Jumatatu, 7 Januari 2019

Umeme wa Mashariki | Walio Gizani Wanapaswa Kuinuka

I
Kwa maelfu ya miaka,
hii imekuwa nchi ya taka,
chafu sana, taabu imesheheni,
na pepo wakitangatanga kwa kila pembe.
Pepo huhadaa, hudanganya,
hufanya mashtaka yasiyo na msingi,
ni wakatilii, waovu,
wakiukanyaga mji huu wa mahame,
wakiuacha kama umechafuliwa na maiti.
Sasa ndio wakati: Watu kwa muda mrefu
wamekusanya nguvu zao zote,
wakatoa juhudi zao zote,
kuukwanyua uso wa kutisha wa pepo huyu.
Hili litawawezesha wale waliopofushwa
waliovumilia kila aina ya mateso, shida,
kuinuka kutoka kwa maumivu yao
na kumkwepa huyu ibilisi muovu mkongwe.
II
Uvundo wa uozo unaenea kote.
Nchi hii imelindwa sana.
Nani anayeweza kuona ulimwengu mbele ya mbingu?
Watu wa mahame haya wangewezaje kumwona Mungu?
Wamewahi kufurahia mapenzi ya Mungu, uzuri?
Wao hufurahia masuala ya ulimwengu?
Ni nani kati yao anayejua mapenzi ya Mungu yenye shauku?
Sasa ndio wakati: Watu kwa muda mrefu
wamekusanya nguvu zao zote,
wakatoa juhudi zao zote,
kuukwanyua uso wa kutisha wa pepo huyu.
Hili litawawezesha wale waliopofushwa
waliovumilia kila aina ya mateso, shida,
kuinuka kutoka kwa maumivu yao
na kumkwepa huyu ibilisi muovu mkongwe.
III
Mbona kuweka kazi ya Mungu mbele ya kizuizi kisichopenyeka?
Mbona kutumia hila mbalimbali za kuwadanganya watu wa Mungu?
Uhuru wa kweli uko wapi, haki za kisheria na maslahi?
Haki iko wapi?
Faraja na wema mwingi viko wapi?
Mbona kutumia mipango ya ujanja kuwahadaa watu wa Mungu?
Mbona kutumia nguvu kama hiyo kuukandamiza ujio wa Mungu?
Sasa ndio wakati: Watu kwa muda mrefu
wamekusanya nguvu zao zote,
wakatoa juhudi zao zote,
kuukwanyua uso wa kutisha wa pepo huyu.
Hili litawawezesha wale waliopofushwa
waliovumilia kila aina ya mateso, shida,
kuinuka kutoka kwa maumivu yao
na kumkwepa huyu ibilisi muovu mkongwe.
IV
Mbona kumfuatafuata Mungu mpaka Hana pa kupumzisha kichwa Chake?
Kufanya hivi kungekosaje kuchochea ghadhabu?
Maelfu ya miaka ya chuki yamejaa ndani ya moyo,
milenia nyingi za uhalifu zimeandikwa juu ya moyo.
Haya yote yangekosaje kuchochea chuki?
Lipizia Mungu kisasi, maliza adui Wake kabisa.
Sasa ndio wakati: Watu kwa muda mrefu
wamekusanya nguvu zao zote,
wakatoa juhudi zao zote,
kuukwanyua uso wa kutisha wa pepo huyu.
Hili litawawezesha wale waliopofushwa
waliovumilia kila aina ya mateso, shida,
kuinuka kutoka kwa maumivu yao
na kumkwepa huyu ibilisi muovu mkongwe.
kutoka kwa "Kazi na Kuingia (8)" katika Neno Laonekana katika Mwili

 kutoka kwa Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya


0 意見:

Chapisha Maoni