Jumapili, 24 Februari 2019

Hakuna Anayeelewa Matamanio ya Mungu Yenye Bidii ya Kumwokoa Mwanadamu

I
Wakati wa kazi ya Mungu ya wokovu,
Atawaokoa wale wote Anaoweza kuwaokoa
kwa kiasi kikubwa mno iwezekanavyo,
na Hatamwacha yeyote.
Lakini wale wote wasioweza
kubadilisha tabia yao,
au kumtii Mungu kabisa
watakuwa walengwa wa adhabu.
Wote ambao wanakubali kushinda kwa maneno
watakuwa na nafasi nyingi za wokovu.
Wokovu wa Mungu utawaonyesha
huruma Yake kubwa sana na uvumilivu.
Watu wakirudi kutoka kwa njia mbaya,
wakitubu, Mungu atawapa fursa
kupata wokovu Wake.
II
Hatua hii ya kazi, kazi ya maneno,
inafungua tu kwa watu
njia zote na mafumbo
ambayo hawayaelewi.
Hili humsaidia mwanadamu kuyajua mapenzi ya Mungu
na matakwa ya Mungu kwa mwanadamu.
Kwa hiyo wanaweza kutenda maneno ya Mungu
na kubadilisha tabia yao.
Wote ambao wanakubali kushinda kwa maneno
watakuwa na nafasi nyingi za wokovu.
Wokovu wa Mungu utawaonyesha
huruma Yake kubwa sana na uvumilivu.
Watu wakirudi kutoka kwa njia mbaya,
wakitubu, Mungu atawapa fursa
kupata wokovu Wake.
III
Mungu anatumia maneno tu kufanya kazi Yake.
Huwa hawaadhibu watu
kwa sababu ya uasi wao mdogo,
kwani sasa ni wakati wa wokovu.
Wote wanaoasi wangeadhibiwa,
hakuna ambaye angekuwa na fursa ya kuokolewa.
Wote wangeadhibiwa
na wangeanguka Kuzimu.
Maneno yanayomhukumu mwanadamu humruhusu
kujijua na kumtii Mungu,
si kwa yeye kuadhibiwa
kwa hukumu ya maneno haya.
Wote ambao wanakubali kushinda kwa maneno
watakuwa na nafasi nyingi za wokovu.
Wokovu wa Mungu utawaonyesha
huruma Yake kubwa sana na uvumilivu.
Watu wakirudi kutoka kwa njia mbaya,
wakitubu, Mungu atawapa fursa
kupata wokovu Wake.
IV
Watu wanapomwasi Mungu kwanza,
Yeye hana shauku ya kuwaua,
lakini badala yake Yeye hufanya analoweza kuwaokoa.
Kama mtu hana nafasi ya wokovu, Mungu atamtelekeza.
Hana haraka ya kuadhibu kwani Anataka kuwaokoa
wote ambao wanaweza kuokolewa.
Wote ambao wanakubali kushinda kwa maneno
watakuwa na nafasi nyingi za wokovu.
Wokovu wa Mungu utawaonyesha
huruma Yake kubwa sana na uvumilivu.
Watu wakirudi kutoka kwa njia mbaya,
wakitubu, Mungu atawapa fursa
kupata wokovu Wake.
Yeye huwahukumu, huwatia nuru, huwaongoza watu Akitumia maneno tu,
sio kuwapiga kwa fimbo.
Kutumia maneno kuokoa ndilo kusudi,
maana ya hatua hii ya mwisho ya kazi.
kutoka katika "Mnapaswa Kuweka Pembeni Baraka za Hadhi na Kuelewa Mapenzi ya Mungu kwa ajili ya Wokovu wa Mwanadamu" katika Neno Laonekana katika Mwili

 kutoka kwa Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya

Kuhusu Sisi: Asili ya Kanisa la Mwenyezi Mungu


0 意見:

Chapisha Maoni