Jumapili, 6 Januari 2019

Kazi Ya Mungu Ikipingana na Fikira za Wanadamu Huwakamilisha Vyema Zaidi

I
Kama unamwamini Mungu, lazima umtii,
utende ukweli na kutimiza wajibu wako wote, aa, aa.
Lazima uelewe mambo unayopaswa kupitia.
Kama unapitia tu hukumu na nidhamu, aa, aa,
lakini huwezi kujua Mungu anapokushughulikia 
au kukufundisha nidhamu, basi hili halitoshi kamwe.
Haitoshi kustahimili usafishwaji katika jambo moja,
huna budi kuendelea kusonga, kuendelea kusonga.
We, kumpenda Mungu huendelea milele, ho, ho.
We, ni fundisho bila mipaka.
Kazi ya Mungu ilivyo ya ajabu zaidi katika mtu,
ndivyo ilivyo na thamani na maana zaidi.
Ndivyo inavyozidi kutoeleweka nawe,
ndivyo isivyolingana na fikira zako zaidi,
kazi ya Mungu inaweza kukushinda zaidi,
kukupata na kukukamilisha.
II
Mungu anapomsafisha mwanadamu, yeye hupitia mateso,
upendo kwa Mungu unakua, uwezo wa Mungu unaonekana zaidi katika mtu.
Lakini wakati usafishaji wa Mungu ni kidogo kwa mtu,
upendo wake ni fukara, nguvu za Mungu ndani yake dhaifu, aa, aa.
Lakini usafishwaji wake, uchungu na mateso vinavyozidi,
ndivyo atakavyozidi kumpenda Mungu sana, atampenda Mungu,
ndivyo imani yake katika Mungu itakavyozidi kuwa halisi,
ndivyo atakavyozidi kumjua Mungu sana, atamjua Mungu.
We, kumpenda Mungu huendelea milele, ho, ho.
We, ni fundisho bila mipaka.
Kazi ya Mungu ilivyo ya ajabu zaidi katika mtu,
ndivyo ilivyo na thamani na maana zaidi.
Ndivyo inavyozidi kutoeleweka nawe,
ndivyo isivyolingana na fikira zako zaidi,
kazi ya Mungu inaweza kukushinda zaidi,
kukupata na kukukamilisha.
III
Wale wanaopitia usafishwaji mkubwa na nidhamu,
humpenda Mungu sana, na kumjua zaidi.
Wale ambao hawajashughulikiwa hata mara moja
wana maarifa ya juujuu tu.
Baada ya kushughulikiwa na kufundishwa nidhamu,
watu wanaweza kuzungumzia maarifa halisi ya Mungu.
Kazi ya Mungu ilivyo ya ajabu zaidi katika mtu,
ndivyo ilivyo na thamani na maana zaidi.
Ndivyo inavyozidi kutoeleweka nawe,
ndivyo isivyolingana na fikira zako zaidi,
kazi ya Mungu inaweza kukushinda zaidi,
kukupata na kukukamilisha.
kutoka kwa "Ni Lazima Wale Wanaofaa Kufanywa Wakamilifu Wapitie Usafishaji" katika Neno Laonekana katika Mwili


kutoka kwa Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya


0 意見:

Chapisha Maoni