopenda na kuacha kile ambacho hakiambatani na nia Yake. Je, si Mungu huyachukia yale niliyoyafichua kujihusu leo? Je, matendo yangu leo yalikuwa yakitimizaje wajibu wangu? Hapana, kwa dhahiri nilikuwa nikitenda uovu. Baadaye nilisoma “Kanuni za Kuwasaidia Wengine Kwa Moyo wa Upendo,” na kanuni ya kwanza ilisema: “Ni lazima utofautishe aina tofauti za watu kulingana na neno la Mungu. Kwa wale ambao kwa kweli humwamini Mungu na kuukubali ukweli, ni lazima uwasaidie kwa moyo wa upendo na uaminifu.” (Utendaji na Mazoezi kwa Mwenendo Wenye Maadili). Nilipata pia maneno haya ya Mungu, “Neno la Mungu linahitaji nini kama kanuni ya kuwatendea wengine? Kipende kile ambacho Mungu anapenda, kichukie kile ambacho Mungu anachukia. Hivyo ni kusema, watu wanaopendwa na Mungu ambao kweli hufuatilia ukweli na wanaofanya mapenzi ya Mungu, ndio watu ambao unapaswa kuwapenda. Wale ambao hawafanyi mapenzi ya Mungu, wale wanaomchukia Mungu, wale wasiomtii Mungu, na wale wanaodharauliwa na Mungu, ndio watu tunaopaswa kuwadharau na kuwakataa. Hicho ndicho neno la Mungu linahitaji” (“Ni kwa Kujua Maoni Yako Yaliyopotoka Tu Ndipo Unapoweza Kujijua Mwenyewe” katika Kumbukumbu za Maongezi ya Kristo). Kwa sababu Mungu anatupenda, Yeye huwa mwili na kujificha Mwenyewe kwa unyenyekevu, akifanya chochote ili kuuokoa binadamu wote. Yeye huchukia vipengele viovu vya wanadamu, lakini husikitikia udhaifu wao, bila kuwashughulikia watu kamwe kuhusu upotovu wao, lakini daima Akiwatia moyo watu kwa maonyo madogomadogo ya ari, mafundisho yasiyokwisha na upendo ili watambue makosa ya njia zao na kutafuta njia mpya ya kwendelea mbele. Mungu hunipa neema Yake, huniinua na kuniruhusu kutimiza wajibu huu ili niweze kupenda kile ambacho Mungu hupenda, kuwasaidia na kuunga mkono ndugu zangu wa kiume na wa kike kwa moyo wenye upendo wanapokabiliwa na shida na kuwatendea watu wote kwa moyo mwaminifu. Mimi, hata hivyo, nilikwenda kinyume na kanuni Zake: Kwa sababu tu nilikuwa na hadhi ndogo na niliona kuwa wengine walikuwa wameonyesha upotovu wao kiasi, nilikosa kuuhurumia udhaifu wao, lakini badala yake nilitumia neno la Mungu kama silaha ya kuwakandamiza na kuwalazimisha wakubaliane nami. Si hiki ni kitendo cha chuki? Kwa ghafla nilihisi kutahayarishika na kuaibika juu ya kiburi na ujinga wangu. Baadaye, nilisoma kifungu cha neno la Mungu kutoka kwa Kanuni ya 43, “Kanuni ya Kushiriki Kutoka Moyoni”: “‘Kushiriki na kuwasiliana kuhusu uzoefu’ kunamaanisha kuzungumza kuhusu kila wazo katika moyo wako, hali yako, uzoefu wako na maarifa ya maneno ya Mungu, na pia tabia potovu ndani yako—na baada ya hayo, wengine wanatofautisha, na kukubali mazuri na kutambua kile kilicho hasi. Huku tu ndiko kushiriki, na huku tu ndiko kuwasiliana kwa kweli” (“Ili Kuwa Mtu Mwaminifu, Unapaswa Kujiweka Wazi kwa” katika Kumbukumbu za Maongezi ya Kristo). Kupitia kula na kunywa neno la Mungu, nilijifunza jinsi ya kuwasiliana kwa karibu na dada yangu kwa namna ambayo ingekuwa ya manufaa kwake. Wakati huu, nilipochukua kalamu, nilihisi msisimko wa upendo ukifurika ndani yangu. Nilihisi hamu kubwa ya kuufunua moyo wangu katika majadiliano na dada yangu. Wakati huu, nilijadili utambuzi wangu juu ya tabia yangu yenye kiburi na asili yangu ya majivuno na katili—sikuwa nimewatendea ndugu wa kiume na wa kike kwa usahihi, nikikosa kuonyesha upendo na huruma kwao. Katika barua niliandika yafuatayo: Kwa hakika namshukuru Mungu kwa kukuweka mbele yangu, akiniruhusu kuona uovu ndani ya moyo wangu. Kama kiongozi, sina ukweli au uhalisi. Sistahili kuwa kiongozi, kwa sababu nilishindwa kuwajibikia wajibu ambao Mungu alinipa—nilishindwa kutenda kama mtumishi mbele ya Mungu. Badala yake, nilichukua wajibu wangu kama cheo cha mamlaka, hadhi, nikijiona kuwa juu ya wengine. Nilipoona barua yako, nilijaa dharau na hukumu, na hata nikaamini kwamba nilikuwa na mamlaka ya kukupogoa na kukushughulikia. Jinsi nilivyokuwa na kiburi na majivuno! Kwa ukweli, upungufu wako ulikuwa pia upungufu na makosa yangu. Wakati mimi na ndugu zangu wa kiume na wa kike hatuwezi kufanya kazi pamoja kwa mpangilio wa kuridhisha, huyu ni Mungu akionyesha ukweli kwamba maafa haya yote ya dhiki yalikuwa matokeo ya kutoweza kwangu kuingia katika ukweli kwa ushirikiano wenye kuridhisha. Asante Mungu kwa ufunuo huu, ambao ulinisaidia kutambua kwamba licha ya kumwamini Mungu kwa miaka mingi, bado sijapata ufahamu juu ya wokovu wa Mungu wa wanadamu. Bado sijaielewa nia ya Mungu katika kuwaokoa wanadamu. Sijui ni kwa njia gani mwanadamu anapaswa kuokolewa na kukamilishwa. Kutokana na haya, katika hali yoyote ninayoweza kuikabili, sijaweza bado kukubali hukumu na kuadibu kwa Mungu, kushughulikiwa na kupogolewa. Badala yake, daima mimi hugaagaa katika mambo ya juujuu. Kama haungekuwa umenituma barua hii kunifichua, singekuwa nimeona asili ya suala langu. Hebu sote tufanye mazoezi ya kuingia katika uhalisi wa ukweli siku zijazo.
Wakati kwa kweli nilipoiacha nafsi yangu, nikaja kujijua na kujichangua, na kutumia hali halisi ambayo nina uzoefu nayo kuwasiliana kwa karibu na kuingia katika ukweli na dada yangu, nilijihisi kuwa na mwenye hekima kabisa na kuwa na amani na kuona kuwa hakukuwa na umbali na utengano kati yetu. Kwa kweli niliona alama ya baraka ya Mungu katika hali ambazo nilitenda ukweli. Ni kwa njia ya mwongozo wa mfululizo wa Mungu na kupata nuru tu, ambapo mimi, ambaye ningeweza kuzungumza juu ya ukweli tu lakini sio kuutumia, ambaye nilipitia uzoefu kwa kutoonyesha hisia bila kuingia katika uhalisi wa ukweli, polepole nilianza kuboreka. Niliona tabia takatifu na ya haki ya Mungu katika uzoefu wangu wa zamani. Kama vile tu kifungu katika mahubiri kilisema, “Popote palipo na upotovu, patakuwa na hukumu, popote palipo na uovu, patakuwa na kuadibu” (“Zile Hatua Tatu za Kazi ya Mungu tu Ndizo Kazi Kamili ya Wokovu wa Wanadamu” katika Mkusanyiko wa Mahubiri—Ruzuku ya Maisha). Pia nilikuja kuwa na ufahamu zaidi na zaidi kwamba hukumu ya Mungu na adabu ndivyo tu tunavyovihitaji. Kupitia hukumu na kuadibu kwa Mungu ni zawadi ya wokovu mkubwa na neema. Ni kwa kupokea hukumu hii na kuadibiwa tu tunapoweza kupokonywa kutoka kwa ushawishi wa giza wa Shetani, tuondoe giza, tutafute mwanga na ukweli, tuingie katika ukweli, na tutende ukweli. Naomba kwamba hukumu na adhabu ya Mungu vinifuate popote nitakapokwenda, ili niweze kupata usafi na kuishi kama mwanadamu wa kweli.
Chanzo: Kanisa la Mwenyezi Mungu | Ushuhuda wa Kuipitia Hukumu ya Kristo

Ijumaa, 1 Juni 2018

Sura ya 9. Kutafuta Mapenzi ya Mungu na Kuuweka Ukweli Katika Vitendo Kwa Kiasi Kikubwa Zaidi Iwezekanavyo

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, ukweli

Sura ya 9. Kutafuta Mapenzi ya Mungu na Kuuweka Ukweli Katika Vitendo Kwa Kiasi Kikubwa Zaidi Iwezekanavyo

     Mwenyezi Mungu alisema, Punde tu watu wanapokuwa na haraka wakati wakiutumiza wajibu wao, hawajui jinsi ya kuuzoea; punde tu wanaposhughulika na mambo, hali yao ya kiroho inakuwa na matatizo; hawawezi kudumisha hali yao ya kawaida. Inawezekanaje kuwa hivi? Unapoombwa kufanya kazi kidogo, haufuati ukawaida, unakosa mipaka, husogei karibu na Mungu na unajitenga mbali na Mungu.Hili linadhibitisha kwamba watu hawajui jinsi ya kuwa na uzoefu. Haidhuru nini ufanyacho, unapaswa kwanza kuelewa halisi kwa nini unalifanya hili na asili ya jambo hili ni lipi. Ikiwa imepangwa kama kutimiza wajibu wako, basi unapaswa kutafakari: Nitalifanyaje hili? Nitatimizaje wajibu wangu vyema ili nisiwe nafanya kwa uzembe? Hili ni jambo ambalo kwalo unapaswa kusogea karibu na Mungu. Kusogea karibu na Mungu ni kutafuta ukweli katika jambo hili, ni kutafuta jinsi ya kutenda, ni kutafuta mapenzi ya Mungu, na ni kutafuta jinsi ya kumridhisha Mungu. Hizi ndizo njia za kusogea karibu na Mungu unapofanya vitu; sio kufanya sherehe za kidini au tendo lionekanalo kwa nje; inafanywa kwa kusudi la kutenda kulingana na kweli baada ya kufauta mapenzi ya Mungu.

Ijumaa, 11 Januari 2019

Matamshi ya Kristo | Kuwa Mtu Anayekubali Ukweli

I
Eh~ Chagua njia yako mwenyewe, usikatae ukweli
au kumkufuru Roho Mtakatifu.
Usiwe mjinga, usiwe na kiburi.
Tii mwongozo wa Roho Mtakatifu.

Jumapili, 15 Julai 2018

Tafakuri kuhusu Kubadilishwa

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu, ukweli,

Tafakuri kuhusu Kubadilishwa

Yi Ran    Mji wa Laiwu , Mkoa wa Shandong
Wakati fulani awali, kwa sababu yangu kutoelewa kanuni iliyotumiwa na kanisa ya masahihisho ya wafanyakazi wa kanisa, wakati kanisa lilibadilisha kiongozi, dhana iliibuka ndani yangu. Kutoka kwa kile nilichoweza kuona, dada aliyebadilishwa alikuwa mzuri sana kwa kupokea na kushirikiana ukweli, na aliweza kuwa wazi juu ya maonyesho yake ya upotovu. Kwa hiyo sikuweza kujua asilani jinsi mtu fulani aliyetafuta ukweli sana angeweza kubadilishwa. Inawezekana kwamba yeye alizungumza juu ya maonyesho yake mwenyewe ya upotovu sana, na hivyo kiongozi wake kwa makosa alimchukua kuwa mtu asiyefuatilia ukweli, na kumbadilisha? Kama hili ndilo lililotokea kweli, basi si fursa ya mafunzo kwa mtu ambaye alikuwa anafuta ukweli imeangamizwa?

Jumamosi, 10 Februari 2018

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Kwa Nini Nimetembea Njia ya Mafarisayo?

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, hukumu,

73. Kwa Nini Nimetembea Njia ya Mafarisayo?

Suxing Mkoa wa Shanxi
Mimi ni mtu mwenye kiburi na majivuno, na cheo kimekuwa udhaifu wangu. Kwa miaka mingi, nimefungwa na sifa na cheo na sijaweza kujiweka huru kutoka kwazo. Mara kwa mara nimepandishwa cheo na kubadilishwa na mtu mwingine; nimekuwa na vizuizi vingi katika cheo changu na nimekumbwa na matuta mengi njiani.

Jumatano, 27 Juni 2018

Sura ya 92. Njia ya Utendaji katika Kusuluhisha Ukaidi

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Mwenyezi Mungu

Sura ya 92. Njia ya Utendaji katika Kusuluhisha Ukaidi

Mwenyezi Mungu alisema, Mtu huwa na tatizo lipi anapopenda kupeana visingizio? Ni nini kiini chake? Yeye ni mkaidi. Watu wakaidi hawakubali ukweli kwa urahisi; sio watiifu, na wanaposikia neno moja ambalo haliambatani na dhana, mitazamo, wanayopenda, hisia au mihemko yao wenyewe, basi hawalikubali; husema, “Sijali iwapo liko sahihi au ni mbaya, ni nani aliyelinena, lilinenwa katika muktadha gani, au iwapo linahusiana na majukumu na wajibu wangu; siyajali mambo haya.